About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, January 19, 2015

DKT NCHIMBI; WANACCM WAJIPANGA SHEREHE ZA MIAKA 38 YA CCM TAIFA



MWENYEKITI WA KAMATI YA MAANDALIZI YA MAADHIMISHO YA MIAKA 38 YA CCM TAIFA DKT EMMANUEL NCHIMBI AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI SONGEA

NA, STEPHANO MANGO, SONGEA

WANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi Mkoani Ruvuma Wametakiwa kuendelea kujipanga Kikamilifu Katika Sherehe za Maadhimisho ya kutimiza miaka 38 ya kuzaliwa kwake ambayo yanatarajiwa kufanyika Katika Viwanja vya Majimaji Mjini Songea Februari 2 mwaka huu

Akizungumza na Waandishi wa Habari Jana katika Viwanja vya Ccm Mkoa wa Ruvuma Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Sherehe hizo za Maadhimisho ya miaka 38 Ccm Dkt Emmanuel Nchimbi alisema kuwa Maadhimisho hayo ni Muhimu sana kwani yanalenga zaidi kukumbuka toka kuzaliwa kwake hadi hapa kilipo hivyo wanaccm hawana budi kuhakikisha wanajipanga vizuri kufanikisha maadhimisho hayo

Dkt Nchimbi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo La Songea Mjini alisema kuwa Wanaccm wanatakiwa kutumia fursa hiyo muhimu kujiimarisha kiuchumi na kiutalii kwani kuwepo kwa wageni wengi wakati wa Maadhimisho hayo kutachangia ununuzi wa bidhaa mbalimbali ambazo zinazalishwa na Wajasiliamali Mjini hapa

Alisema kuwa Kitendo cha Viongozi Wakubwa  wa Ccm Taifa katika Vikao Vyao kuridhia kuwa Maadhimisho hayo Kufanyika Songea ni cha Busara sana hivyo Tunawajibika kujiandaa vyema kuwapokea Wageni na kufanya mambo ambayo yanaendana na maudhui ya Maadhimisho hayo

Alieleza kuwa Mwaka huu ni Mwaka wa Uchaguzi ni lazima wanachama na wapenzi wa chama hicho kuelezea mafanikio yaliyopatika katika miaka 38 ya kuzaliwa kwa chama hicho makini na kikubwa cha siasa nchini ambacho kinaongoza nchi kwa zaidi ya miaka 50 sasa

Alifafanua kuwa  Mafanikio ambayo chama hicho na kwa namana inavyotatua changamoto za Wananchi wake ndio msingi wa Vyama vya Upinzani Nchini kukionea  wivu na hata kukieneza vibaya katika mikutano yao ya hadhara

Hata hivyo amewataka Viongozi wote wa Jumuiya za Chama hicho kuendelea kujipanga ili kufanikisha Maadhimisho hayo  Muhimu yatahudhuriwa na wageni mbalimbali toka nchi jirani pamoja na wegeni kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini.
 MWISHO

RC MWAMBUNGU AWACHARUKIA WALIMU WAKUU RUVUMA




 MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu

NA, STEPHANO MANGO, SONGEA

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu amewataka Walimu wakuu wa Sule za Sekondari na Msingi za Serikali Mkoani Ruvuma kutomrudisha Nyumbani Mwanafunzi Yeyote Kwa Kosa la Kutokuwa na ada, michango au Sare za Shule badala yake Washirikiane na Mzazi kuweza kutatua tatizo husika

Akizungumza na www.stephanomango.blogspot.com  Ofisini Kwake alisema ni Marufuku kumfukuza Mwanafunzi Shule kwa kosa ambalo sio lake kwani anayewajibika kulipa Ada au Michango  husika ya Shule ni Mzazi na Sio Mwanafunzi

Mwambungu Alisema kuwa Mwanafunzi anasomeshwa na Mzazi au Mlezi wake kitendo cha Kumfukuza Shule kwa Kosa ambalo sio Lake ni kumnyanyasa na  kumnyima haki yake ya msingi ya kupata Elimu Bora na Kwa Wakati Stahiki

