About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, April 30, 2013

MANGULA AGONGANA NA CARTAPILLA LA CCM


NA PIUS NTIGA


MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi-CCM Tanzania Bara Mzee PHILP MANGULA, amekutana na kufanya mazungumzo na Makamu Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Bara Mzee JOHN MALECELA na kushauriana kuwa Chama kisiendelee kuwafumbia Macho wanachama wanaokiuka taratibu za Chama.

Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika Ofisi Ndogo Lumumba yamelenga kuzungumzia umuhimu wa Chama kuendelea kusimamia ipasavyo kanuni za Chama hasa katika kupata viongozi kupitia chaguzi mbalimbali za Chama.

Katika mazungumzo hayo Mzee MANGULA amesisitiza kuwa viongozi wote waliochaguliwa kwa kutoa rushwa siku zao zinahesabika ndani ya Chama kwani Kamati Ndogo iliyoundwa kufuatilia suala hilo itaanza kuwaita kwa ajili ya mahojiano kila mmoja kwa wakati wowote kuanzia sasa.

Mzee MANGULA amesema Kamati hiyo ambayo ipo chini yake tayari imepokea malalamiko mengi kutoka kwa wanachama wanaowashutumu wagombea kuchaguliwa kwa kutoa rushwa katika chaguzi mbalimbali za Chama zilizofanyika mwaka jana.

Kwa upande wake Mzee MALECELA amempongeza Mzee MANGULA kutokana na kuchaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara huku akimtaka kusimamia pasipo woga kurudisha nidhamu ya Chama kwa kuendelea kuwachukulia hatua kali viongozi waliochaguliwa kwa njia ya kutoa rushwa ndani ya Chama.

MSTAAFU AFARIKI KWA UNYWAJI WA GONGO BAADA YA KUPATA MAFAO



Na Steven Chindiye, Tunduru

MWALIMU mstaafu katika Kijiji cha Kidodoma Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma Rajab Mohamed Kalesi (65) amefariki dunia baada ya kunywa pombe haramu ya Moshi ambayo inafahamika kwa jina la Gongo.

Mashuhuda wa tukio hilo akiwemo mdogo wa marehemu Athuman Saidi walisema kuwa kabla ya mkasa huo marehemu alionekana akinywa Pombe hizo kwa siku mbili mfululizo akiwa amefungiwa katika nyumba ya muuzaji wa pombe hiyo Hamdi Swalehe huku akiwa anatamba kuwa ana fedha nyingi alizokuwa ametoka kulipwa kama mafao ya kustaafu kazi hiyo.

Walisema kufuatia taarifa hiyo ya kupokea fedha hizo zinazo daiwa kuwa zilikuwa ni zaidi ya Shilingi Milioni 48 mstaafu huyo alionekana kutembea na wapambe muda wote huku wakienda kujipatia kinywaji hicho kwa wingi na kumsababishia dhahama hiyo ya kupatwa na umaiti.

Wakiongea kwa nyakati tofauti Diwani wa viti maalumu wa Tarafa ya Nampungu Rehema Nyoni na Mtendaji wa Kijiji hicho Mbuyu Ally Mbuyu walisema kuwa baada ya wapambe hao kuona hali ya tajiri yao imebadilika walitimua mbio na kumtelekeza katika nyumba ya muuza pombe hiyo hadi umauti ukamkuta akiwa peke yake.

Walisema akiwa katika hali yha kutapatapa Mke wa muuza pombe hiyo alijitahidi kuokoa maisha yake kwa kumpatia huduma ya kwanza kwa kumpepea, kummwagia maji ya baridi na baadae akamnywesha uji lakini hali ilizidi kuwa tete na alipo kata roho mumewe Hasani Swalehe alitimua mbio na kumwacha marehemu akiwa juani.

Akizungumzia tukio hilo Mganga aliye ufanyia uchunguzi mwili wa Marehemu Kalesi Dkt, George Chiwangu alisema kuwa chanzo cha kifo hicho kilisababishwa na unywaji wa pombe nyingi.

Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Ruvuma Deusdedit Nsimeki amethibitisha kuwepo kwa tukio hilo na kuongeza kuwa kufuatia hali hiyo wanamshikilia mke wa muuza pombe huyo ambaye hakumtaja jina lake kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

Mwisho

Monday, April 29, 2013

LEMA AENDELEA KULA BATA BAADA YA KUPEWA DHAMANA

            Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema



MVUA nyepesi iliyonyesha kuanzia alfajiri, jana haikuwazui mamia ya wafausi wa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, kujitokeza kwa wingi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, wakati mbunge huyo alipofikishwa kusomewa shtaka la uchochezi.


Lema ambaye alikamatwa Ijumaa usiku kwa amri ya Mkuu wa Mkoa, Magesa Mulongo, na kuwekwa rumande kwa siku tatu, alifikishwa mahakamani saa tatu asubuhi akiwa katika gari dogo lenye vioo vyeusi likiwa na namba za usajili T 818 AJD.

Mbunge huyo alisindikizwa na askari wawili waliovaa suti wakiwa na silaha pamoja na Mkuu wa Upelelezi Mkoa (RCO).

Ilipofika saa nne, mbele ya Hakimu Devota Msofe, Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Elianenyi Njiro, alidai kuwa kesi hiyo ni mpya na inatajwa mara ya kwanza, angeomba asome mashtaka na ipangiwe tarehe nyingine.

Akisoma mashtaka hayo, alidai kuwa Aprili 24, mwaka huu, katika eneo la Freedom Square Chuo cha Uhasibu, Lema alichochea utendaji makosa na kukiuka kifungu 390 na 35 cha kanuni za dhabu sura ya 16 kama ilivyorekebishwa mwaka 2000.

Alitaja shtaka la Lema ni kutamka maneno: “Mkuu wa mkoa anakwenda kwenye ‘send off’, hajui chuo cha uhasibu mahali kilipo wala mauaji ya mwanafunzi wa chuo hiki. Ameshindwa kuwapa pole kwa kufiwa na kusikiliza shida zenu na anasema hawezi kuongea na wanafunzi wasio na nidhamu.” Alisisitiza kuwa maneno haya ndiyo yaliyosababisha kuvurugika kwa amani.

Baada ya kusoma shtaka hilo, aliongeza kuwa kwa upande wao hawana kipingamizi cha dhamana na hivyo hakimu Msofe alimuuliza wakili wa mshtakiwa, Method Kimomogolo, kama ana la kusema.

Kimomogolo alimueleza hakimu kuwa kwa vile maelezo ya shtaka hayaonyeshi kuelekea kwenye kutenda kosa, anaomba mshtakiwa aruhusiwe kujidhamini mwenyewe kwa kuwa ni mbunge wa Arusha, hivyo hawezitoroka.

Hakimu Devota alitaja masharti ya dhamana kuwa ni mdhamini mmoja mwenye kitambulisho na atakaesaini dhamana ya sh milioni moja ambapo Diwani wa Viti Maalumu (CHADEMA), Sabina Francis, aliitwa na Kimomogolo akamdhamini Lema baada ya kukidhi masharti hayo.

Mara baada ya kukamilika kwa taratibu hizo, hakimu Msofe aliahirisha kesi hiyo hadi Mei 29 itakapofika kwa ajili ya kutajwa tena.

Hali mahakamani

Lango la kuingilia katika chumba cha mahakama hiyo lilikuwa na askari sita ambapo watatu walivalia mavazi rasmi wakiwa na silaha na wengine wakiwa wanaangalia kila mtu anaekaribia hapo.

Askari wengine waliovalia kiraia walikuwa ndani ya chumba cha mahakama wakiratibu kila mtu aliyekuwemo ndani ambapo wengi waliokuwamo ni madiwani wa CHADEMA na waandishi wa habari.

Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nasari, alikaa na Lema wakibadilishana mawazo juu ya kilichotokea.


Nje ya mahakama ambako wananchi wengi walikuwa wamekusanyika, nako kulikuwa na askari wengi waliokuwa wamevalia kiraia.

Mbali na askari kanzu kujaa mahakamani hapo pia askari waliovalia sare wakiwa na gari tano huku wakisheheni silaha nzito pamoja na mabomu ya machozi walifanya doria mahakamani na maeneo ya barabara zote za kuelekea na kutoka eneo hilo.

Kulikuwa na magari yenye namba za usajili PT 2077, PT 1076, PT 2017 na PT 1844, zote zikiwa na askari wenye silaha kati ya saba na tisa wakizunguka maeneo yote jirani na Mahakama Kuu mjini Arusha wakati katika Kituo Kikuu cha Polisi kuliimarishwa ulinzi ambapo hakuna gari lililokuwa likiruhusiwa kuingia.

 

Lema ahutubia

Baada ya kesi kuahirishwa, wafuasi wa Lema waliandamana naye kutoka katika viwanja vya mahakama na kupitia ofisi ya mkuu wa mkoa wakishangilia hadi ofisi za CHADEMA mkoa.

Kutokana na wingi wa wafuasi hao ililazimu Lema kuzungumza nao katika kiwanja cha Shule ya Msingi Ngarenaro.

Aliwashukuru kwa kujitokeza kumuunga mkono na kuwasihi kuwa kamwe wasiwe waoga katika kutetea haki zao mpaka wahakikishe nchi inakombolewa.

Pia Lema alivishukuru vyombo vya habari kwa kuripoti ukweli halisi wa tukio na kusaidia kuepuka kubambikiwa mashtaka.

Alisema licha ya kuwekwa rumande lakini imemsaidia kujua masahibu mengi wanayoyapata mahabusu wanapokuwa sero, kwamba kuna mahabusu wana siku 26 hadi 40 hawajafikishwa mahakamani.

Alisema ameshangazwa kukuta chumba cha kukaa watu 20 wanalazwa watu 90 kitendo ambacho alidai kinahatarisha usalama wa mahabusu.

Lema alisema kuwa hatokwenda bungeni wiki yote ili apate muda wa kufanya mikutano ya hadhara huku akiwasisitizia wananchi wa Arusha mjini kumzomea mkuu wa mkoa popote atakapokwenda.

“Nasisitiza ilikuwa ni haki yake kuzomewa na wanafunzi wa Chuo cha Uhasibu kutokana na dharau alizozionyesha alipofika chuoni hapo na nawaambia wakazi wa Arusha kuendelea kumzomea popote atakapokwenda jimboni kwangu,’’ alisema.

Nao baadhi ya wananchi waliozungumza na gazeti hili baada ya Lema kuachiwa walimlalamikia mkuu wa mkoa wakisema ametumia madaraka vibaya pamoja na kumpotezea muda Lema wakati shtaka lenyewe halina mashiko.

Walisema kuwa ifike wakati uwekwe utaratibu wa kuwadhibiti viongozi kama hao wanaochezea kodi za wananchi kwa mambo yasiyo na msingi.

