About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, August 14, 2012

WAANDISHI WAASWA KUIKUMBUSHA SERIKALI KUTIMIZA AHADI ZA WAZEE


Na Stephano Mango, Songea


WAANDISHI wa habari nchini wametakiwa kuona umuhimu wa kuisukuma Serikali ili iweze kutimiza ahadi yake ya kuwajali na kuwathamini wazee nchini ili waweze kukabiliana na changamoto zinazowakabili katika maisha yao kutokana na uzembe wa baadhi ya watumishi wa umma

Wito huo umetolewa jana na Katibu Mkuu Mtendaji wa Mtandao wa Kinga Jamii Tanzania Iskaka Msigwa wakati akizungumza na waandishi wa Habari ofisini kwake kuhusu kusuasua kwa ahadi mbalimbali ambazo serikali ili ahidi kuzitekeleza

Msigwa alisema kuwa waandishi wa habari wanawajibika kufuatilia na kuikumbusha Serikali juu ya matamko yake mbalimbali katika hotuba za viongozi wake, Sera ya Wazee ya mwaka 2003, Mkukuta na mengineyo kuhusu ustawi wa hali za wazee katika afya,kulipwa pensheni wazee wote, kusamehewa kulipa kodi za majengo, uwakilishi, kuzuia vitendo vya ukatili kwa wazee na uwepo wa mabaraza ya wazee

“Kwa sababu wazee kwa masikitiko makubwa tumeona kwamba nia njema ya serikali ya kuboreshwa maisha ya wazee inakwamishwa na utendaji usioridhisha wa baadhi ya watumishi wa umma katika sekta mbalimbali unaofanywa kwa makusudi” alisema Msigwa

Alifafanua kuwa ukosefu wa huduma ya uhakika ya afya ya wazee pamoja na kuwepo sera inayotoa haki ya wazee kupatiwa huduma hii bure bado haipatikani na hata pale inapotolewa bado madawa hayapatikani,pato duni miongoni mwa wazee na wategemezi wao, Ukandamizaji wa haki za wazee ikiwemo haki ya kuishi-(wazee kuuawa kwa hisia za uchawi) ukosekana kwa mfumo wa hifadhi ya jamii/Kinga ya kijamii ni miongoni mwa changamoto zinazowakabili wazee nchini

Alisema kuwa wazee wanapaswa kuthaminiwa utu wao kwani uzee sio ugonjwa bali ni hatua muhimu katika maisha ya mwanadamu ,kwani tunapaswa kuuona uzee ni ufahari si tu kwake yeye tu bali kwa jamii pana kwa sababu Taifa lisilo na wazee ni taifa lililokufa

Alieleza kuwa miongoni mwa wajibu wa waandishi wa habari ni kupaza sauti za wanyonge wakiwamo wazee ili zisikike kwenye majukwaa tofauti tofauti ya watoa maamuzi ili kuweza kuleta ustawi stahiki kwa wazee
MWISHO