About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Friday, June 1, 2012

WALIMU WAOMBA KUTENGEWA MAENEO YA KUJENGA MAKAZI YAO

Na, Steven Augustino,Tunduru

HALMASHAURI ya Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma imeombwa kuandaa utaratibu wa kutoa viwanja vya makazi kwa Watumishi wa Hamashauri hiyo kama kivutio na kuwafanya wasifikilie kuhama.

Ombi hilo lilitolewa na Walimu wa Shule ya Sekondari Tunduru Wilayani humo wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza wanafamilia hao kufuatia Shule yao kufanya vizuri katika matokeo ya mitihani ya  Kidato cha Sita mwaka 2012.

Akifafanua ombi hilo kwa niaba ya wanafamilia hao, Mkuu wa Shule hiyo Mwl. Ausi Limia alisema kuwa endapo kutakua na utaratibu huo kuna uwezekano mkubwa kwa watumishi wanaopangiwa kufanya kazi katika halmashauri hiyo kushawishika na kufanya kazi na kusaidia kukuza mji huo haraka baaa ya kujenga nyumba zao.

Pamoja na Ushauri huo pia wanafamilia hao wakaanika Changamoto mbalimbali zinazoikwamisha Shule yao kupa hatua za kimaendeleo kwa haraka yakiwemo ya ukosefu wa Walimu wa masomo ya Sayansi, Uchakavu wa Majengo na Shule kutokuwa na gari dogo kwa ajili ya kutoa huduma kwa
wanafunzi wake pamoja na kutokuwa na watumishi wasio walimu.

Awali akisoma risala katika hafla hiyo Mwl. Limia pia akabainisha kuwa katika matokeo hayo mwaka huu Shule hiyo iliweza kufaulisha wanafunzi wote 155 waliosajiriwa kujiunga na kidato cha tano mwaka jana,

Mwl. Limia aliendelea kueleza kuwa kufuatia matokeo hayo Shule yake ilishika nafasi ya pili kimkoa kati ya Shule 9 na kushika nafasi ya 21 kitaifa kati ya Shule 326 ikiwa ni tofauti na matokeo ya mwaka 2011
ambapo shule hiyo ilifaulisha wanafunzi 111 kti ya wanafunzi 133 waosajiriwa waka 2010

Ajikibu Risala hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya Chande Nalicho, Afisa Tarafa wa tarafa ya Milingoti Manfredi Hyera pamoja na mambo mengine aliahidi kuzifikisha kero hizo kwa wahusika kwa ajili ya
utatuzi.

Kuhusu ukosefu wa Watumishi wasio walimu Hyera aliwaasa wanafamilia hao kubuni miradi mbalimbali ikiwemo ya kilimo ili wawezesha kumudu kuwalipa watumishi hao.

Mwisho