Naye Nasari alimuonya Mulongo kuacha tabia ya kuwadharau wabunge wa CHADEMA na kusema hali hiyo itamfanya ashindwe kuongoza mkoa huu.

Katibu wa CHADEMA Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa, mbali na suala hilo la Lema alitoa tamko la chama kuitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kupitia kwa Mkurugenzi wa Jiji kuiunganisha kata ya Sombetini katika uchaguzi mdogo utakaofanyika Juni 16.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), Hussein Bashe, amesema kuwa Mulongo alionyesha dharau ya wazi mbele ya wanafunzi wa Chuo cha Uhasibu jijini Arusha na kwamba hali hiyo inapaswa kulaaniwa na kila mmoja.

Bashe alisema kwa dharau hiyo ni dhahiri ameivunjia heshima serikali na kuwafanya wananchi kuongeza chuki zaidi dhidi ya CCCM.

Mjumbe huyo alitoa maoni hayo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Facebook wakati akijadili suala zima la kukamatwa kwa Lema pamoja na uamuzi wa baraza la madiwani wilayani Nzega mkoani Tabora kujitengea zaidi ya sh milioni 80 kwa ajili ya safari ya mafunzo jijini Arusha na Dodoma.

Alisema watu badala ya kutumia nguvu kubwa kuwatafuta wahalifu waliosababisha kifo cha mwanafunzi wa chuo hicho, wameamua kutengeneza mazingira ya kumkamata Lema.

“Kaka yangu Mulongo katika hili alivyolisimamia na kulitekeleza ameonyesha udhaifu wa hali ya juu na matokeo yake ni kuivunjia heshima serikali ya chama chetu na kuongeza chuki,” alisema.

Sunday, April 28, 2013

RC MANYANYA APEWA TUZO YA HESHIMA TANZANIA



Mbunge wa Viti Maalum (Ccm) Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa



Na, Stephano Mango, Songea
WAFANYAKAZI wa Sekta mbalimbali Halmashauri ya Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma wamelipongeza Baraza Kuu la Chama cha Wafanyakazi, Viwandani, Biashara, Taasisi za fedha, Huduma na Ushauri Tanzania (Tuico) kwa kitendo chake cha kuwatunuku vyeti vya uanachama wa Heshima baadhi ya wadau muhimu wa chama hicho akiwemo Mbunge wa Viti Maalum (Ccm) Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Mtandao wa www.stephanomango.blogspot.com  walisema kuwa katika nchi hii kuna baadhi ya Viongozi wanathamini sana juhudi za Wafanyakazi waliopo katika sekta mbalimbali kwa kuwashauri, kuwatia moyo na kushiriki kuyatatua matatizo yanayowakabili

Walisema kuwa Mhandisi Manyanya amekuwa kinara wa kuwatetea wafanyakazi toka alipokuwa anafanya kazi katika Shirika la Tanesco, hadi sasa akiwa katika nafasi ya Mbunge na Ukuu wa Mkoa wa Rukwa,

“Katika shughuli za kuwatetea Wafanyakazi kwa dhati ili aweze kujenga mshikamano zaidi katika Chama cha Tuico wanachama na Kamati mbalimbali waliamua kumchagua kuwawakilisha kwenye shughuli mbalimbali zitakazo sababisha maslahi bora ya wafanyakazi nchini” walisema

Walifafanua kuwa tuzo iliyotolewa inaheshimika sana katika Tuico kwani inatambua na kuthamini mchango wa mtu, uzoefu, busara, uamuzi, wa haki uliokifanya chama hicho kiweze kuendelea na kuwa na umoja na mshikamano miongoni mwa wanachama katika mambo mengi ikiwemo kutetea maslahi ya wafanyakazi ambao kimsingi ndio wanachama

Akizungumza kwa njia ya simu mara baada ya tafrija iliyofanyika Morogoro Mjini katika ukumbi wa Midland Inn, kuwatunuku wanachama Tuzo za heshima Mwenyekiti wa Tuico Taifa Omary Ayubu alisema kuwa chama chake kitakuwa kimekosa shukrani kwa wanachama wake ambao wametumia nguvu kubwa ya kutetea maslahi ya chama toka wamekuwa wanachama katika chama hicho

Ayubu alisema kuwa chama kimethamini na kitaendelea kuthamini ujuzi na juhudi walionao wanachama hao waliopewa tuzo katika kukiendeleza chama ili kiwe na tija kwa jamii ambayo inaitumikia na pia kwa maendeleo mapana ya Taifa

“Tumefanya hivyo baada ya kujifunza kwenye Mataifa ya wenzetu kama vile Zambia, Nigeria, Uholanzi, Ivory Cost, Afrika ya Kusini ambapo chama kimekuwa kikijisahau na kuepusha migogoro ikiwamo ya ndani na nje hivyo juwa tegemeo na heshima kubwa” alisema Ayubu

Aliwataja Wanachama hao ambao waliotunukiwa vyeti vya heshima na kupewa tuzo ni pamoja na Rc wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya(Mb), Mhadhili wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam Kitivo cha Sheria Profesa Issa Shivji, Felista Bulaya, Barozi Afred Tandau, Wakili Julius Bundala, Zephania Sumbe

Alizitaja majukumu ya wanachama mara baada ya kutunikiwa tuzo hizo kuwa ni pamoja na kushauri knuu8ongozi mambo ya kimaendeleo, kushiriki kampeni za kuelimisha jambo lolote linalohusu chama, kushiriki mikutano na kutoa michango, kutatua migogoro ya kichama, kujenga misimamo ya kichama na kuwakilisha jambo lolote ambalo chama kinataka kwa wakati wowote

Akizungumza kwa njia ya simu kwa niaba ya wanachama ambao wamebahatika kupata tuzo hizo za Mhandisi Stella Manyanya alisema sekta isiyo rasmi ya ajira ina zaidi ya watanzania milioni moja wanaohitaji kujengewa msingi imara juu ya haki zao za msingi ikiwamo mishahara na marupu rupu yanayokwenda sambamba na hali ya maisha

Manyanya alisema kuwa muda umefika sasa kwa vyama vya Wafanyakazi nchini kutumia tafiti na hesabu zilizotafitiwa kwa kina na kubainisha faida na hasara ili wanapoamua kudai haki zao waweze kusikilizwa kwa kina na madai yao kutafutiwa ufumbuzi na waajiri badala ya kukalia kubishana na kuburuzana mahakamani

Alisema kuwa wanachama wa Tuico wanapaswa kwa dhati kabisa kuzitambua haki zao za utumishi na kwamba Waandishi wa habari na vyombo vyao nchini kushiriki kikamilifu kukabiliana na changamoto zinazowakabili wafanyakazi hususani walioko kwenye sekta isiyo rasmi ili waweze kusaidia na uongozi uliopo

MWISHO

Friday, April 26, 2013

NI UJUMBE WA MAJONZI AMBAO UMEWALIZA WENGI ULIOTOLEWA NA JOSHUA NASSARI MBUNGE WA ARUMERU MASHARIKI KUHUSIANA NA POLISI KUPIGA MKWALA NYUMBANI KWA LEMA NA TISHIO LA KUKAMATWA KWAKE

Nimepata kwa mshtuko na nikakataa kuamini kama ni kweli kuwa polisi wa Arusha wamevamia na kuizingira nyumba ya mbunge mwenzangu wa Arusha, Lema.


Nimelazimika kumpigia simu RPC kuthibitisha na cha ajabu akaniambia ni kweli.

Nimemshauri kama kiongozi mwenzake mwenye dhamana ya kusaidia kuilinda

kweli na haki ili kuleta Amani ya kweli kwenye mkoa wangu wa Arusha. Sidhani kama ni busara kutaka kuvamia nyumbani kwa Raia mwema achilia mbali Kiongozi mkubwa kama mbunge. "Kama watawala wanafanya hivi kwa mti mbichi, itakuwaje kwa mti mkavu" itakuwaje kwa mwananchi wa kawaida anayeishi usa river au unga ltd? Ukifuatilia na kuangalia video ya tukio la uhasibu chuoni arusha, utagundua makosa ya mtawala mkuu wa mkoa, ambaye kimsingi ni mkiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa kuwa sehemu ya sababu ya uvunjifu wa amani, kutokujua hata kusoma saikolojia ya watu.

Nyumbani kwa mbunge hakai mbunge mwenyewe. Kuna watoto akiwemo mwenye umri wa miezi mitano, mke, ndugu etc. Utapigaje mabomu kwenye nyumba hii, bila shaka yatakuwa mauaji. Lema si jambazi, ni kiongozi, ni role model, ni raia mwema sana na mzalendo kwa taifa lake.

Hii wapi sababu ya kuvamia kwake usiku na kuwapa wanafamilia pychological tortue.

Kama amenielewa atasikia, otherwise "truth will always stand" . Tuko tayari na tulishakuwa tayari, hatujashtukizwa. Tunaendelea kuongezewa kura za madiwani arusha juni 16, 2013. Ni vyema watawala wakakumbuka habari ya Farao na Mungu juu ya mateso ya wana wa Israel utumwani. "Mungu akaufanya moyo wa farao kuwa mgumu, ili azidi kujidhihirisha kwa wana wa Israel"

MWISHO

Thursday, April 25, 2013

BABU UMESIKIKA, SHIRIKI KIKAMILIFU KUTATUA CHANGAMOTO ZINAZOLIKABILI JUKWAA



Na Stephano Mango, Songea

HIVI karibuni nilibahatika kutembelea Wilaya ya Rufiji iliyopo Mkoa wa Pwani kwa lengo la kwenda kujifunza namna Wakulima wa zao la Embe, Ufuta na Muhogo wanavyojihusisha na kilimo cha mazao hayo na tija yake katika ukombozi wa kiuchumi kwa jamii na Taifa kiujumla

Katika safari hiyo nilijifunza mambo mengi sana kuhusu kilimo cha mazao hayo ambayo yakiwekewa kipaumbele na wadau wake na Serikali, naamini kutokana na ushahidi uliopo kwa wakulima niliozungumza nao umaskini ungepungua kwa asilimia kubwa kwenye kaya nyingi zinazojihusisha na kilimo cha mazao hayo

Nina mengi sana ya kuelezea, lakini naomba wasomaji kwa leo nizungumzie ushirikiano uliopo kati ya Wakulima wa Embe, Ufuta na Muhogo, Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Nurdin Babu na Wasimamizi wa Mradi wa Muvi Mkoa wa Pwani

Hakika ushirikiano huo utawezesha uzalishaji wa mazao hayo kuongezeka na upatikanaji wa masoko yenye uhakika kwani jukwaa ambalo wameliunda litawezesha kukabiliana na changamoto zilizopo na kusababisha upatikanaji wa maslahi bora

Jukwaa hilo ni muhimu sana katika maendeleo ya kilimo cha mazao hayo kwani watapata muda wa kujadiliana juu ya fursa, matatizo na changamoto wanazokabiliana nazo ili kuongeza tija kwa kila mmojawapo na kuepukana na unyonyaji unaofanywa na baadhi ya wajanja wachache kwenye minyororo ya thamani ya mazao hayo

Ili kulinda hali hiyo wajasiliamali hao wanalelewa kwa kiasi kikubwa sana na Mradi wa Muunganiko wa Wajasiriamali Vijijini (MUVI) ulioibuliwa kutekelezwa katika mikoa sita ya Tanzania bara, ukiwemo Mkoa wa Pwani na Ruvuma.

