About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, February 23, 2012

MTOTO MCHANGA AOKOTWA NA MSAMALIA MWEMA AKILIA MSITUNI

Na,Steven Augustino,Tunduru

MTOTO mchanga anayekadiliwa kuwa na umri wa wiki moja au mbili kameokotwa baada ya kutelekezwa na mama yake mzazi na kukomea kusiko julikana

Taarifa kutoka kwa msamalia mwema aliyemuokota kichanga hicho Halima
Chalamanda alisema kuwa kabla ya tukio hilo alisikia Sauti ikitokea
katika vichaka vya Msitu uliokuwa kambi iliyofungwa ya Jeshi la Wananchi wa JWTZ wakati akielekea Shambani katika kijiji cha Namsalau.

Alisema kuwa baada ya kusikiliza kwa makini aligundua kuwa sauti ya kitoto
hicho ikitokea vichakani  hali iliyo msukuma kuingia katika msitu huo na kumkuta akiwa peke yake na kuamua kumchukua.

Chalamanda aliendelea kufafanua kuwa baada ya kumuokota mtoto huyo alichukua uamuzi wa kumpeleka katika Kituo kikuu cha Polisi kilichopo Mjini hapa na baadae akaelekezwa kumpeleka katika Hospitali ya Serikali ya Wilaya hiyo kwa ajili ya uchunguzi.

Akizungumzia hali ya  Mtoto huyo, Mganga wa Hospitali ya Serikali ya Wilaya hiyo Dkt. Goerge Chiwangu alisema kuwa hali ya mtoto huyo ilikuwa ni dhaifu sana lakini baada ya Msamalia huyo ambaye pia
analea Mtoto mchanga kumsaidia kwa kumnyonyesha Maziwa na kupatiwa hudumu za matibabu hali yake imeendelea kuimarika.

Alisema baada ya uchunguzi pia maafisa tabibu waligundua kuwepo kwa vidonda sehemu mbalimbali za mwili wake vilivyo sababishwa na  kukaa polini kwa muda mrefu hali iliyo wafanya wadudu kuanza kumshambulia sehemu mbalimbali za mwili wake.

Dkt. Chiwangu alieendelea kueleza kuwa kutokana na mtoto huyo kukosa mtu ayemtambua ofisi yake kwa kusaidiana na idara ya Ustawi wa Jamii
Wilayani humo wanampango wa kumpeleka katika Kituo cha Kulelea Watoto
Yatima kilichopo katika Hospitali ya Missioni ya Mbesa ili alelewe
huko na Watoto wengine.

Wakiongea kwa nyakati tofauti Afisa ustawi wa jamii wa Wilaya hiyo
Alto Philipo na Mlezi wa Watoto yatima Katika Kituo cha Mbesa Mchungaji Ignas Nchimbi walisema kuwa hilo ni tukio la kwanza la mama kutupa mtoto mchanga Wilayani humo toka Kituo cha kulelea Watoto yatima kifunguliwe mwaka 1960.

Akizungumzia hali ya Watoto wanao lelewa katika kitu hicho Mchungaji Nchimbi alisema kuwa kituo hicho chenye Watoto 27, kichanga hicho kitakuwa cha 28 na kwamba hali ya kituo ni nzuri.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda mbali na kuthibitisha kuwepo kwa tukio hilo amesema kuwa jeshi hilo linaendelea na uchunguzi na kwamba sheria itafuta mkondo wake endapo mtuhumiwa atabainika.

Mwisho

No comments:

Post a Comment