About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Saturday, August 25, 2012

WASHAURIWA KUTOHARIBU SENSA WILAYANI TUNDURU


Na Steven Augustino, Tunduru

HALMASHAURI ya Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma imewahimiza viongozi wote kushiriki na kuwajibika katika nafasi zao ili kufanikisha zoezi la kuhesabu watu kupitia zoezi la Sensa ya watu na makazi kwa matumaini kuwa takwimu hizo zitasaidia Wilaya hiyo kugawanywa na kuwa Wilaya mbili.

Sambamba na faida hizo pia Wilaya hiyo kongwe iliyoundwa na wakoloni mwaka 1941 imetangaza kujivunia matokeo hayo kwa kuzitumia takwimu hizo katika mazoezi ya ugawaji wa Vitongoji, Vijiji,Kata Tarafa,Wilaya penngine na kilio chao cha kuomba kupatiwa mkoa wa Kusini kati (Selous) kikafanikiwa ili kuwawezesha wananchi wake kujikwamua kutoka katika lindi la umaskini uliopindukia.

Kufuatia hali hiyo kamati za Ulinzi na Usalama za Kata Wilayani humo zikaongezewa meno kwa kuzitaka kuwachukulia hatua watu wote waanao wapotosha kwa kuwajataza wananchi wasikubali kuhesabiwa katika zoezi la Sensa ya watu na makazi ainayotarajiwa kufanyika Agositi 26 mwaka huu huku wakihamasishwa kuijulisha jamii kuwa watakaogoma kuhesabiwa pia hawatapatiwa vitambulisho vya Taifa.

Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Faridu Khamis wakati akiongea na madiwani wa halmashauri hiyo katika kikao cha madiwani hao kilichofanyika katika ukumbi wa Boma mjini hapa na kuongeza kuwa watu hao wanaotumia kivuli cha uislam hawana nia nzuli nanchi yetu.

Khamisi pia aliwataka madiwani wa halmashauri hiyo kutumia nafasi zao kwa kuendelea kutoa elimu kwa wananchi wao juu ya faida za kuhesabiwa kuwa ni pamoja na kuwrzesha Serikali kupanga mipango yake kulingana na idadi yao kauanzia ngazi za vitongoji, vijiji, Kata.Tarafa, Wiaya , Mkoa na Taifa alisema endapo zoezi hilo litafanikiwa
Wilaya ya Tunduru itanufaika zaidi ya faida hizo.

Alisema pamoja na ukongwe huo Wilaya hiyo ambayo ukubwa wake ni sawa na mkoa wa Mtwara ambao kwa sasa umegawanywa na Wilaya 6 eneo lake lina kilometa za mraba zinazofanana na ukubwa hivyo anaamini kuwa endapo wananchi wote watatoa ushirikiano katika zoezi hilo sifa sitahili zitapatikana na kuifanya igawike katika maeneo madogo ya utawala na kuharakisha maendeleo yao.

Wakiongea kwa nyakati tofauti Mwenyekiti wa kamati ya sensa, Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Chande Nalicho na Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo Ephraem Ole nguyaine mbali na kubaliki kwa kampeni ya orodha ya watakao hesabiwa kutumika wakati wa kugawa vitambulisho vya taifa waliwahimiza waandikishaji wa sense kujaza kwa makini nyalaka husika pamoja na fomu zitakazo takiwa kujaza majina ya watu watakaogomea zoezi hilo.
Mwisho