About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Sunday, February 26, 2012

CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA WA WAKULIMA WILAYA YA TUNDURU KIMEELEMEWA NA MZIGO WA MADENI

Na,Steven Augustino Tunduru

WAKATI Makampuni ya Wanunuzi wa Korosho Nchini wakiendele kutunishiana misuli na Serikali Chama Kikuu cha Ushirika wa Wakulima wa Wilaya ya Tunduru (TAMCU) kimekiri kuelemewa na mzigo wa Madeni ya Wakulima yaliyotokana na Chama hicho kununua Korosho za Wakulima wa
zao hilo.

Hayo yameeelezwa na Meneja wa Chama hicho Imani Kalembo wakati akitoa taarifa kwa Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Juma Madaha wakati wa kikao cha pamoja na Wadau wa Kilimo na viongozi wa Vyama vya Siasa .

Katika taarifa yake, Meneja huyo alifafanua kuwa hadi sasa chama hicho kupitia vyama vikuu vya Ushirika vya wakulima wa zao hilo kinadaiwa Jumla ya Shilingi Bilioni 2,441,870,350 .

Taarifa hiyo iliendelea kueleza kuwa fedha hizo zimetokana na chama hicho kununua jumla ya Kilo 6,976,821 ambazo Chama hicho kupitia vyama vya msingi vimeweza kuzilipia kwa asilimia 70% pekee .

Alisema sambamba na Deni hilo pia Tamcu bado inakabiriwa na deni la Shilingi Milioni.608,260,000 zilizo tokana na Mkopo wa  kilo 506,855 za Korosho za zilizo kopeshwa na wakulima kwa vyama vya Msingi .

Kalembo aliendelea kueleza kuwa wakati hayo yakiendelea Chama hicho pia  kinakabiliwa na changamoto ya Chama kushindwa kununua jumla
ya kilo 86,324 zenye thamani ya Shilingi Milioni 17,264,800 ambazo bado zipo mikononi mwa wakulima wa zao hilo hali inayo endelea
kuwakatisha tamaa ya kuendelea na kilimo hicho.

Akizungumzia hali uzalishaji wa zao hilo katika Msinu wa mavuno wa
mwaka 2011/2012,Kalembo alisema kuwa Takwimu za manunuzi na Korosho
zilizopo mikononi mwa wakulima zinazonesha kuwa Jumla ya Kilo 7,570,000
zilizalimwa katika kipindi hicho.

Akizungumzia madhara yaliyo sababishwa na mgomo wa  Makampuni ya Wanunuzi zao hili Mkuu wa Wilaya hiyo Juma Madaha aliwataka wakulima kupitia wadau hao kuwa na uvumilivu wakati Serikali ikitafuta
suluhisho la kudumu la soko la mazao hayo.

Mwisho

No comments:

Post a Comment