Alisema kuwa Jukumu kubwa la Walimu ni Kutoa Elimu Bora na Malezi mazuri kwa Watoto kwani wao pia ni Sehemu ya Wazazi kitendo cha kuwafukuza kinaleta picha mbaya kwani mara nyingi wanafunzi hao wanapofukuzwa  wamekuwa wakiranda randa mitaani hali inayoweza kusababisha wakapatavishawishi vya kuingia kwenye makundi mabovu ya uvutaji bangi na ngono zembe kabla ya wakati

Alifafanua kuwa Walimu wanachotakiwa kufanya ni kuwasiliana na Wazazi wa Wanafunzi husika  Kupitia Maafisa Watendaji wa Vijiji au Mitaa ili kubaini ni tatizo gani ambalo linalomfanya Asilipe Ada na Michango kwa Wakati

"Maafisa Elimu na Wakaguzi hakikisheni agizo hili linatekelezwa kikamilifu ili kuongeza kiwango cha ufaulu katika Mkoa wa Ruvuma na kwamba yeyote Atakaye bainika kuzembea kutekeleza Wajibu wake basi Sheria zitafuata juu yake", Alisema Mwambungu

Alieleza kuwa Juhudi za Ujenzi wa Maabara ikiwa ni Utekelezaji wa Agizo la Rais Jakaya Kikwete zinaendelea kwa kasi Kubwa na Ifikapo mwezi Mei Mwaka huu Zitakuwa Zimekamilika na Kuanza kutumika kadri ilivyopangwa
MWISHO


Wednesday, July 16, 2014

TIDO ATIMKA MWANANCHI

 
 Mkurugenzi Mtendaji wa Mwananchi Communications Limited (MCL), Tido Mhando akizungumza na wafanyakazi wa MCL jijini Dar es Salaam jana. Picha na Venance Nestory
CHANZO: MWANANCHI
Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL), Tido Mhando amewaaga wafanyakazi wa kampuni hiyo baada ya kumaliza mkataba wake wa miaka miwili na nusu.
Mkataba wa Tido katika kampuni ya Mwananchi utafika kikomo mwishoni mwa mwezi huu.
Taarifa ya Ofisa Mtendaji Mkuu wa Nation Media Group (NMG), Linus Gitahi kwa wafanyakazi wote wa Afrika Mashariki ambako kampuni hiyo inamiliki vyombo vya habari, inasema Mhando anaondoka MCL huku akiacha mafanikio makubwa katika nyanja zote na kwamba atakumbukwa kwa mchango wake.
MCL ni kampuni tanzu ya NMG inayochapicha magazeti ya Mwananchi, Mwananchi Jumamosi, Mwananchi Jumapili, The Citizen, The Citizen on Saturday, Sunday Citizen na Mwanaspoti.
Kabla ya kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa MCL mwaka 2012, Mhando alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kati ya mwaka 2006 na 2010. Awali alikuwa Mkuu wa Idara ya Kiswahili ya Shirika la Utangazaji la BBC (1999-2006).
Mhando aliiwezesha MCL kukua kwa kasi kubwa katika mapato na katika mpango wa uchapishaji wa magazeti ya MCL Kanda ya Ziwa ambako wakazi wa mikoa hiyo sasa wamekuwa wakisoma magazeti asubuhi tofauti na zamani.
Wafanyakazi wa MCL walimpongeza kwa kuboresha masilahi yao kwa kipindi cha uongozi wake na kuandaa misingi bora ya uongozi, ikiwamo kumwandaa mrithi wake.
Akiwaaga wafanyakazi jana asubuhi, Mhando aliwashukuru kwa ushirikiano wao pia alisema amejifunza mambo mengi mapya, ikizingatiwa kuwa kwa miaka mingi alikuwa kwenye sekta ya habari ya utangazaji tofauti na uchapishaji. “Safari hii ilinipa uzoefu mpya na wenye changamoto nyingi lakini kupitia ushirikiano wenu wa dhati tulifanikiwa kuiweka kampuni katika hali nzuri,” alisema Mhando.
Gitahi alisema nafasi ya Mhando itachukuliwa na aliyekuwa Ofisa Mwendeshaji Mkuu wa MCL (COO), Francis Nanai.
Nanai alijiunga MCL , Agosti mwaka jana akitokea Kampuni ya Saruji ya Mbeya Cement (Lafarge Tanzania) ya mkoani Mbeya akiwa Mkurugenzi wa Biashara.