Kupitia mkopo ambao Serikali ya Tanzania ilipata toka shirika la IFAD ili kuinua hali duni ya wananchi wake ambapo fedha hizo ziko chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara katika shirika la SIDO kama watekelezaji wakuu

Mradi wa MUVI-Pwani unalenga kuwawezesha wajasiriamali wadogowadogo ili kuendeleza biashara zao zitakazo wawezesha kuinua vipata vyao ambapo mojawapo ya uwezeshwaji huo, ni kuimarisha ushiriki wa wadau mbalimbali katika minyororo ya thamani ya muhogo na embe, ili kuimarisha na kuongeza ubora wa mazao hayo.

Hivyo basi jukwaa la Majadiliano la wadau wa embe, muhogo na ufuta ni miongoni mwa jitihada za MUVI kwa kushirikiana na Halmashauri na wadau mbalimbali katika minyororo ya thamani ya mazao hayo ili kuwa na sehemu ya kukutana na kujadiliana namna ya kutatua kero mbalimbali

Kutokana na umuhimu huo Machi 26 mwaka huu, wadau hao walikutana mji mdogo wa Ikwiriri Wilayani Rufiji mkoani Pwani

Lengo likiwa wadau wakupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa Mradi wa MUVI Pwani pia kupokea taarifa za wadau mbali mbali katika minyororo ya thamani ya embe, muhogo na ufuta. Kamati zilizotoa taarifa ni kamati ya wazalishaji, wasindikaji, pembejeo, fedha na mitaji.

Katika mkutano huo ambao uliwashirikisha wadau wengi zikiwemo taasisi za fedha ikiwemo Benki ya CRDB, watafiti, wasindikaji vyakula, wataalamu na viongozi wa Halmashauri ya wilaya na wadau wengine

Kwenye mkutano huo Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Nurdin Babu alialikwa kuwa mgeni rasmi ambapo pamoja na mambo mengine aliyoyasema ni pamoja na … Nia yetu kubwa ya kukusanyika hapa leo hii, ni kwa ajili ya kufanya tathimini kupitia Jukwaa la Majadiliano kuhusu changamoto zinazokabili mazao matatu ambayo ni, embe, muhogo na ufuta

Pia alisema kwa fursa ya pekee tuliyoipata leo, ni vizuri tuzungumzie zaidi mazao ya muhogo na embe ambayo yana wanyonyaji wengi sana pasipo kujali nguvu nyingi inayotumiwa na wazalishaji hususani wakulima. Ninawasihi sana, tuuze mazao haya kwa faida za maendeleo kama vile kusomesha watoto, kujenga nyumba nzuri za kudumu na mambo mengine ya muhimu na si kuoa wake wengi wanaopelekea kuzorota kwa maendeleo.

“ Ndugu wakulima, siwezi kujitenga nanyi nawaahidi ushirikiano wa bega kwa bega ili tuweze kufikia malengo ya maendeleo endelevu ya wilaya yetu na watanzania kwa ujumla” alisema Babu

Hayo ndio yaliyonifanya niyatafakari kwa muda wa zaidi ya wiki mbili na kulazimika kuyaweka katika ukurasa huu ili wadau popote walipo waweze kuyajadili na kuyaenzi kwa maslahi ya jamii pana zaidi na Taifa kiujumla

Ni dhahiri wanarufiji wamejitahidi sana kuunda Jukwaa la Majadiliano la Wadau wa Muhogo, ufuta na Embe Rufiji ambalo lina malengo mbalimbali ambapo lengo kuu ni kuzalisha kwa wingi na kutetea thamani ya zao hilo katika masoko

Katika mradi huo wa Muvi unakabiliwa na changamoto ambazo zinapaswa kutatuliwa kwa haraka ili kuweza kuleta matokeo chanya kwenye Jukwaa hilo, na hapa ndipo ninapomuweka wazi Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Nurdin Babu kushiriki kwa kina ndani na nje ya Serikali ili kufikia malengo ya wakulima hao, kwani alichokisema kwenye hotuba yake ya ufunguzi kimesikika

Na kilichobaki yeye kushiriki kutatua changamoto zinazowakabili wakulima hao ili kuweza kufikia malengo stahiki ya wanajukwaa ambao wanamatumaini mbalimbali katika jitihada za kilimo cha mazao hayo

Kwa mujibu wa taarifa ya utekelezaji wa Muvi Mkoa wa Pwani 2012/2013 kuna changamoto ambazo zinawakwaza kufikia malengo yao kwa wakati ikiwemo ,Mbinu za kisasa za uzalishaji ni mdogo, Ukosefu wa soko la mkataba, Kuinua kiwango cha usindikaji, Uzalishaji na usambazaji wa mbegu bora, Tozo zilizo na tija kwa wajasiliamali

Katika hilo ni vema Serikali mkoani Pwani ikajipanga kikamilifu kutatua changamoto hizo na jukumu kubwa la wanajukwaa kila mmoja kutimiza wajibu wake kwani Jukwaa la Majadiliano kwa mazao ya biashara ni muhimu sana kwa sababu wadau mbali mbali wanashirikishwa kuanzia ngazi ya chini hadi ya juu

Katika swala la huduma za fedha Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Ruvuma Devotha Likokola ambaye pia ni Mkurugenzi wa Vikoba Tanzania alikuwa ni miongoni mwa watu waliotoa mada siku hiyo

Pamoja na mambo mengine alisikika akiwashauri wanajukwaa kwa kusema ,,, huduma za fedha zilizo rasmi ni (12%) na wengine wanapata huduma zisizo rasmi. Aliendelea kwa kuzielezea huduma za fedha zinazotolewa na mabenki kama ya CRDB, NBC na NMB kuwa ni huduma rasmi kwa sababu zinasimamiwa na Benki Kuu ya Tanzania (B.O.T).

Likokola alisema kuwa huduma ambazo si rasmi alizitolea mfano kuwa ni SACCOS, FINCA, PRIDE, SELF, TUNAKOPESHA, na nyinginezo ambazo zinajumuisha (34%). Aidha aliendelea kwa kusema kwamba (36%) hawapo katika upande wowote iwe rasmi ama si rasmi.

Alizitaja njia kuu tatu (3) ambazo zinaweza kumpatia mtu pesa; nazo ni kufanya kazi/kilimo, kuajiriwa na kuwekeza na kuwataka kwamba wana Rufiji wakitaka kupatapesa, ni lazima wawe na pesa kwa kujiunga kwenye vikundi hasa Village Community Bank (VICOBA).

Kwa leo ninachoweza kusema tuanze upya kwa kuwa wajasiriamali mahiri chini ya Jukwaa bunifu kwani ujasiriamali ni ile hali, uwezo na mkakati au mchakato wa kubuni, kuanzisha, kuendesha na kumudu shughuli halali ya maendeleo ya kiuchumi

Tunahitaji ujasiliamali wa kujiamini, kuthubutu, kubuni na kuendeleza zao tokeo la ubunifu huo kwa kuleta faida chanya katika maisha yake, jamii na Taifa kiujumla kwani ujasiliamali ni nguzo muhimu kwa uchumi wa kisasa wa karne ya 21

Dhana ya ujasiliamali inatimia endapo hali ya kugundua au kubuni biashara mpya au kuiendeleza ile ya zamani kwa ajili ya kuwekeza na kutoa huduma stahiki kwa jamii pana, hivyo tuamue sasa kuwa katika hali hiyo katika jukwaa la dunia ili kuzifaidi fursa za uchumi za ndani na nje ya nchi

Uchumi wa dunia umebadilika, uchumi wa soko katika utandawazi ndio unashikilia mfumo wa kiuchumi wa dunia ili kuharakisha maendeleo kwa kutoa ajira mbadala kwa kujiajili, kujitegemea na kujenga uwezo wa kujiamini katika maisha na biashara kubwa dhana ya ujasiliamali chini ya Jukwaa inahitajika

Wahenga walisema huwezi kuzuia sikio lako kusikia lakini unaweza kuzuia mdomo wako usiseme, nami kwa hakika nasema nauzuia mkono wangu usiandike zaidi lakini siwezi kukuzuia msomaji kuendelea kusoma

Mwandishi wa Makala

Anapatikana 0715-335051

www.stephanomango.blogspot.com
DC BABU UMESIKIKA, SHIRIKI KIKAMILIFU KUTATUA CHANGAMOTO ZINAZOLIKABILI JUKWAA


Na Stephano Mango, Songea

HIVI karibuni nilibahatika kutembelea Wilaya ya Rufiji iliyopo Mkoa wa Pwani kwa lengo la kwenda kujifunza namna Wakulima wa zao la Embe, Ufuta na Muhogo wanavyojihusisha na kilimo cha mazao hayo na tija yake katika ukombozi wa kiuchumi kwa jamii na Taifa kiujumla

Katika safari hiyo nilijifunza mambo mengi sana kuhusu kilimo cha mazao hayo ambayo yakiwekewa kipaumbele na wadau wake na Serikali, naamini kutokana na ushahidi uliopo kwa wakulima niliozungumza nao umaskini ungepungua kwa asilimia kubwa kwenye kaya nyingi zinazojihusisha na kilimo cha mazao hayo

Nina mengi sana ya kuelezea, lakini naomba wasomaji kwa leo nizungumzie ushirikiano uliopo kati ya Wakulima wa Embe, Ufuta na Muhogo, Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Nurdin Babu na Wasimamizi wa Mradi wa Muvi Mkoa wa Pwani

Hakika ushirikiano huo utawezesha uzalishaji wa mazao hayo kuongezeka na upatikanaji wa masoko yenye uhakika kwani jukwaa ambalo wameliunda litawezesha kukabiliana na changamoto zilizopo na kusababisha upatikanaji wa maslahi bora

Jukwaa hilo ni muhimu sana katika maendeleo ya kilimo cha mazao hayo kwani watapata muda wa kujadiliana juu ya fursa, matatizo na changamoto wanazokabiliana nazo ili kuongeza tija kwa kila mmojawapo na kuepukana na unyonyaji unaofanywa na baadhi ya wajanja wachache kwenye minyororo ya thamani ya mazao hayo

Ili kulinda hali hiyo wajasiliamali hao wanalelewa kwa kiasi kikubwa sana na Mradi wa Muunganiko wa Wajasiriamali Vijijini (MUVI) ulioibuliwa kutekelezwa katika mikoa sita ya Tanzania bara, ukiwemo Mkoa wa Pwani na Ruvuma.

