About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, July 23, 2012

AUAWA KWA TUHUMA ZA KUIBA KANISANI


Na Augustino Chindiye, Tunduru

WANANCHI wenye hasira wamempiga na kumuua kazi wa mtaa wa Kadewele mjini Tunduru mkoani Ruvuma aliyefahamika kwa jina la Nasoro Hashim (18) baada ya kutuhumiwa kuingia na kuiba katika nyumba ya Paroko wa Kanisa kuu lililopo katika Jimbo la Tunduru/ Masasi.

Mashuhuda wa tukio hilo walidai kuwa katika mkasa huo marehemu Hashim alikutwa na kidhibiti cha simu tatu za mkononi mali za viongozi wa Kanisa hilo.

Walisema katika tukio hilo marehemu alishtukiwa baada ya kuonekana wakati akitoka katika nyumba hiyo na Sista mmoja ambaye hawakutaja jina lake ambapo baada ya kugundua hali hiyo alipiga kelele za kuomba msaada na kulifanya kundi hilo kujitokeza.

Walisema baada ya kipigo hicho marehemu alikimbizwa katika hospitali ya serikali ya Wilaya kwa matibabu ambapo alifariki baada ya muda mfupi.

Mganga aliye ufanyia uchunguzi mwili wa marehemu Hashim Dkt. Jeshi Daraja alisema kuwa chanzo cha kifo hicho ni kutokwa na damu nyingi kuliko sababishwa na kupasuka kwa fuvu la kichwa kulikotokana na kupigwa na kitu kizito.

Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Deusdedit Nsimeki, mbali na kukiri kuwepo kwa tukio hilo alisema kuwa Polisi wanaendelea na uchunguzi ili sheria iweze kufuata mkondo wake kwa waliohusika na tukio hilko.

Aidha kamanda Nsimeki alitumia nafasi hiyo kuwataka wananchi wa Mkoa huo kuachana na tabia za kuchukua sheria mikononi.
Mwisho

No comments:

Post a Comment