About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Friday, March 9, 2012

WANANCHI WAUA SIMBA NA KUTAFUNA NYAMA YAKE

Na Steven Augustino Tunduru

WAKAZI wa Kijiji cha Mkowela Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma wamefanikiwa kumuua Simba na kula nyama yake ikiwa ni ishara ya kuonesha machungu waliyo kuwa nayo dhidi yake.

Wakiongea kwa nyakati tofauti baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa Simba huyo ali uawa kufuatia msako mkali ulio washirikisha wananchi na mhifadhi wa wanyama Pori Ahmadi Ally aliye tumwa na Idara yake kuhakikisha kuwa Simba huyo anauawa.

Walisema msako wa Simba huyo ulianza Feb 23 mwaka huu baada ya Simba huyo kuonekana akizunguka katika mitaa ya Kijiji hicho na vijiji jirani na kusababisha hofu kwa wananchi.

Akizungumzia tukio hilo Kaimu Afisa Wanyama pori wa Wilaya hiyo Peter Mtani mbali na kuthibitisha kuwepo kwa tukio hilo alisema kuwa katika kipindi hicho Simba huyo alifanikiwa kuua Ng`ombe 2 Mbuzi 4 na Mbwa 2.

Mtani aliendelea kufafanua kwa kuwataja wamiliki wa Mifugo hiyo kuwa Ng`ombe walikuwa ni mali ya Hasan Mbwana na Mfugaji wa Jamii ya Kisukuma aliyetambulika kwa jina moja la Relesh.

Kuhusu Mbuzi na Mbwa Mtani alisema kuwa walikuwa mali ya  Alli Ngalaisho, Edward Immeni, Peter Hasani,James Ado na Lilasi Said  wote wakiwa niu wakazi wa Kijiji hicho.

Kufuatia tukio hilo Mtani alitumia nafasi hiyo kuwaomba wananchi wanapo waona wanyama wakali kama huyo wawahi kutoa taarifa katika idara yake ili waweze kuchukua hatua kabla hawajasababisha madhara kwao

Mwisho

No comments:

Post a Comment