Kupitia mkopo ambao Serikali ya Tanzania ilipata toka shirika la IFAD ili kuinua hali duni ya wananchi wake ambapo fedha hizo ziko chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara katika shirika la SIDO kama watekelezaji wakuu

Mradi wa MUVI-Pwani unalenga kuwawezesha wajasiriamali wadogowadogo ili kuendeleza biashara zao zitakazo wawezesha kuinua vipata vyao ambapo mojawapo ya uwezeshwaji huo, ni kuimarisha ushiriki wa wadau mbalimbali katika minyororo ya thamani ya muhogo na embe, ili kuimarisha na kuongeza ubora wa mazao hayo.

Hivyo basi jukwaa la Majadiliano la wadau wa embe, muhogo na ufuta ni miongoni mwa jitihada za MUVI kwa kushirikiana na Halmashauri na wadau mbalimbali katika minyororo ya thamani ya mazao hayo ili kuwa na sehemu ya kukutana na kujadiliana namna ya kutatua kero mbalimbali

Kutokana na umuhimu huo Machi 26 mwaka huu, wadau hao walikutana mji mdogo wa Ikwiriri Wilayani Rufiji mkoani Pwani

Lengo likiwa wadau wakupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa Mradi wa MUVI Pwani pia kupokea taarifa za wadau mbali mbali katika minyororo ya thamani ya embe, muhogo na ufuta. Kamati zilizotoa taarifa ni kamati ya wazalishaji, wasindikaji, pembejeo, fedha na mitaji.

Katika mkutano huo ambao uliwashirikisha wadau wengi zikiwemo taasisi za fedha ikiwemo Benki ya CRDB, watafiti, wasindikaji vyakula, wataalamu na viongozi wa Halmashauri ya wilaya na wadau wengine

Kwenye mkutano huo Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Nurdin Babu alialikwa kuwa mgeni rasmi ambapo pamoja na mambo mengine aliyoyasema ni pamoja na … Nia yetu kubwa ya kukusanyika hapa leo hii, ni kwa ajili ya kufanya tathimini kupitia Jukwaa la Majadiliano kuhusu changamoto zinazokabili mazao matatu ambayo ni, embe, muhogo na ufuta

Pia alisema kwa fursa ya pekee tuliyoipata leo, ni vizuri tuzungumzie zaidi mazao ya muhogo na embe ambayo yana wanyonyaji wengi sana pasipo kujali nguvu nyingi inayotumiwa na wazalishaji hususani wakulima. Ninawasihi sana, tuuze mazao haya kwa faida za maendeleo kama vile kusomesha watoto, kujenga nyumba nzuri za kudumu na mambo mengine ya muhimu na si kuoa wake wengi wanaopelekea kuzorota kwa maendeleo.

“ Ndugu wakulima, siwezi kujitenga nanyi nawaahidi ushirikiano wa bega kwa bega ili tuweze kufikia malengo ya maendeleo endelevu ya wilaya yetu na watanzania kwa ujumla” alisema Babu

Hayo ndio yaliyonifanya niyatafakari kwa muda wa zaidi ya wiki mbili na kulazimika kuyaweka katika ukurasa huu ili wadau popote walipo waweze kuyajadili na kuyaenzi kwa maslahi ya jamii pana zaidi na Taifa kiujumla

Ni dhahiri wanarufiji wamejitahidi sana kuunda Jukwaa la Majadiliano la Wadau wa Muhogo, ufuta na Embe Rufiji ambalo lina malengo mbalimbali ambapo lengo kuu ni kuzalisha kwa wingi na kutetea thamani ya zao hilo katika masoko

Katika mradi huo wa Muvi unakabiliwa na changamoto ambazo zinapaswa kutatuliwa kwa haraka ili kuweza kuleta matokeo chanya kwenye Jukwaa hilo, na hapa ndipo ninapomuweka wazi Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Nurdin Babu kushiriki kwa kina ndani na nje ya Serikali ili kufikia malengo ya wakulima hao, kwani alichokisema kwenye hotuba yake ya ufunguzi kimesikika

Na kilichobaki yeye kushiriki kutatua changamoto zinazowakabili wakulima hao ili kuweza kufikia malengo stahiki ya wanajukwaa ambao wanamatumaini mbalimbali katika jitihada za kilimo cha mazao hayo

Kwa mujibu wa taarifa ya utekelezaji wa Muvi Mkoa wa Pwani 2012/2013 kuna changamoto ambazo zinawakwaza kufikia malengo yao kwa wakati ikiwemo ,Mbinu za kisasa za uzalishaji ni mdogo, Ukosefu wa soko la mkataba, Kuinua kiwango cha usindikaji, Uzalishaji na usambazaji wa mbegu bora, Tozo zilizo na tija kwa wajasiliamali

Katika hilo ni vema Serikali mkoani Pwani ikajipanga kikamilifu kutatua changamoto hizo na jukumu kubwa la wanajukwaa kila mmoja kutimiza wajibu wake kwani Jukwaa la Majadiliano kwa mazao ya biashara ni muhimu sana kwa sababu wadau mbali mbali wanashirikishwa kuanzia ngazi ya chini hadi ya juu

Katika swala la huduma za fedha Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Ruvuma Devotha Likokola ambaye pia ni Mkurugenzi wa Vikoba Tanzania alikuwa ni miongoni mwa watu waliotoa mada siku hiyo

Pamoja na mambo mengine alisikika akiwashauri wanajukwaa kwa kusema ,,, huduma za fedha zilizo rasmi ni (12%) na wengine wanapata huduma zisizo rasmi. Aliendelea kwa kuzielezea huduma za fedha zinazotolewa na mabenki kama ya CRDB, NBC na NMB kuwa ni huduma rasmi kwa sababu zinasimamiwa na Benki Kuu ya Tanzania (B.O.T).

Likokola alisema kuwa huduma ambazo si rasmi alizitolea mfano kuwa ni SACCOS, FINCA, PRIDE, SELF, TUNAKOPESHA, na nyinginezo ambazo zinajumuisha (34%). Aidha aliendelea kwa kusema kwamba (36%) hawapo katika upande wowote iwe rasmi ama si rasmi.

Alizitaja njia kuu tatu (3) ambazo zinaweza kumpatia mtu pesa; nazo ni kufanya kazi/kilimo, kuajiriwa na kuwekeza na kuwataka kwamba wana Rufiji wakitaka kupatapesa, ni lazima wawe na pesa kwa kujiunga kwenye vikundi hasa Village Community Bank (VICOBA).

Kwa leo ninachoweza kusema tuanze upya kwa kuwa wajasiriamali mahiri chini ya Jukwaa bunifu kwani ujasiriamali ni ile hali, uwezo na mkakati au mchakato wa kubuni, kuanzisha, kuendesha na kumudu shughuli halali ya maendeleo ya kiuchumi

Tunahitaji ujasiliamali wa kujiamini, kuthubutu, kubuni na kuendeleza zao tokeo la ubunifu huo kwa kuleta faida chanya katika maisha yake, jamii na Taifa kiujumla kwani ujasiliamali ni nguzo muhimu kwa uchumi wa kisasa wa karne ya 21

Dhana ya ujasiliamali inatimia endapo hali ya kugundua au kubuni biashara mpya au kuiendeleza ile ya zamani kwa ajili ya kuwekeza na kutoa huduma stahiki kwa jamii pana, hivyo tuamue sasa kuwa katika hali hiyo katika jukwaa la dunia ili kuzifaidi fursa za uchumi za ndani na nje ya nchi

Uchumi wa dunia umebadilika, uchumi wa soko katika utandawazi ndio unashikilia mfumo wa kiuchumi wa dunia ili kuharakisha maendeleo kwa kutoa ajira mbadala kwa kujiajili, kujitegemea na kujenga uwezo wa kujiamini katika maisha na biashara kubwa dhana ya ujasiliamali chini ya Jukwaa inahitajika

Wahenga walisema huwezi kuzuia sikio lako kusikia lakini unaweza kuzuia mdomo wako usiseme, nami kwa hakika nasema nauzuia mkono wangu usiandike zaidi lakini siwezi kukuzuia msomaji kuendelea kusoma

Mwandishi wa Makala

Anapatikana 0715-335051

www.stephanomango.blogspot.com

RC ARUSHA AAGIZA LEMA AKAMATWE KWA UCHOCHEZI

MKUU wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo ameliagiza Jeshi la Polisi mkoani humo, kumkamata Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema akihusishwa na uchochezi wa vurugu zilizotokea katika Chuo cha Uhasibu kilichopo Njiro jijini Arusha jana asubuhi.

Mulongo alithibitisha kukamatwa kwa mwanasheria wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Albert Msando ambaye anadaiwa kuwepo chuoni hapo na Lema pamoja na baadhi ya wanafunzi wanaodaiwa kuwa vinara wa vurugu hizo.

Vurugu hizo zilitokea jana saa nne asubuhi baada ya Mkuu wa Mkoa kufika chuoni hapo kwa ajili ya kuwasikiliza wanachuo ambao walitaka kuandamana kufuatia mwenzao Elly Kago (22) kuuawa na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia jana jirani na chuo.

Mulongo alifika chuoni hapo baada ya kupigiwa simu na Lema ambaye alifika mapema na kuzungumza na wanafunzi hao, huku akiwatuliza wasiandamane kufuatia kifo cha mwenzao.

Lema aliwaambia vijana hao kuwa mazingira ya nchi ya sasa ni magumu kufuatia wengi wao kukosa ajira na hivyo baadhi yao wasio wastahamilivu kujiingiza katika vitendo vya ujambazi na unyang'anyi.

Hivyo aliwataka wasiwe na jazba badala yake watafute ufumbuzi wa matukio hayo na kuangalia jinsi ya kumsitiri mwenzao.

Baada ya Mulongo kufika na kuwakuta wanafunzi wakizungumza na Lema, alipewa nafasi naye kuzungumza, lakini aliutaka uongozi wa chuo kuandaa vipaza sauti na mahala pazuri pa kuzungumzia.

Maelekezo hayo ya mkuu wa mkoa kutaka vipaza sauti yaliamsha maneno ya chini kwa chini na baada ya kuanza kuzungumza wanafunzi hao walianza kumzomea wakimlazimisha aache.

Alipokatisha hotuba yake, wanafunzi walianza kurusha mawe na hivyo kulazimika kuondolewa chuoni hapo pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali chini ya ulinzi, huku mabomu yakirindima kuwatawanya wanafunzi hao.

