About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, April 23, 2013

MKIA MIWILI YA TEMBO YAMSABABISHIA KUSHIKILIWA NA POLISI RUVUMA

Na Gideon Mwakanosya,Songea.


JESHI la Polisi mkoani Ruvuma linawashikilia watu wa tano kwa matukio tofauti likiwemo la watu wawili kukamatwa na mikia miwili ya Tembo ,Risasi tatu na kichwa kimoja cha bunduki aina ya Rifle huku tukio la pili ni mtu moja kukamatwa na bangi kilo 50 na miche ya bangi yenye uzito wa kilo 62 wakati tukio la tatu yote ya wizi wa pikipiki huku pikipiki mbili ziliibiwa jijini Dare-Esalaam na moja ya mjini Songea mkoani Ruvuma.

Watuhumiwa wanaoshikiliwa na polisi katika matukio matatu tofauti ni Rashidi Kapesa [29] Teofanesi Mapunda [29] Eleneus Mapunda [37] Bakari Milanzi [40] na Yahaya Rajabu umri wake haukutajwa

Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake kamanda wa polisi mkoani Ruvuma Deusdedit Nsimeki alisema kuwa tukio la kuwakamata watuhumiwa na mikia ya Tembo lilitokea Aprili 18mwaka huu majira ya 1.30 jioni baada ya askari wanyama pori Hassani Mihuka alipokuwa doria na wenzake waliwakamata Rashidi Kapesa [29]mkazi wa kijiji cha Mandepwende na Teofanesi Mapunda [29]mkazi wa kjiji cha Mtonya .

Kamanda wa polisi alisema kuwa watuhumiwa hao waliokamatwa eneo la kambi ya watu wakujenga barabara Progressive lililopo Mchomolo wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma ambao walikutwa na mikia 2 ya Tembo ,Risasi 3 kichwa kimoja cha bunduki aina ya Rifle kilichokuwa kimefichwa ndani ya begi.

Kamanda Nsimeki alisema kuwa mnamo Aprili 20 mwaka huu mjira ya saa kumi jioni huko katika kijiji cha Ngahokola mashambani wilayani Songea ambako askari polisi wakiwa kwenye doria yao ya kila siku walifanikiwa kumkamata Eleneusi Mapunda akiwa na bangi kiasi cha kilo 50 na miche ya bangi yenye uzito wa kilo 62.

Alifafanua zaidi kuwa katika tukio lingine inadaiwa kuwa mnamo Marchi 7 mwaka huu katika muda usiofahamika kwenye eneo la Lizaboni manispaa ya Songea polisi ilifanikiwa kumtia mbaloni Bakari Milanzi [40]aliwa na pikipiki yenye namba za usajili T354 BNZ SANLG na baada ya uchunguzi yakinifu ilibainika kuwa namba halisi za usajili wa pikipiki hiyo ni T 775 BWC mali ya Teodora Sephan Mtweve wa jijini Dare –Esalaam ambaye inadaiwa pikipiki yake iliibiwa tangu mwezi Julai 2012 katika eneo la Kimara baada ya mwendesha bodaboda huyo kuporwa na mtu asiye fahamika.

Kanda alilitaja tukio lingine kuwa inadaiwa mnamo Marchi 7 nwaka huu askari polisi walio kuwepo eneo la doria la Lizaboni manispaa ya Songea mtuhumiwa Yahaya Rajabu alikamatwa na pikipiki yenye namba za usajili T 557 BYR aina ya SANLG ambayo baada ya kufanya uchunguzi ilibainika kuwa namba zake halisi za usajili kuwa ni T 7551 BSY ambayo mmiriki wake halisi ni Rose Gerevas Makene mkazi wa jijini Dare –Esalaam ambaye pikipiki hiyo iliibiwa katika maeneo ya Kimara Julai 7 mwaka 2012 baada ya mwendesha bodaboda huyo kuporwa na watu wasiofahamika.

Aidha alilitaja tukio jingine kuwa mnamo Februari mwaka huu khuko katika wilaya ya Tunduru askari wakiwa kwenye doria walifanikiwa kukamata pikipiki yenye namba za usajiri T.736 aina ya SANLG ambayo baada ya polisi kufanya uchunguzi wa kina ilibainika kuwa namba hizo kuwa ni bandia hivyo namba halisi za usajili wa pikipiki hiyo kuwa ni T 787 CDL na kuwa ni mali ya Isdori Mdolino mkazi wa Songea mjini ambayo inadaiwa iliibiwa Januari 26 mwaka huu. na baada ya mwendasha bodaboda kuporwa na kuwa watuhumiwa watafikishwa mahakani mara baada ya upelelezi kukamilika.

MWISHO.

TAFAKARI MAANDIKO HAYA KWA AFYA YA AKILI YAKO

Umaarufu au Udhaifu Haulazimishwi, Bali Unajithibitisha Wenyewe!


Ukweli siku zote ni lazima ubakie ukweli, watu wengi mara kwa mara wamejitahidi kurudia uongo na hata wakati mwingine uongo huo ukiandamana na vitendo vya uhalifu wa kupangwa ili mradi tu kuuhalalisha uongo huo! Yote hii ni kujitahidi kuficha ukweli, lakini ukweli siku zote haupotei, unaweza kujificha kwa kipindi kifupi lakini mwishowe ni lazima ujitokeze.