Thursday, June 5, 2014

MATUKIO MUHIMU YA KUMBUKUMBU YA KUZALIWA SANGA ONE

Mwenyekiti wa Chama Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Ruvuma Golden Sanga  akipokea maelezo kutoka kwa Viongozi wa Ligi ya SANGA ONE CUP kabla hajakagua timu ya TMK na Timu ya Manispaa katika mchezo wao muhimu ikiwa ni sehemu ya kumbukumbu yake ya kuzaliwa, ingawa pia ni kawaida yake kila mwaka kuanzisha Ligi katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea
SANGA ONE akipokea salamu za kuzaliwa kwake kupitia simu kutoka kwa ndugu, jamaa na marafiki kabla hajala nao chakula cha jioni katika ukumbi wa Hotel ya Top one inn

SANGA ONE ATIMIZA MIAKA 50 YA KUZALIWA KWAKE

Mwenyekiti wa Chama Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Ruvuma Golden Sanga (Sanga One) leo Juni 5, 2014 anatimiza miaka 50 ya kuzaliwa kwake 
HONGERA KWA KUTIIMIZA MIAKA HIYO SANGA NA MUNGU AKUJALIE AFYA TELE

Monday, March 3, 2014

MWANJA ; MAFANIKIO YA MBIO ZA BENDERA YAMELETA HAMASA MPYA CCM



Ni miaka minne sasa toka nilipoandika makala haya, leo kutokana na umuhimu wake naomba ndugu wasomaji wa Blog hii muweze kujikumbusha nilichokiandika na kama itawapendeza niko tayari kufanya uchambuzi mpya na wa kina kuhusu makala haya, endelea kutafakari kupitia maandisha haya 

picha nitaziweka hivi punde

MWANJA ; MAFANIKIO YA MBIO ZA BENDERA YAMELETA HAMASA MPYA CCM

Na: Stephano Mango, Songea
MIONGONI mwa kazi za chama cha siasa kilichopo Madarakani ni kuwa daraja la kuwaunganisha watu na serikali waliyoichagua katika kufanikisha ahadi zilizo ahidiwa wakati wa kampeni.

Mbali na jukumu  hilo, wajibu wa chama ni kusaidia watu kuielewa serikali yao inafanya nini kwa wakati gani na kwa lengo lipi.

Ni wajibu wa chama kutumia mbinu mbalimbali za kidemokrasia kuwahamasisha watu ili washirikiane na serikali yao ili kuwaondolea matatizo sugu ya umaskini, maradhi na ujinga ambao umewaelemea.

Chama pia kina wajibu wa kuhakikisha kuwa serikali inaendelea kuyajua maoni, shida na matakwa ya watu katika kufanikisha vita dhidi ya maadui ujinga, umaskini na maradhi.
Hata hivyo, chama kinawajibu wa kuwakemea wanachama wanaokwenda kinyume na matakwa ya kanuni na taratibu za chama.

Ingawa pia kina wajibu wa kuwaelimisha watu na wanachama wote kwa ujumla ili waweze kuona shughuli zinazofanywa na serikali yao katika kuwaletea maendeleo kusudiwa.

Hivyo basi, chama cha mapinduzi (CCM) kuelekea uchaguzi wa Serikali za mitaa mwaka huu, na mwaka 2010 katika uchaguzi wa Madiwani, Wabunge na Rais

Kimejiandaa kushinda kwa kishindo katika chaguzi hizo kwa sababu katika uwanja mpana wa siasa mwisho wa uchaguzi mmoja ni mwanzo wa uchaguzi mwingine

Na lengo kubwa la Chama chochote cha siasa katika Nchi yoyote duniani ni kushinda katika uchaguzi Mkuu na kuunda Serikali yaani kukamata dola

Kwa mantiki hiyo, Uongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Ruvuma kwa kushirikiana na kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Ruvuma iliamua kupeleka ujumbe kwa Wanachama na Wananchi kwa kutumia mbio za Bendera ya Chama Cha Mapinduzi

Mbio hizo za Bendera zilizinduwa rasmi Mei 28 mwaka huu wa 2009 Wilayani Tunduru katika Kijiji cha Matemanga Mkoani Ruvuma na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa  Ruvuma  Coleneus Msuha.