Wanafunzi hao walisikika wakisema mkuu huyo ‘amewaboa’ kwa kuwa wao wana msiba yeye anaenda kudai vipaza sauti ili kusikiliza madai yao, huku akiwa amevaa suti, hatua iliyotafsiriwa kama kutojali msiba wao.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mbele ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama, Mulongo alisema wameuagiza uongozi wa chuo hicho kukifunga kwa muda usiojulikana kwa ajili ya usalama.

Alisema taarifa za awali za polisi zinasema kuwa vurugu na kifo cha mwanafunzi huyo vina mahusiano makubwa na masuala ya kisiasa kwa ajili ya watu kujijenga kisiasa na kwamba vyombo vya usalama vinaendelea na uchunguzi wa kina juu ya suala hilo.

Mkuu huyo wa mkoa hakutaja idadi ya wanafunzi waliokamatwa hadi jana bali alisema vinara wote wamekamatwa pamoja na Msando huku akisisitiza kuwa Lema ametoroka na anaendelea kusakwa.

“Jambo baya kwa leo ni siasa kuingia katika vurugu hizo, kwani Lema ndiye alihusika hata kuita viongozi wa serikali chuoni hapo ambapo aliingia hapo bila kufuata utaratibu na kuanza kuzungumza na wanafunzi,’’ alisema Mulongo.

Kaimu Mkuu wa Chuo, Dk. Faraji Kasida baada ya kupewa maagizo ya kukifunga chuo hicho ambacho kipo chini ya Wizara ya Fedha alitangaza kuwa kimefungwa kwa muda usiojulikana.

Vurugu hizi zimeibuka zikiwa zimebaki siku chache kabla ya kuanza kwa kampeni za uchaguzi mdogo wa madiwani katika kata nne za Jiji la Arusha.

Liwale balaa

Mwandishi Wetu kutoka Liwale anaripoti kuwa wananchi wasiojulikana wamechoma moto ofisi na nyumba za mbunge wa Liwale mkoani Lindi, Faith Mitambo pamoja na nyumba za viongozi wa CCM na wa vyama vya ushirika vya msingi kwenye mji wa Liwale.

Tukio hilo la aina yake lilitokea juzi likianzia katika Kijiji cha Liwale B ambako wakulima wa Chama cha Msingi cha Minali walikataa malipo ya korosho ya sh 200 kwa kilo yakiwa ya pili badala ya sh 600 waliyoahidiwa mwaka jana.

Kwa mujibu wa Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, Advera Senso, vurugu hizo zilitokea saa tisa alasiri, huko wilayani Liwale ambapo kundi la watu wanaodhaniwa kuwa wakulima wa korosho walijaribu kuzuia gari lililokuwa na malipo.

Alisema kuwa wakulima hao walikuwa wakipinga malipo ya pili ya korosho na hivyo kuanza kufanya vurugu na uharibifu mkubwa wa mali.

Senso alisema hadi jana taarifa za awali zilionesha kuwa nyumba 14 zilichomwa moto, baadhi ya mifugo ilijeruhiwa na kuangamizwa na kufanyika uharibifu wa miundombinu ya barabara.

Alisema kufuatia tukio hilo, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Said Mwema alituma timu maalumu ikiongozwa na Kaimu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini (DCP), Issaya Mngulu kwenda kuongeza nguvu kwa kushirikiana na uongozi wa mkoa.

“Lengo ni kuhakikisha kuwa hali ya amani na utulivu inarejea haraka na wale wote waliohusika kufanya vitendo vya uhalifu wanakamatwa na kufikishwa mahakamani ili sheria iweze kuchukua mkondo wake. Hadi sasa watuhumiwa 19 wamekamatwa kwa mahojiano,” alisema.

Wakati taarifa za polisi zikieleza hivyo, mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa Mwenyekiti wa chama hicho cha ushirika, Mohamed Limbwilindi alikwenda kijijini hapo akiwa na sh milioni 61.4 ambazo wakulima hao wangelipwa sh 200 kwa kila kilo ya korosho.

Kwamba wengine ambao hawakupewa malipo ya awali walielezwa kuwa watalipwa sh 800, jambo ambalo lilizua mtafaruku miongoni mwao na hivyo kurudisha fedha.

Kutokana na hali hiyo, ilielezwa kuwa wananchi wenye hasira walianza kukateketeza moto ofisi ya chama hicho na nyumba ya mwenyekiti kisha pia nyumba ya katibu wake, Juma Majivuno.

Baada ya vurugu hizo huko Liwale B, alasiri vurugu hizo zilihamia mjini Liwale ambako uharibifu mkubwa wa mali ulifanyika.

Wananchi hao walichoma ofisi ya mbunge, duka la pembejeo la Hassan Mpako, ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Msingi cha Umoja mjini Liwale pamoja na nyumba yake.

Akizungumzia tukio hilo, Mpako alisema; “niliona kundi kubwa la watu wanakuja nyumbani kwangu saa 3 usiku wakiwa wamebeba nondo, mawe pamoja na madumu ambayo nadhani yalikuwa na petroli,” alisema.

Mpako alifafanua kuwa watu hao walimweleza; “tunataka fedha zetu za korosho” mazingira aliyodai kuwa yalimlazimisha atimue mbio ili kujisalimisha.

Alisema watu hao waliteketeza nyumba yake pamoja na trekta dogo la mkono, pikipiki, jenereta pamoja akiba ya pembejeo za kilimo ambazo zilikuwa dukani.

Wengine waliochomewa nyumba ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya, Mohamed Ngomambo ambaye alisema anamwachia Mungu.

“Kama nimepoteza wazazi ambao wana thamani kubwa maishani mwangu nyumba ni kitu gani?” alisema Ngomambo.

Kutokana na vurugu hizo, kundi kubwa la askari wa kutuliza ghasia (FFU) toka Lindi limewasili wilayani Liwale kudhibiti hali ya usalama ambayo imetoweka.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, George Mwakajinga alizungumza kwa simu akisema kuwa mbunge wa Liwale nyumba zake mbili na ofisi vilichomwa moto.

Pia Mwenyekiti wa CCM Wilaya, Chande nyumba yake moja ilichomwa moto huku mwenyekiti wa Halmashauri ya Liwale, Abasi Matulilo naye nyumba yake ilichomwa.

“Meneja wa Chama cha Msingi cha Ilulu, Hamza Mkungura nyumba zake mbili ziliteketezwa na duka la dawa na pembejeo vile vile yaliteketezwa huku mifugo ikijeruhiwa na kuchinjwa,” alisema.

Kamanda aliwataja wengine walioathirika na vurugu hizo kuwa ni meneja mikopo wa NMB, Mohamedi Pimbi ambaye duka lake la vifaa vya umeme lilichomwa pamoja na duka la Kanisa Katoliki.

Aliwataja pia Diwani wa CCM, Hasan Muyao na Diwani wa Viti Maalumu Amina Mnocha kuwa nyumba zao zilichomwa pamoja na nyumba ya mjumbe wa NEC wa chama hicho, Hemedi Ngonani ambaye aliharibiwa maduka ya simu na vyakula.





Tuesday, April 23, 2013

MKIA MIWILI YA TEMBO YAMSABABISHIA KUSHIKILIWA NA POLISI RUVUMA

Na Gideon Mwakanosya,Songea.


JESHI la Polisi mkoani Ruvuma linawashikilia watu wa tano kwa matukio tofauti likiwemo la watu wawili kukamatwa na mikia miwili ya Tembo ,Risasi tatu na kichwa kimoja cha bunduki aina ya Rifle huku tukio la pili ni mtu moja kukamatwa na bangi kilo 50 na miche ya bangi yenye uzito wa kilo 62 wakati tukio la tatu yote ya wizi wa pikipiki huku pikipiki mbili ziliibiwa jijini Dare-Esalaam na moja ya mjini Songea mkoani Ruvuma.

Watuhumiwa wanaoshikiliwa na polisi katika matukio matatu tofauti ni Rashidi Kapesa [29] Teofanesi Mapunda [29] Eleneus Mapunda [37] Bakari Milanzi [40] na Yahaya Rajabu umri wake haukutajwa

Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake kamanda wa polisi mkoani Ruvuma Deusdedit Nsimeki alisema kuwa tukio la kuwakamata watuhumiwa na mikia ya Tembo lilitokea Aprili 18mwaka huu majira ya 1.30 jioni baada ya askari wanyama pori Hassani Mihuka alipokuwa doria na wenzake waliwakamata Rashidi Kapesa [29]mkazi wa kijiji cha Mandepwende na Teofanesi Mapunda [29]mkazi wa kjiji cha Mtonya .

Kamanda wa polisi alisema kuwa watuhumiwa hao waliokamatwa eneo la kambi ya watu wakujenga barabara Progressive lililopo Mchomolo wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma ambao walikutwa na mikia 2 ya Tembo ,Risasi 3 kichwa kimoja cha bunduki aina ya Rifle kilichokuwa kimefichwa ndani ya begi.

Kamanda Nsimeki alisema kuwa mnamo Aprili 20 mwaka huu mjira ya saa kumi jioni huko katika kijiji cha Ngahokola mashambani wilayani Songea ambako askari polisi wakiwa kwenye doria yao ya kila siku walifanikiwa kumkamata Eleneusi Mapunda akiwa na bangi kiasi cha kilo 50 na miche ya bangi yenye uzito wa kilo 62.

Alifafanua zaidi kuwa katika tukio lingine inadaiwa kuwa mnamo Marchi 7 mwaka huu katika muda usiofahamika kwenye eneo la Lizaboni manispaa ya Songea polisi ilifanikiwa kumtia mbaloni Bakari Milanzi [40]aliwa na pikipiki yenye namba za usajili T354 BNZ SANLG na baada ya uchunguzi yakinifu ilibainika kuwa namba halisi za usajili wa pikipiki hiyo ni T 775 BWC mali ya Teodora Sephan Mtweve wa jijini Dare –Esalaam ambaye inadaiwa pikipiki yake iliibiwa tangu mwezi Julai 2012 katika eneo la Kimara baada ya mwendesha bodaboda huyo kuporwa na mtu asiye fahamika.

Kanda alilitaja tukio lingine kuwa inadaiwa mnamo Marchi 7 nwaka huu askari polisi walio kuwepo eneo la doria la Lizaboni manispaa ya Songea mtuhumiwa Yahaya Rajabu alikamatwa na pikipiki yenye namba za usajili T 557 BYR aina ya SANLG ambayo baada ya kufanya uchunguzi ilibainika kuwa namba zake halisi za usajili kuwa ni T 7551 BSY ambayo mmiriki wake halisi ni Rose Gerevas Makene mkazi wa jijini Dare –Esalaam ambaye pikipiki hiyo iliibiwa katika maeneo ya Kimara Julai 7 mwaka 2012 baada ya mwendesha bodaboda huyo kuporwa na watu wasiofahamika.