Kuna wanasiasa mchwara ambao wanadhani kutumia magenge ya uhalifu wa kupangwa kwa kuwadhuru waandishi wa habari na wale wote wanaoonekana kuwa wawazi wa kujieleza na kutoa maoni yao juu hali halisi ya kisiasa na kiuchumi hapa nchini, ndiyo watakuwa wamefanikiwa kuuficha udhaifu wao usijulikane mbele ya jamii! Hizi ni fikra dhaifu zisizokuwa na maono ya mbali kwa vile udhaifu au umaarufu wa mtu hudhihirishwa na mtu mwenyewe, na wala haudhihirishwi na mwandishi wa habari, chombo cha habari wala mtu yeyote zaidi ya wewe mwenyewe! Hivyo kuwaandama waandishi au watu wanaoonekana kujua udhaifu wako haina maana kwamba ukimaliza kuwaangamiza ndiyo umeimarisha umaarufu wako, hapana, bali utakuwa umezidi kujidhoofisha!

Tukirudi nyuma kwenye uchaguzi wa mwaka 2005 lile genge la uhalifu wa kupangwa ambalo lina matawi hata huko kwenye nyombo vya habari; lilipomchafua Dr. Salim Ahmed Salim ili aonekane hafai mbele ya jamii kuwania kile kiti cha kula bila kuulizwa unakulaje? Genge hili lilidhani limemdhoofisha Dr. Salim moja kwa moja lakini kiukweli limemuimarisha, na limejikuta ule upande lililokuwa linaushabikia ndiyo umedhoofika tena upo taaban! Hii yote imetokea kwa vile Dr. Salim alijua kwamba umaarufu wa mtu unatengenezwa na mtu mwenyewe, na ndiyo maana hata alipochafuliwa hakutaka kulumbana, bali alikaa kimya akisubiri ukweli ujilete wenyewe ambao wote tunauona!

Watanzania inabidi tuwe makini wa kuweza kutambua wenyewe bila ushawishi watu wenye sifa za kuwa viongozi wa umma bila ya msukumo wowote toka kwenye lile genge ambalo siku zote lipo mustari wa mbele kabisa kutuchagulia viongozi kwa kuwajengea umaarufu wa uongo ili mradi mambo yao yaendelee kuwa mazuri na sisi tukiendelea kuwa masikini zaidi! Sasa hivi genge hili hili lipo katika kampeni chafu za kuwajengea baadhi ya wanasiasa umaarufu wa uongo na baadhi yao hata umri wao bado haujawaruhusu kujipenga makamasi peke yao, ni mpaka wapengwe makamasi na hata nguo bado wanavalishwa, lakini mikakati inafanywa ili hata katiba ibadilishwe watu wao waweze kugombea urais! Watoto wadogo wawe marais wa taifa lipi!? Hao watoto wamefanya miujiza gani mkapa hata tuone kwamba wana umuhimu wa kuliongoza taifa hili!? Au kupiga makelele bungeni ndiyo busara kwa uelewa wa Watanzania!? Au kutumiwa na mitandao kwa kupewa siri za serikali na kuzitoa bungeni ndiyo wameshakuwa mashujaa kiasi ambacho hatuwezi kuishi bila wao kutawala!? Kwani nani hawezi kusimama bungeni na kuzungumza kama ameshapewa kitu au hoja ya kuhoji!? Wabunge hawa wanaotumiwa na genge la kuandaa viongozi kiukweli ni wabunge dhaifu sana kuliko hata wale ambao wamekuwa wakitumia fikra zao binafsi bungeni; Marais watoto wakaongoze nchi zilizoendelea kama vile Amerika na UK ambako democrasia imekuwa na rais ni taasisi siyo mtu binafsi kama hapa kwetu Tanzania.

Watanzania tumeshindwa kuwatambua watu wenye busara kwa mtizamo wetu binafsi! Tunadhani kuandikwa sana kwenye kila gazeti ndiyo ubusara wa mtu, unaweza kuandikwa sana lakini ukawa huna lolote zaidi ya umaarufu wa uongo, na ukawa huandikwi sana lakini ukawa na busara zaidi kuliko wale wanaopamba kurasa za mbele za magazeti ya kila siku! Pia unaweza kutumiwa na genge la media si kwa sababu unaweza hapana, bali unatumiwa ili uwaharibie wale wanaofaa, ili wananchi wasiokuwa wadadisi wazuri wa mambo ya siasa washindwe kutofautisha ni yupi anapengwa makamasi au ni nani anajipenga mwenyewe! Siyo kila mtoto akililia gozi lazima umpe, watoto wengine ukiwapa gozi badala ya kulicheza wao hulilambalamba na kulitemea mate! Mtoto mdogo mpe pipi amumunye! Gozi licheze mwenyewe!

Kulingana na hali halisi ya nchi yetu kwa sasa nchi ambayo ina migogoro mingi ya kidini, ardhi, mauaji na vitendo vya uhalifu wa kupangwa (mafia), ufisadi uliokithiri, ubadirifu wa mali ya umma, kuzorota kwa uchumi na maendeleo ya jamii, kuzorota kwa mfumo wa elimu na afya bora nchini; tunahitaji rais mpevu mwenye busara ya hali ya juu asiyefungamana na upande wowote, mwadilifu, mbunifu na mwenye maono ya mbali ili aweze kuliokoa hili taifa ambalo tukilifanyia mizaha ya kushabikia watu wasiokuwa na sifa tutalielekeza gizani!

Ukitumia nguvu zinazoambatana na vitendo vya uhalifu wa kupangwa kwa madhumuni ya kujijengea au kuwajengea umaarufu wale wasiostahili, utakuwa hujijengi wala huwajengei bali unawabomoa! Kama hatuamini haya tusubirini ukweli wa uhalifu wote wa kupangwa utajitokeza mwishoni, na hapo ndipo tutakapoona kwamba je, wale wataalamu wa kupanga na kushabikia uhalifu huo watakuwa wamejijenga au wamejibomoa!?

Dr. Noordin Jella Email: norjella@yahoo.com Mobile: +255 782 000 131