Akizungumzia malengo ya mbio hizo za Bendera Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Ruvuma Bw. Emmanuel Mteming’ombe anasema kuwa mbio za Bendera ni ngeni na kwa mara ya kwanza zimekimbizwa Mkoa wa Ruvuma na kuleta mafanikio.

Anasema malengo ya mbio hizo za Bendera ni kukifanya Chama kionekane kwa watu na kwa Wanachama, kisha kisikike na watu waonyeshe dalili ya kusikia uwepo wa Chama hicho.

Ni lazima Chama kitumie mbinu mpya katika kujipenyeza kwa Wananchi katika Siasa za ushindani ili kuweza kuwahamasisha waingie Chamani anasema Kiongozi wa Mbio za Bendera Nestory Mwanja

Mwanja anaendelea kufafanua kuwa tumeamua kukimbiza Bendera ili kuwahamasisha Wanachama wawe hai kwa kulipia ada zao za Uanachama na kuhudhuria vikao vya Chama kuanzia ngazi ya mashina, matawi, Wilaya na Mkoa. 

Mbio hizo za Bendera zimefanya kazi kubwa ya kuwaeleza Wanachama wote ujumbe kutoka Halmashauri Kuu ya CCM Taifa NEC kuhusu mabadiliko ya upigaji kura za maoni kuhusu kumpigia kura Diwani, Mbunge na Rais anasema Kiongozi huyo.

Anasema pia mbio hizo zimetumika kupeleka ujumbe kwa Wananchi kuhusu umuhimu wa kujiandikisha katika daftari la wapiga kura katika 

Misingi ya Demokrasia.Kueleza Sera imara za CCM kwa Wananchi ili waweza kuzitafakari na kushawishika kuingia Chamani
Kwani kila Chama kinapaswa kujipambanua kwa Wananchi ili waweze kuchukua maamuzi sahihi ya Chama gani Wajiunge nacho anasema Kiongozi huyo wa CCM  Mwanja

Kinachoonekana sasa, baadhi ya Watu wanakimbilia kujiunga katika Chama chochote cha Siasa, wanakimbilia katika hivyo sio kwa sababu ya kuvutiwa na itikadi zake zinazo ambatana na imani, bali wanakwenda kwa sababu wamevutiwa na sera papo kwa papo ambazo huwa zinamwagwa jukwaani bila kuwepo kwa mikakati stahiki ya kuzitekeleza sera hizo anasema Mwanja

Mbio za Bendera zimetumika pia kuwahamasisha Wanachama kuanzisha miradi mipya na kuiendeleza miradi ya zamani ya Chama ili kijikwamue Kiuchumi. Kwa sababu Siasa ni Uchumi bila Uchumi imara hatuwezi kufanya Siasa katika Chama hivyo Chama imara ni chenye Uchumi imara anasema Mwanja

Anaendelea kufafanua kuwa, mbio hizo za Bendera zimetumika kuelezea bayana mafanikio ambayo Serikali ya CCM imeyapata kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita. 

Kwani kuyaanika hadharani mafanikio hayo kutawafanya Wananchi waelewe jinsi ilani ya Chama Cha Mapinduzi ilivyotekelezwa chini ya Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa ambaye ndiye Rais wa Jamhuri ya Muungano, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete.

Kwani tunatambua kufanya hivyo kutaziba mianya kwa Viongozi wa vyama vya upinzani ambao kila kukicha wanajifanya vipofu na viziwi kwa kudai eti hakuna jambo lolote la maendeleo ya Watanzania linalofanywa na Serikali ya CCM huku wakijua wanayoyasema sio ya kweli anasema Mwanja

 Anaendlea kufafanua kuwa, CCM bado ni Chama makini kilicho na malengo makubwa ya kuwainua Wananchi wake hivyo wanapaswa kuwa na subira na kuridhika kwa yale mazuri yanayofanywa na Serikali pamoja na Chama tawala.