Aidha alilitaja tukio jingine kuwa mnamo Februari mwaka huu khuko katika wilaya ya Tunduru askari wakiwa kwenye doria walifanikiwa kukamata pikipiki yenye namba za usajiri T.736 aina ya SANLG ambayo baada ya polisi kufanya uchunguzi wa kina ilibainika kuwa namba hizo kuwa ni bandia hivyo namba halisi za usajili wa pikipiki hiyo kuwa ni T 787 CDL na kuwa ni mali ya Isdori Mdolino mkazi wa Songea mjini ambayo inadaiwa iliibiwa Januari 26 mwaka huu. na baada ya mwendasha bodaboda kuporwa na kuwa watuhumiwa watafikishwa mahakani mara baada ya upelelezi kukamilika.

MWISHO.

TAFAKARI MAANDIKO HAYA KWA AFYA YA AKILI YAKO

Umaarufu au Udhaifu Haulazimishwi, Bali Unajithibitisha Wenyewe!


Ukweli siku zote ni lazima ubakie ukweli, watu wengi mara kwa mara wamejitahidi kurudia uongo na hata wakati mwingine uongo huo ukiandamana na vitendo vya uhalifu wa kupangwa ili mradi tu kuuhalalisha uongo huo! Yote hii ni kujitahidi kuficha ukweli, lakini ukweli siku zote haupotei, unaweza kujificha kwa kipindi kifupi lakini mwishowe ni lazima ujitokeze.

Kuna wanasiasa mchwara ambao wanadhani kutumia magenge ya uhalifu wa kupangwa kwa kuwadhuru waandishi wa habari na wale wote wanaoonekana kuwa wawazi wa kujieleza na kutoa maoni yao juu hali halisi ya kisiasa na kiuchumi hapa nchini, ndiyo watakuwa wamefanikiwa kuuficha udhaifu wao usijulikane mbele ya jamii! Hizi ni fikra dhaifu zisizokuwa na maono ya mbali kwa vile udhaifu au umaarufu wa mtu hudhihirishwa na mtu mwenyewe, na wala haudhihirishwi na mwandishi wa habari, chombo cha habari wala mtu yeyote zaidi ya wewe mwenyewe! Hivyo kuwaandama waandishi au watu wanaoonekana kujua udhaifu wako haina maana kwamba ukimaliza kuwaangamiza ndiyo umeimarisha umaarufu wako, hapana, bali utakuwa umezidi kujidhoofisha!

Tukirudi nyuma kwenye uchaguzi wa mwaka 2005 lile genge la uhalifu wa kupangwa ambalo lina matawi hata huko kwenye nyombo vya habari; lilipomchafua Dr. Salim Ahmed Salim ili aonekane hafai mbele ya jamii kuwania kile kiti cha kula bila kuulizwa unakulaje? Genge hili lilidhani limemdhoofisha Dr. Salim moja kwa moja lakini kiukweli limemuimarisha, na limejikuta ule upande lililokuwa linaushabikia ndiyo umedhoofika tena upo taaban! Hii yote imetokea kwa vile Dr. Salim alijua kwamba umaarufu wa mtu unatengenezwa na mtu mwenyewe, na ndiyo maana hata alipochafuliwa hakutaka kulumbana, bali alikaa kimya akisubiri ukweli ujilete wenyewe ambao wote tunauona!

Watanzania inabidi tuwe makini wa kuweza kutambua wenyewe bila ushawishi watu wenye sifa za kuwa viongozi wa umma bila ya msukumo wowote toka kwenye lile genge ambalo siku zote lipo mustari wa mbele kabisa kutuchagulia viongozi kwa kuwajengea umaarufu wa uongo ili mradi mambo yao yaendelee kuwa mazuri na sisi tukiendelea kuwa masikini zaidi! Sasa hivi genge hili hili lipo katika kampeni chafu za kuwajengea baadhi ya wanasiasa umaarufu wa uongo na baadhi yao hata umri wao bado haujawaruhusu kujipenga makamasi peke yao, ni mpaka wapengwe makamasi na hata nguo bado wanavalishwa, lakini mikakati inafanywa ili hata katiba ibadilishwe watu wao waweze kugombea urais! Watoto wadogo wawe marais wa taifa lipi!? Hao watoto wamefanya miujiza gani mkapa hata tuone kwamba wana umuhimu wa kuliongoza taifa hili!? Au kupiga makelele bungeni ndiyo busara kwa uelewa wa Watanzania!? Au kutumiwa na mitandao kwa kupewa siri za serikali na kuzitoa bungeni ndiyo wameshakuwa mashujaa kiasi ambacho hatuwezi kuishi bila wao kutawala!? Kwani nani hawezi kusimama bungeni na kuzungumza kama ameshapewa kitu au hoja ya kuhoji!? Wabunge hawa wanaotumiwa na genge la kuandaa viongozi kiukweli ni wabunge dhaifu sana kuliko hata wale ambao wamekuwa wakitumia fikra zao binafsi bungeni; Marais watoto wakaongoze nchi zilizoendelea kama vile Amerika na UK ambako democrasia imekuwa na rais ni taasisi siyo mtu binafsi kama hapa kwetu Tanzania.

Watanzania tumeshindwa kuwatambua watu wenye busara kwa mtizamo wetu binafsi! Tunadhani kuandikwa sana kwenye kila gazeti ndiyo ubusara wa mtu, unaweza kuandikwa sana lakini ukawa huna lolote zaidi ya umaarufu wa uongo, na ukawa huandikwi sana lakini ukawa na busara zaidi kuliko wale wanaopamba kurasa za mbele za magazeti ya kila siku! Pia unaweza kutumiwa na genge la media si kwa sababu unaweza hapana, bali unatumiwa ili uwaharibie wale wanaofaa, ili wananchi wasiokuwa wadadisi wazuri wa mambo ya siasa washindwe kutofautisha ni yupi anapengwa makamasi au ni nani anajipenga mwenyewe! Siyo kila mtoto akililia gozi lazima umpe, watoto wengine ukiwapa gozi badala ya kulicheza wao hulilambalamba na kulitemea mate! Mtoto mdogo mpe pipi amumunye! Gozi licheze mwenyewe!

Kulingana na hali halisi ya nchi yetu kwa sasa nchi ambayo ina migogoro mingi ya kidini, ardhi, mauaji na vitendo vya uhalifu wa kupangwa (mafia), ufisadi uliokithiri, ubadirifu wa mali ya umma, kuzorota kwa uchumi na maendeleo ya jamii, kuzorota kwa mfumo wa elimu na afya bora nchini; tunahitaji rais mpevu mwenye busara ya hali ya juu asiyefungamana na upande wowote, mwadilifu, mbunifu na mwenye maono ya mbali ili aweze kuliokoa hili taifa ambalo tukilifanyia mizaha ya kushabikia watu wasiokuwa na sifa tutalielekeza gizani!

Ukitumia nguvu zinazoambatana na vitendo vya uhalifu wa kupangwa kwa madhumuni ya kujijengea au kuwajengea umaarufu wale wasiostahili, utakuwa hujijengi wala huwajengei bali unawabomoa! Kama hatuamini haya tusubirini ukweli wa uhalifu wote wa kupangwa utajitokeza mwishoni, na hapo ndipo tutakapoona kwamba je, wale wataalamu wa kupanga na kushabikia uhalifu huo watakuwa wamejijenga au wamejibomoa!?

Dr. Noordin Jella Email: norjella@yahoo.com Mobile: +255 782 000 131

Sunday, April 21, 2013

KIBANDA AMPONZA WASSIRA



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu), Stephen Wassira

Na Josephat Isango,Dar

KAULI ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu), Stephen Wassira kudai kuwa Idara ya Usalama wa Taifa haiwezi kumtesa Kibanda kwa kuwa hana umaarufu kisiasa nchini, imeibua mjadala mkali, Tanzania Daima Jumapili limebaini.


Juzi wakati akihitimisha hoja ya hotuba ya bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2013/ 2014, Wassira aliitetea Idara ya Usalama wa Taifa dhidi ya tuhuma zinazowahusu baadhi ya watendaji wake kuhusika katika matukio kadhaa ya utekeji na utesaji wa raia.

Wassira alisema haiwezekani kwa watumishi wa idara hiyo kujihusisha na matukio hayo na kueleza mafanikio mbalimbali ambayo imeliletea taifa.

Alihoji sababu za kulihusisha tukio la kutekwa na kuteswa kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri nchini (TEF), Absalom Kibanda na idara hiyo na kuhoji; ‘kwani yeye ni nani?’

Katika kuali hiyo ambayo imeibua mjadala, Wassira alisema haiwezekani idara hiyo ikahusika kwa kuwa Kibanda hana umaarufu katika siasa za Tanzania, na kwamba labda wangekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe na Katibu Mkuu wake, Dk. Willibrod Slaa angeelewa.

Kibanda alivamiwa akiingia nyumbani kwake Mbezi Juu jijini Dar es Salaam usiku wa Machi 6 mwaka huu na watu wasiojulikana, na kushambuliwa vibaya kwa kupigwa nondo kichwani, kutobolewa jicho la kushoto, kung’olewa ukucha, meno mawili na kukatwa kidole.

Kauli ya Wassira imepokelewa kwa mtazamo hasi na watu mbalimbali katika jamii, huku wengi wakisema kuwa hiyo ni ishara kwamba chombo hicho kinahusika na vitendo hivyo, lakini kwa kundi fulani la watu.

Akizungumza na Tanzania Daima Jumapili, mwanasheria maarufu nchini, Mabere Marando alisema mjadala huo unatokana na hoja aliyoanzisha yeye ya kuwataja watu wa Usalama wa Taifa kuwa wanahusishwa na utekaji na utesaji.

Marando ambaye pia ni ofisa wa zamani wa idara hiyo, alifafanua kuwa ni vema Wassira ashauri sera za Idara ya Usalama zifanyiwe mabadiliko, waache kulinda heshima ya chama badala yake walinde taifa.

“Kazi za usalama ni kugundua mapema na kutoa taarifa habari zinazohusu serikali kupinduliwa, kusaidia serikali katika ujasusi wa uchumi ili nchi iendelee na mwisho kabisa ni kushauri serikali kuhusu hali ya kisiasa nchini. Wala sio kupambana na wanasiasa au waandishi wa habari,” alisema.

Marando aliongeza kuwa Usalama wa Taifa sasa unafanya kazi za usalama wa raia ambazo ni za polisi kimsingi. Kwamba Usalama wa Taifa huwa hawakamati, lakini siku hizi wanakamata.

“Sasa kama hawa wakifanya hivi polisi watafanya kazi gani? Tunashindwa kutofautisha kazi za usalama wa taifa na usalama wa raia,” alisema.

Katibu wa TEF, Neville Meena alisema kuwa Wassira ni kielelezo cha ulevi wa madaraka. Anaona kuwa wanasiasa ndio watu zaidi kuliko wengine.

