About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Wednesday, June 29, 2011

WATENDAJI WAZAWADIWA KWA UTUMISHI ULIOTUKUKA Na Stephano Mango,Songea HALMASHAURI ya Wilaya ya Songea imewatunuku zawadi ya Pikipiki mbili ya utumishi uliotukuka Watendaji wawili wa Kata ya Kilagano na Kata ya Litisha kwa kusimamia vizuri shughuli za maendeleo katika msimu wa bajeti ya mwaka wa 2010/2011 Akizungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo mara baada ya kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa Maendeleo jana Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Rajabu Mtiula alisema kuwa watendaji hao wamejitahidi kufanya kazi zao kwa kujituma na kwa uaminifu mkubwa Mtiula aliwataja Watendaji hao kuwa ni Notka Tewele wa kata ya Litisha na Skolastika Mkanula wa kata ya Kilagano ambao wameisaidia Halmashauri hiyo katika ukusanyaji wa mapato na usimamizi mzuri wa ujenzi wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao Alisema kuwa pikipiki hizo mbili aina ya Sunlg zimegharimu jumla ya milioni 4.6 na kwamba wazitunza na kuboresha utendaji wao wa kazi ili waendelee kuwa na rekodi ya utendaji unaostahili kwa mtumishi wa umma Alisema kuwa Halmashauri inaendelea kuwapa motisha watumishi wake wanaofanya vizuri katika kusukuma guruduma la maendeleo la Wilaya ya Songea na Taifa kiujumla ambapo watumishi hao wamekuwa wakipata zawadi mbalimbali kulingana na eneo lake la kazi Awali Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Anna Mbogo alisema kuwa kwa mwaka wa fedha wa 2010/2011 Halimashauri ilikasimia kukusanya mapato ya jumla ya Shs 10,145,866,000 kutoka kwenye vyanzo vyake vya mapato Mbogo alisema kuwa hadi mei 31,2011 Halmashauri ilikuwa imefanikiwa kukusanya jumla ya Shs 7,776,727,211.84 sawa na asilimia 76.65% ya mapato yote na kwamba ili kuongeza mapato kwa mwaka ujao wa 2011/2012 Halmashauri imejipanga kutekeleza mikakati mbalimbali MWISHO