Kwani mambo mengi tumetekeleza kama ilani inavyoelekeza na katika maeneo mengine hasa katika Nyanja za miundo mbinu ya barabara, maji, afya na elimu, kuna mipango mbalimbali ya utekelezaji inaendelea  anasema kiongozi huyo.

Mwanja anasema kuwa mbio hizo zimetumika pia kumpongeza Rais Kikwete kwa kazi nzuri alayoifanya ya kutekeleza vyema ilani ya Chama Cha Mapinduzi. Kwani ni dhahiri juhudi zake za kuanzisha saccos na kutoa mitaji kwa wajasiriamali, kukuza Demokrasia katika misingi ya amani.utulivu na mshikamano.

Hata kuendeleza miradi ya Afya, barabara, maji, elimu na maboresho mbalimbali ya mishahara katika Sekta za Umma na mengineyo ni miongoni mwa utekelezaji mzuri wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi anasema Mwanja

Anaendelea kufafanua  Mwanja , mbio hizo za Bendera zimepita kwenye mashina na Matawi yote ya Chama Cha Mapinduzi Mkoani Ruvuma na kufanikiwa kuingiza jumla ya wanachama wapya 3951.

Na imezindua jumla ya miradi 35 ya Chama kwa Mkoa mzima, yaani imeweka mawe ya Msingi katika Ofisi za Matawi na pia zimefanikiwa kufungua Ofisi tano za Matawi.

Miradi hiyo imeghalimu jumla ya shilingi Milioni 380 ikiwa ni jitihada za Wanachama kutoka kwenye mashina na Matawi kwa ushirikiano Mkubwa na Uongozi wa CCM Mkoa.

Hata hivyo anasema mbio hizo zimepita kuangalia pia miradi ya Maendeleo inayotekelezwa na Serikali ya awamu ya nne.
Pia zimepita kuangalia miradi ya Wananchi na Wanachama wa CCM ya ufugaji wa Kuku, mbuzi,ng’ombe pamoja na ujenzi wa nyumba bora za watu binafsi ambapo miradi hiyo yote inagharimu Milioni  750.

 Katibu wa CCM Mkoa Ruvuma Emmanuel Mteming’ombe, amewashukuru wakimbiza Bendera kutoka katika Jumuiya ya umoja wa Vijana wa CCM Mkoa UVCCM.   

Ambao amewataja majina ya Mwanahamisi Ngaje kutoka Wilaya ya Namtumbo, Doris Ngareka kutoka Mbinga, Hamis Nkali kutoka Tunduru, Mkandu Ngonji kutoka Songea Vijijni, Nestory Mwanja ambaye ndio Kiongozi Mkuu, Hilda Mgao na Mwajuma Rashid kutoka Songea Mjini,   

Mteming’ombe anamalizia kwa kusema mbio hizo zenye mafanikio makubwa zilifikia kilele chake Juni  19 katika Kata ya Mletele iliyopo Manispaa ya Songea ambapo mgeni Rasmi alikuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa Coleneus Msuha.

Hata hivyo, Nestory Mwanja ambaye ndiye kiongozi wa mbio hizo za bendera amewataka Vijana wajiunge katika Chama kwani mhimili wa Taifa lolote ni Vijana.

Mwandishi wa Makala hii
Anaptikana kwa simu no.   0755 335051
Barua pepe:  Stephano12mango@yahoo.com



Sunday, March 2, 2014

FUIME ATANGAZA NIA YA UBUNGE 2015 JIMBO LA SONGEA MJINI KUPITIA CHADEMA


MWENYEKITI WA CHADEMA RUVUMA AMTIMULIA VUMBI DKT NCHIMBI



 MTANGAZA NIA YA UBUNGE JIMBO LA SONGEA MJINI JOSEPH FUIME AKIHUTUBIA MOJA YA MIKUTANO YAKE
MAMIA YA WAKAZI WAKIMSIKILIZA MTANGA NIA YA KUGOMBEA UBUNGE KATIKA KATA YA LIZABONI