Alisema kwa kauli ile pengine ndiyo maana uchunguzi wa suala la Kibanda haufanyiki wala hakuna taarifa rasmi ya polisi iliyotolewa tangu atekwe na kuteswa.

“Tunafurahi kwa kuwa tumepata mawazo ya watawala na kauli ya Waziri huyu wa Nchi, Ofisi ya Rais pengine ndiyo msimamo wa serikali maana alisema bungeni.

“Huyu anatoka Ofisi ya Rais, tena anashughulikia mahusiano. Anapotoa kauli hii zikiwa zimefika siku 45 tangu Kibanda atekwe na kuteswa, mauaji au mateso kama hayo hayataisha katika nchi kwa kuwa sisi wengine sio watu kwa mujibu wa Wassira. Kauli hii ni mbaya na haina afya,” alisema Meena.

Mwandishi nguli wa habari nchini na mshauri wa masuala ya habari, Ndimara Tegambwage alisema; “Kwanza tunafurahi kwa kuwa Wassira amethibitisha kuwa wana usalama wanawaandama watu na mara zingine kuwadhuru viongozi wakubwa hasa wasiofuata au kukubaliana na sera zao.

“Pili, kwa mujibu wa Wassira kwa sasa Watanzania tunajua kuwa baya lolote likimpata Dk. Slaa au Mbowe litakuwa limetekelezwa na watu wa usalama.”

Ndimara aliongeza kuwa kwa kauli ya Wassira kusema kuwa Idara ya Usalama inashughulikia wanasiasa maarufu, ameivua nguo idara hiyo na wangetarajia idara hiyo imwajibishe kwa kutoa siri za Usalama wa Taifa.

“Linapokuja suala la haki za binadamu hakuna mdogo au mkubwa, hakuna rais au mama ntilie. Hakuna aliye mdogo asiyehusiana na mkubwa, ikifikia hatua ya dharau ya aina hii tunashindwa kumwelewa waziri huyu,” alisema.

Mkurugenzi wa mashirika yasiyo ya kiserikali yanayotetea haki za binadamu, Onesmo Olengurumwa alisema Wassira amethibitisha kuwa kumbe Usalama wa Taifa kuna watu wanawateka na kuna wengine hawatekwi.

“Tunashukuru kwa kusema kuwa kuna kundi fulani linawindwa, ni dharau sana kwa kauli ile kwa kuwa Kibanda ni Mtanzania, awe na cheo asiwe na cheo, awe mwanasiasa au sio mwanasiasa serikali inapaswa kumlinda.

“Kauli ya Wassira inaleta matabaka, inaonesha wengine wana thamani zaidi, wengine hawana thamani,” aliema.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Benson Bana alizungumza kwa kifupi akisema; “hiyo kauli haikupimwa, sio kauli iliyotarajiwa kutoka kwa kiongozi wa CCM. Kweli hakutumia busara katika kutamka kauli hii tena bungeni.”

Saturday, April 20, 2013

VIBAKA WAUA ASKARI POLISI KAHAMA



Na Ali Lityawi, Kahama

ASKARI polisi wa kitengo cha usalama barabarani, wilayani Kahama, Salum Mtepa, ameuawa usiku wa kuamkia jana na watu wanaosadikiwa kuwa ni vibaka kutoka machimbo madogo ya dhahabu ya Nyangarata na Mwime, baada ya kumpiga na kitu kizito kifuani.

Tukio hilo lilitokea nyumbani kwake eneo la kata ya Majengo mjini Kahama usiku wa kuamkia jana baada ya watu hao wanaokadiriwa kuwa wanne kwenda nyumbani kwa askari huyo mwenye cheo cha Staff Sajenti na kuvunja kibanda cha biashara kwa lengo la kuiba ndipo askari huyo alipotoka nje kwenda kupambana nao.

Inadaiwa kuwa baada ya kutoka nje vibaka hao waliokuwa na pikipiki, watatu kati yao walikimbia akabaki mmoja aliyekuwa na kifaa ambacho hutumiwa na wachimbaji wa dhahabu katika machimbo madogo madogo kwa ajili ya kuvunjia miamba ya mawe ambacho hujulikana kwa jina la Moko.

Kwa mujibu wa taarifa ya mkuu wa polisi wilaya ya Kahama, George Simba, askari huyo alipigwa na kifaa hicho kifuani wakati akijaribu kupambana na kibaka huyo, hali iliyosababisha avuje damu nyingi ndani ya kifua na kusababisha kifo chake.

Simba alisema hali ya vibaka katika mji wa Kahama ni mbaya kwani wameongezeka kutokana na machimbo ya Nyangarata kujaa maji na Mwime kuisha uzalishaji wake, hali iliyofanya vijana wengi kutoka kwenye maeneo hayo kutokuwa na fedha.

Alisema hivi sasa wimbi la vibaka hao limekuwa tishio huku akiahidi kupambana nao pia kuwasaka kwa nguvu zote waliohusika na kifo cha askari huyo wa usalama barabarani, ingawa hadi jana hakuna mtu yeyote aliyekuwa amekamatwa kuhusiana na tukio hilo.

Friday, April 19, 2013

ZAO LA UFUTA KUBADILI MAISHA YA WAKULIMA MKOA WA PWANI






Miongoni mwa wakulima wa ZAO la ufuta waliopo  mkoani Ruvuma wakiwa kwenye Picha ya Pamoja

 Na Stephano Mango

UFUTA ni zao lisilotiliwa maanani na wakulima wengi nchini kwa miaka mingi pamoja na uwingi wa faida zake kwa binadamu, lakini kwa miaka ya hivi karibuni, takribani sehamu zote ambako hali ya hewa imekuwa rafiki wa kulistawisha zao hilo, wakulima wameligeukia na kuanza kulima kwa kasi.

Zao la ufuta linatabiriwa kuwa zao kuu mbadala la kibiashara mkoani Pwani kutokana na mahitaji ya soko kuwa makubwa kwa sasa likifuatiwa na Muhogo pamoja na Embe.

Wilaya ya Rufiji ni mojawapo ya wilaya ambazo zinastawisha zao la ufuta kwa siku nyingi na siku za hivi karibuni kasi ya uzalishaji imeongezeka kutokana na upatikanaji wa uhakika wa soko la ufuta.

Katika msimu wa mwaka 2010 mpaka 2011, kwa mujibu wa Mkuu wa Wilaya hiyo Nurdin Babu. zao la ufuta liliiingizia mapato halimashauri ya wilaya ya Rufiji kiasi cha shilingi milioni sitini (60,000,000/=), hivyo kuongoza katika kuiingizia halimashauri mapato kupitia vyanzo vyake vya mapato

Hata hivyo, Mkuu wa wilaya hiyo alisema kuwa ni lazima kujiwekea malengo ya kuzalisha walau kwa kuanzia tani elfu tano (5000) katika msimu ujao wa kilimo 2012/2013 kutoka tani za sasa 400 kwa mwaka na tani 280 mwaka 2005/06.



Utafiti uliofanywa na jarida la “MUVI – Nuru ya Mafanikio” umebaini kuwa tofauti na mazao mengine ya kibiashara yanayolimwa mkoa wa Pwani kama vile Embe, Nanasi na Muhogo ni kuwa zao la ufuta hususani wilayani Rufiji wanunuzi hununua likiwa bado shambani na kulipa pesa pale linapoanza kuvunwa na mteja ndiye anayepanga bei na sio mnunuzi.

Hali ya soko kwa zao la ufuta ni kuwa bei ya kilo moja ya ufuta imepanda toka Tshs500/= mwaka 2000 hadi Tshs 1500/= mwaka huu 2012 kwa kilo, na hivyo kuchochea uzalishaji wa zao la ufuta kwa wakulima, anaeleza mkufunzi wa mafunzo na Afisa Mazao wa Wilaya ya Rufiji Ndugu Bahinga.

Kwa mujibu wa tafiti iliyofanywa na Dkt.Elly Kafriti, kutoka katika kituo cha utafiti Naliendele mkoani Mtwara katika mazao ya mbegu za mafuta,zao la ufuta linaongoza kwa kulipatia taifa fedha nyingi za kigeni.Mwaka 2005 taifa lilipata zaidi ya shilingi bilioni 20 kutokana na mauzo ya tani 32,000 za ufuta nje ya nchi.

Nchini Tanzania zaidi ya asilimia 75% ya ufuta hulimwa katika mikoa ya kusini ya Mtwara, Lindi na Ruvuma na katika mikoa hiyo ufuta ni zao la Pili la biashara baada ya Korosho. Mikoa mingine ni Tanga,Pwani na Morogoro.

Katika wilaya ya Rufiji Ufuta hulimwa ukanda wa juu yaani tarafa za kibiti,Kikale,Mohoro na Ukanda wa tambalale tarafa za Mkongo na Ikwiriri.

Inafahamika wazi kuwa mradi wa MUVI ni wa miaka saba (7) uliibuliwa na Serikali kupitia wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko ambao unatekelezwa kwa mkopo wa Serikali toka Shirika la IFAD ambapo SIDO inatekeleza mradi huu kwa niaba ya Serikali ya Tanzania.

Madhumuni ya mradi ni kumwezesha mjasiriamali mdogo wa kijijini awe mkulima, mfanyabiashara, msindikaji vyakula n.k ili aweze kujiongezea kipato katika shughuli zake na kupunguza umasikini. Hivyo basi mradi wa MUVI unalenga kutoa ajira kwa vijana toka familia masikini vijijini.

Ili kufanikisha hilo Afrikan Image imepewa jukumu la kusimamia utoaji huduma ya mawasiliano ya kibiashara vijijini kwa wajasiriamali wadogowadogo katika mikoa sita na Pwani ikiwemo.

Njia mbalimbali zimekuwa zikitumika kama kutengeneza na kurusha vipindi mbalimbali vya radio, kutengeneza machapisho mbalimbali, mbao za matangazo vijijini, taarifa za bei za mazao kwa njia ya simu na mtandao wa MUVI kwa lugha ya Kiswahili ili kuwezesha mawasiliano ya kibiashara kufanikiwa vijijini.

Hadi robo ya pili ya mwaka wa tatu wa uhai wa mradi, jumla ya vikundi 90 vya wajasiriamali vimefikiwa, wanaume wakiwa 803 na wanawake 775, machapisho mbalimbali yanayofikia zaidi ya 50 elfu yakiwemo ya maembe, mananasi, jarida la muvi, kalenda, alizeti, muhogo na mwongozo wa namna ya kutumia ubao wa matangazo kwa wajasiriamali vijijini,

Kwa kipindi cha miaka miwili ya uhai wa mradi katika wilaya tatu za mkoa wa Pwani, Mkuranga, Bagamoyo na Rufiji yamesambazwa vijijini na kutoa mchango mkubwa katika kubadili mazoea ya wakulima na hivyo kuongeza tija katika kilimo.

