About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, May 24, 2012

WAGONJWA WAISHUKIA WIZARA YA AFYA UKOSEFU WA EX-RAY RUVUMA

Na Gideon Mwakanosya
BAADHI ya wakazi wa halmashauri ya manispaa ya Songea wameimba serikali kupitia wizara ya Afya na ustawi wa jamii kuona umuhimu wa kuifanyia matengenezo X-ray ya hospitali ya serikali ya mkoa wa Ruvuma ambayo imeshindwa kutoa hiyo kwa wagonjwa kwa muda mrefu na kusababisha wagonjwa wanaotakiwa kupata huduma hiyo kwenda kwenye hospitali ya Peramiho ambako ni mbali na Songea mjini.

Wakizungumza na NIPASHE kwa nyakati tofauti baadhi ya wananchi wa maeneo ya Mfaranyaki, Mjimwema, Ruhuwiko na Mshangano ambao waliomba majina yao yahifadhiwe walieleza kuwa kwa muda mrefu sana huduma ya X ray katika hospitali ya mkoa haipatikani na wanapokwenda hospitalini hapo kupata huduma wamekuwa wakishauriwa kwenda Hospitali ya misheni ya Peramiho ambako ndiko huduma hiyo kwa sasa inatolewa.

Wananchi hao walisema kuwa ni vyema serikali ikaangalia uwezekano wa kuitengeneza mashine hiyo ambayo hapo awali ilikuwa msaada mkubwa kwa wakazi wa Songea na wagonjwa wanaotoka kwenye wilaya nyingine kama vile Mbinga, Natumbo, Tunduru na wilaya mpya ya Nyasa.

Walitoa mfano kuwa hivi karibuni katika eneo la Seedfarm kwenye barabara itokayo Songea kwenda Namtumbo gari la jeshi la wananchi liliwagonga watu wanne ambao walikuwa wakitembea kwa miguu na kusababisha watu wawili kufa papo hapo na wengine wawili walijeruhiwa vibaya na kukimbizwa katika hospitali ya serikali ya mkoa ambako mmojakati yao baadae ililazimika kumpeleka Peramiho baada ya hospitali hiyo kukosa huduma ya X ray jambo ambalo limeonekana kuwa ni kero kubwa kwa wananchi wa Songea na maeneo mengine.

Kwa upande wake kaimu mganga mkuu wa mkoa wa Ruvuma Dr Benedict Ngaiza alipohojiwa na NIPASHE kuhusiana na malalamiko hayo alikirikuwa mashine ya x ray ya hospitali ya serikali ya mkoa wa Ruvuma bado ni mbovu tangu mwezi mmoja uliopita.

Dr Ngaiza ambaye pia ni mganga mfawidhi wa hospitali ya serikali ya mkoa Songea alisema kuwa pamoja na kwamba katika hospitali yake haukuna huduma hiyo ya x ray lakini wagonjwa wanaohitajihuduma hiyo hushauriwa kwenda kupta huduma hiyo kwenye hospitali ya misheni ya Peramiho licha ya kuwa nayo maashine ya hospitali hiyo inaubovu haifanyi kazi kwa kiwango kinachotakiwa.

Alisema kuwa changamoto baadhi ya huduma zinazohusisha huduma ya x ray katika hospitali ya mkoa zimesimamishwa kwa sasa. Hadi hapo wataalamu toka wizara ya afya na ustawi wa jamii watakapofika na kuja kuifanyia matengenezo.

Alieleza zaidi kuwa kwa mujibu wa taarifa toka wizara ya afya na ustawi wa jamii mafundi wanatarajiwa kusambazwa katika hospitali zote za serikali zenye mashine za x ray kwa ajili ya kuzifanyia matengenezo x ray hizo ikiwemo na x ray ya hospitali ya serikali mkoa Songea.

Alifafanua zaidi kuwa pamoja na matengenezo yanayotarajiwa kufanyika bado hali si nzuri kwani chumba cha x ray kinatarajiwa kufanyiwa urakabati mkubwa ambao utafanywa kwa muda wa zaidi ya miezi mitatu. Hivyo hata kama mashine hiyo itakapo tengenezwa bado huduma ya x ray itasimama hadi ukarabati wa chumba hicho utakapo kamilika.

TANI 5480 ZA KOROSHO ZILIZOKWAMA TUNDURU ZAPATA MNUNUZI

Na AUGUSTINO CHINDIYE, Tunduru
JUMLA ya tani 5480 za korosho za Wakulima wa Tunduru Mkoani Ruvuma zilizo kuwa zimekwama katika Vyama vya Msingi vya Wakulima vya Wilaya hiyo baada ya Serikali kutoa dhamana ya fedha za Kugharamia malipo kwa Wakulima husika zimepata mnunuzi.

Taarifa ya kupatikana kwa mteja wa Korosho hizo imetolewa na Meneja wa
Chama kikuu cha Wakulima wa TAMCU  Imani kalembo jana wakati akiongea na wajumbe na wadau wa taasisi hiyo Wilayani humo katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi za Chama hicho mjini hapa.

Akitoa taarifa hiyo Kalembo alisema kuwa Korosho hizo zenye thamani ya Shilingi Bilioni 8 zimenunuliwa na kampuni ya Pan- African Consulting And Exportng (P.A.C.E) kutoka Carfonia
Martekan ambayo imekubali kununua korosho hizo kwa bei ya Shilingi 1491 kwa kila kilo moja.

Kalembo aliendelea kueleza kuwa tayari kampuni hiyo imekwisha tiliana saini mkataba wa kununua Korosho hizo na kuzifanyia uchunguzi wa kuzikagua kwa kuzikata ili kubaini ubora wake na kuahidi kuzilipia kwa kuingiza fedha Benki ya Nmb  muda wowote wiki hii.

Alisema kufuatia hali hiyo Chama hicho kinajipanga kuangalia uwezekano na taratibu za kulipa madeni yote ya wakulima ili kuondokana na kero hiyo iliyochukua muda mrefu.

Kwa mujibu wa takwimu za uzalishaji wa wa zao hilo kutoka katika Chama Kikuu cha Ushirika wa Wakulima wa Korosho Wilayani Tunduru (TAMCU) zinaonesha kuwa katika msimu wa Mwaka 2011/2012 chama hicho kupitia vyama vya msingi umeongezeka na kufikia kilo 7,570,000 kutoka kilo kilo 4,135,042 zilizo zalishwa  mwaka 2010/2011.
Mwisho