Na Stephano Mango, Songea


MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoa wa Ruvuma Joseph  Lusius Fuime ametangaza nia ya  kugombea Ubunge kwa tiketi ya Chama hicho katika Jimbo la uchaguzi la Songea mjini ifikapo mwaka 2015 katika kinyang’anyiro cha uchaguzi mkuu

Fuime  ambaye Diwani wa Kata ya Mjini katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea akitangaza nia hiyo  jana ya kutaka kugombea jimbo ambalo kwa sasalinaongozwa na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt Emmanuel Nchimbi  kwenye mkutano wa hazara uliofanyika kwenye viwanja vya Soko kuu la Songea Mjini alisema kuwa ametafakari kwa muda mrefu pia ameombwa na makundi mbalimbali ya jamii ya Songea kuchukua fomu ya kugombea kiti hicho


Alisema kuwa baada ya kutafakari ameamua kwa dhati kusikiliza kilio cha makundi hayo na kugombea ubunge kwa tiketi ya CHADEMA  ili kwa pamoja kuweza kuondoa kero mbalimbali ambazo zinawasumbua wakazi hao


“Naomba niwaondoe hofu wanachama wenzangu ndani ya Chadema kuwa kutangaza kwangu nia  ya kutaka kugombea Ubunge hakuna maana kuwa wanachama wengine wanaotaka kugombea washindwe kutangaza nia ya kuwania nafasi hiyo”


Alisema kuwa wanachama ndio wenyewe  mamlaka ya kumchagua mgombea mwenye kujua matatizo ya wakazi wa Manispaa ya Songea na mbinu ya kushirikiana na wananchi hao kuweza kuyatatua kwa maslahi mapana ya ustawi wa jamii hiyo, pia atakayeweza kupambana na mgombea wa Ubunge kwa tiketi ya ccm.


Alieleza zaidi kuwa baada ya kufikia uamuzi huo kabla ya kutangaza nia aliamua kukaa na wazee wote wa Songea Mjini ambao wote kwa pamoja wameonyesha ushirikiano mkubwa na wamemwakikishia kuwa mwaka 2015 wakati wa uchaguzi watamuunga mkono kama walivyomuomba


Fuime ambaye pia ni Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Ccm katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea alijigamba na kuwaeleza wakazi wa Songea kuwa yeye ndiye anayefaa kupambana na Mbunge wa Songea Mjini kwa tiketi ya Ccm  Dkt Emmanuel Nchimbi.


Alifafanua zaidi kuwa Chadema imejipanga kwa dhati kutotoa nafasi tena ya uongozi kwenye Jimbo la uchaguzi la Songea Mjini kuchukuliwa na Ccm ambalo lina kata 21 na kati ya hizo 8 zinaongozwa na Madiwani wa Chama cha Chadema na kwamba mwaka 2015 kata zilizobaki zitanyang’anywa na Chadema.


Aliongeza kusema kuwa dawa ya kupambana na manyang’au waliomo ndani ya Ccm ni kujipanga na kuwabana kwa kutowapa nafasi ya aina yeyote kuanzia sasa na mpaka ifikapo 2015 kwani hivi sasa miradi mbalimbali katika Halmashauri ya Manispa ya Songea imekuwa ikijengwa chini ya viwango ambapo alitoa mfano kuwa miundombinu ya barabara, ujenzi wa vyumba vya madarasa na ofisi zimekuwa zikijengwa chini ya viwango huku manyang’au wa Ccm wakineemeka.


Alisema kuwa Wananchi wa Songea ambao wamekuwa wakikabiliwa na shida mbalimbali kutokana na ombwe la uongozi unaotokana na mfumo mbovu wa Ccm wana kila sababu ya kuunga mkono wazo lake la kuwania kiti cha Ubunge ili kuweza kufanikisha ustawi bora wa maisha ya wakazi wote kwa ushirikiano


Awali katika vipindi viwili vya uchaguzi mkuu vilivyopita Chama cha Demokrasia na Maendeleo kilikuwa kinamnadi Wakiri wa kujitegemea Edson Osward Mbogoro kugombea nafasi hiyo ambapo alikuwa akibwagwa na Mgombea wa Ccm  Dkt Emmanuel Nchimbi  ambaye ndiye Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini hadi sasa.


MWISHO