About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Wednesday, January 25, 2012

WAZAZI WAKIWA KUFUATILIA MAENDELEO YA ELIMU YA MTOTO WA KIKE

                   Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Juma Madaha

Na Augustino Chindiye,Tunduru

SERIKALI imewataka Wazazi na Walezi kusimamia na kufuatilia kwa karibu maendeleo ya Watoto wao hasa wa kike zikiwa ni juhudi za kuhakikisha kuwa watoto hao wanafanya vizuri katika masomo yao na kujiletea maendeleo yao.

Wito huo umetolewa kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Juma
Madaha na kaimu Katibu Tawala wa Wilaya hiyo Manfred Hyera wakati akiongea na Wadau wa elimu waliohudhuria katika mafunzo
ya uzinduzi wa Mradi wa Usimamizi na Utetezi wa Haki ya Mtoto wa kike kupata elimu yaliyofanyika katika ukumbi wa Skyway mjini hapa.

Alisema ili kufanikisha hali hiyo serikali imejipanga kutoa elimu kwa kuwaomba wazazi na walezi kuchangia chakula ili kufanikisha watoto wao kuanza kupata chakula mashuleni kama kivutio kwa wanafunzi kupenda masomo.

Akizungumzia mila na destuli za makabila ya Wayao alisema kuwa tayari serikali imeunda kikosi kazi cha kuonana na viongozi wa mila, makungwi na manyakanga kuwaelimisha juu ya utoaji wa elimu kwa watoto wa kike kupenda masomo tofauti na sasa ambapo kundi hilo limekuwa likifundishwa kukabiliana na maisha ya ndoa hali iliyo sababisha kuwepo kwa matukio mengi ya ndoa za utotoni wakiwa shuleni.

Wakiongea kwa nyakaka tofauti baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo Hadija Hasan na Amina Mwajesa katika maoni yao juu ya kinachosababisha elimu kushuka Wilayani humo walidai kuwa Kipato duni cha akina mama ambao mara nyingi ndio wamekuwa wakiachiwa jukumu la kutunza Watoto wa kike .

Kuhusu mila na desturi za makabila hayo washiriki hao waliiomba
Serikali kuchukua hatua za makusudi kusimamia na kutokomeza  mila hizo hasa mafunzo mabaya ambayo hutolewa wakati wa jando na unyago pamoja na kuwataka akina mama kuacha tabia za kutunza siri za watoto wao wa kike.

Akisoma risala ya mafunzo hayo Mwakilishi kutoka shirika lisilokuwa la kiserikali la TUFAE Educcation Aids Trust linalo ratibu mafunzo hayo Hakimu Kilowa alisema kuwa mafunzo hayo yamefuatia majibu mabaya baada ya utafiti uliofanywa na shirika hilo mwaka 2007 hadi 2010 juu ya maendeleo ya elimu kwa mtoto wa kike wilayani humo.

Kilowa alisema katika utafiti huo uliofanyika katika Tarafa za
Muhuwesi,Namasakata,Ligoma,Nandembo,Mlingoti Mashariki na Mlingoti Magharibi zilibainisha kuwapo kwa kundi kubwa la watoto wa kike waliopata mimba pamoja na kikwazo cha uelewa mdogo wa jamii juu ya SERA ya Elimu,Haki ya mtoto wa kike kupata Elimu,Mila zilizopitwa na wakati.

Alisema Takwimu hizo zilifafanua kuwa katika kipindi cha Mwaka
2007-2010 jumla ya waliotarajiwa kuandikishwa shule ni watoto wa kike 17,386, walioandikishwa ni 14,692 ambao ni Sawa na asilimia 85.49%  na waliosajiliwa ni 13,411,waliofanya mitihani wa kumaliza darasa la saba walikuwa 13,097 ambao ni sawa na asilimia 97.65%, huku kukiwa na anguko la watoto 314 ambao waliacha shule kwa sababu mbalimbali ikiwemo kupata mimba wakiwa shuleni pamoja na utoro.

Awali akitoa ufafanuzi wa mafunzo hayo Meneje wa Mradi wa shirika hilo John Nginga katika maelezo yake alisema kuwa lengo la mradi huo ni kuhakikisha kuwa mtoto wa kike anapata elimu kuanzia darasa la awali, elimu ya msingi, sekondari hadi Chuo Kikuu.

Mafunzo hayo ya siku 15 yanayofadhiliwa na Shirika la The Foundation for Civi Society (FCS) la Jijini Dar Es Salaam  yatahusisha wadau 180 kutoka katika makundi ya Walemavu,walimu, wazee,Viongozi wa Vyama vya Siasa, Dini,Watendaji Kata na Vijiji kutoka katika Kata Sita hizo kwa ajili ya kupeana mbinu na kubainisha changamoto zinazotokana na vikwazo vya Mtoto wa kike kupata Elimu badala ya kuwa ozesha wakiwa
wadogo.

Mwisho.