Afrikan Image wanatarajia kuzindua huduma ya mawasiliano kwa njia ya ujumbe mfupi ili kupata taarifa za masoko kwa mazao mbalimbali pamoja na kuanza kurusha vipindi vya radio ifikapo katika ya mwezi machi mwaka huu.

Ili kuweza kuongeza chachu ya ustawishaji wa zao hilo Serikali kupitia wizara ya viwanda, biashara na masoko, chini ya mradi wa MUVI mkoa wa Pwani, hivi karibuni waliendesha mafunzo kwa maafisa ugani ishirini (20) kutoka Kata mbali mbali za Wilaya ya Rufiji ambapo wamepatiwa mafunzo maalum ya kilimo bora cha zao la ufuta.

Mafunzo kwa maafisa ugani wa Kata na Vijiji ni muhimu katika kuleta ufanisi katika utekelzaji wa shughuli za kitaaluma kwa walengwa. Mradi umebaini ya kwamba kutoa mafunzo ya namna hii kutasaidia kueneza taaaluma ya kilimo bora kwa wakulima wadogo wadogo kwa urahisi kwa sababu maafisa ugani wanaishi pamoja na walengwa kila siku.


Ni rahisi kufikisha ujumbe kuliko kungoja taarifa za taaluma kuletwa na maafisa mradi walioko mbali na wakulima hao. Kwa kuzingatia fursa iliyopo sasa ya zao hilo, Elimu waliyoipata wataipeleka moja kwa moja kwa walengwa, ambao ni wakulima wadogowadogo walioko kwenye kata na vijiji husika.

Mafunzo hayo yamelenga kumuwezesha mkulima kupata taaluma na uelewa mzuri zaidi katika kilimo cha zao hili tofauti na wanavvoelewa sasa ili kuboresha uzalishaji kwa lengo la kuongeza mazao yaliyo bora yatakayowezesha kupata bei nzuri kwenye soko.

Nurdini Babu ni mkuu wa wilaya ya Rufiji na hapa anasisitiza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo yaliyofanyika katika mji mdogo wa Ikwiriri wilayani Rufiji, “Hili ni zao lenye faida kubwa kama utekelezaji wa taaluma ya uzalishaji utafuatwa kwa makini, ambalo ndiyo lengo kuu la mafunzo haya”, anasisitiza Babu.

Katika ziara ya kutathmini shughuli za mradi iliyofanywa na wafadhili wa mradi,yaani IFAD, ilipendekezwa kwamba zao lenye mzunguko mfupi linaloweza kuleta mafanikio ya kuongeza kipato kwa mkulima liongezwe kwenye mchakato wa uendelezaji wa mnyororo wa thamani sambamba na mazao ya muhogo na matunda yaliyopo sasa.

Ufuta ulichaguliwa katika ushindani na mazao mengine kama, mahindi, mpunga na mtama mweupe. Mafunzo yanatolewa ili kilimo cha ufuta kianze mara moja katika msimu huu.

Zao la ufuta sio zao geni machoni mwa wakulima waliowengi mkoani Pwani, kwa vile uzalishaji wake hautakuwa mgumu hasa ikizingatiwa kwamba soko la kueleweka lipo na pia ni endelevu.

Pendekezo la kujumuisha zao hili pamoja na mazao ya muhogo na matunda unatokana na faida yake kuwa kubwa katika kuongeza kipato kwa mkulima kwa muda mfupi tofauti na mazao ya muhogo na matunda.

Mjadala mkali wa jinsi zao la ufuta linavyoweza kuendelezwa na kumkomboa mkulima sambamba na fursa za soko zinazolizunguka zao hilo ulitawala kwa muda wa siku tano za mafunzo maalumu kuhusu kilimo bora cha ufuta, uliowashirikisha maafisa ugani zaidi ya ishirini na wadau mbalimbali wa zao la ufuta wilayani Rufiji.

Katika mafunzo hayo ya maafisa ugani, wamejifunza kanuni za kilimo bora cha zao la ufuta, kuanzia uchaguzi wa mbegu bora, utayarishaji wa shamba, udhiti wa mgonjwa na wadudu, utunzaji wa shamba na uhifadhi wa mazao baada ya kuvuna pia na usafirishaji.

Nchini Tanzania zaidi ya asilimia 75% ya ufuta hulimwa katika mikoa ya kusini ya Mtwara, Lindi na Ruvuma na katika mikoa hiyo ufuta ni zao la Pili la biashara baada ya Korosho.

Mikoa mingine ni Tanga,Pwani na Morogoro. Katika wilaya ya Rufiji Ufuta hulimwa ukanda wa juu yaani tarafa za kibiti,Kikale,Mohoro na Ukanda wa tambalale tarafa za Mkongo na Ikwiriri.







Thursday, April 18, 2013

DC TUNDURU AMWAGIZA MKURUGENZI KUWACHUKULIA HATUA WATUMISHI WAZEMBE



Na Steven Augustino, Tunduru

MKUU wa Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma Chande Nalicho amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halamashauri ya Wilaya hiyo kuwachukulia hatua ikibidi hata kuwafukuza kazi Watumishi wasio wajibika zikiwa ni juhudi za Serikali kuinua taaluma Wilayani humo.

Nalicho alisema hayo wakati akifungua Mkutano wa kutathmini matokeo kidato cha pili,Nne na Sita uliofanyika katika ukumbi wa klasta Mjini hapa na kuongeza kuwa hali hiyo imetokana na Serikali kubaini kuwa watumishi wa kada zote Wilayani humo hawako tayari kufanya kazi kwa kujituma hali iliyopelekea Wilaya hiyo kuwa nyuma kielimu.

“Viongozi ndio wasiopenda kufanya kazi, wamebakia kulalamikia mishahara tu na ndiyo maana katika Wilaya hiyo imeendelea kuwa nyuma kielimu” alisema Nalicho na kumtaka Mkurugenzi awachukulie hatua za kinidhamu.

Alisema inashangaza kuona kuwa Wilaya ikiwa imekithiri kwa utoro wa wanafunzi lakini inapotokea ofisi yake inahitaji taarifa za matukio hayo hata Maafisa tarafa ,watendaji wa kata na viongozi wa vijiji wengi wanapoulizwa juu ya idadi ya wanafunzi waliofauru na kucahaguliwa kujiunga na masomo ya sekondari wanadai kutokuwa na takwimu zake.

Nalicho aliendelea kubainisha viashiria vingine vya viongozi hao kutowajibika kuwa ni pamoja na kuwepo kwa takwimu kubwa za utoro uliokithiri ambazo hazifanyiwi kazi ambapo alitolea mfano Shule ya msingi Njenga ambayo takwimu zinaonyesha kuwa mwaka 2010 ilifaulisha wanafunzi 41 waliokwenda shule walikuwa 3, mwaka 2011 waliofauru 46 walioendelea na masomo 7 na mwaka 2012 walifaulu 17 waliokwenda shule hadi sasa 1.

Nae Mwenyekiti wa Huduma za jamii na uchumi Diwani Athumani Nkinde pamoja na kukiri kuwa zipo Shule za Sekondari ambazo zilijengwa kisiasa na kutolea mfano shule za Sekondari Nampungu ambayo inaonesha kutelekezwa na wananchi kwa kutopeleka wanafunzi

Nkinde alipigilia msumali wa moto kwa kuzitaka mamlaka kuchukua hatua za kisheria kwa wanafunzi na wazazi wao kwavile kusoma ni lazima

Akizungumzia mikakati ya kuinua taaluma na kuiondoa idara yake katika kashfa ya kupeleka Sekondari wanafunzi wasiojua kuandika kusoma na kuhesabu Kaimu afisa elimu wa Shule za Msingi Mwl. Fraviani Nchimbi alisema kuwa Wilaya inaendelea kujidhatiti kwa kutumia mitihani ya majaribio katika kata pamoja na kuendesha mafunzo ya mada ngumu kwa walimu zikiwa ni juhudi za kuinua taaluma kwa wanafunzi.

Awali akisoma taarifa ya matokeo ya ufaulu wa wanafunzi katika kipindi cha mwaka 2011 na 2012 Afisa elimu Sekondari Mwl. Ally Mtamila alisema kuwa mbali na Wilaya hiyo kufanya vibaya lakini idadi ya walimu imeongezeka kutoka walimu 213 mwaka 2011 na kufikia 282 mwaka huu ongezeko ambalo pia limeongeza idadi ya walimu na kufikia wastani wa zaidi ya walimu 10 kwa kila shule ya sekondari Wilayani hapa.

Mwisho



Wednesday, April 17, 2013

MADIWANI WA CCM WAHOJIWA KWA KOSA LA KUSHIRIKI KUTAKA KUMNG'OA MEYA SONGEA

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Charles Mhagama

Charles Mhagama ambaye ni Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea akiwa na Diwani wa Kata ya Matarawe James Makene ambaye ndiye MHASISI wa kumtuhumu Meya

Na Stephano Mango, Songea


MADIWANI Sita wa Chama Cha Mapinduzi wakiwemo Madiwani wawili ambao waliungana na Madiwani nane wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo( Chadema) kuandika barua kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea ya kumuomba kuitisha mkutano maalumu wa Madiwani wenye madhumuni ya kujadili hoja za kutokuwa na imani na Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo Charles Mhagama ambaye anadaiwa kutumia nafasi yake vibaya wamehojiwa kwa nyakati tofauti na Kamati ya Siasa Ccm ya Wilaya ya Songea Mjini ikiwataka kujua muanganiko wao na Chadema katika sakata la kutokuwa na imani na Meya wao.

Uchunguzi uliofanywa na mtandao kwa zaidi ya wiki mbili sasa umebaini kuwa lengo kubwa la kamati hiyo ya siasa ni kutaka kufunika hoja ya msingi ya Madiwani kumi wa Halmashauri hiyo ya kutaka kuitisha mkutano ambao una lengo la kuelezea tuhuma zinazomkabili Charles Mhagama ambaye ni Mstahiki Meya wa Halmashauri hiyo bila kujali itikadi zao za kisiasa kwa masloahi ya wakazi wa Manispaa ya Songea

Imebainika kuwa Kamati hiyo ya Siasa iliyokutana tarehe 11/4/2012 iliwahoji, kuwatisha na kuwaonya Madiwani hao kuacha kuungana na Chadema kumtisha tisha Meya wao kwani kufanya hivyo kunaendelea kuwapa umaarufu Chadema ambao hawakitakii mema Chama cha Mapinduzi na badala yake kujikita kulinda heshima ya Ccm

Taarifa za ndani ya kikao hicho zimeeleza kuwa ndani ya kikao hicho kuliibuka malumbano makali yenye kupinga wazo la Chama kumbeba Meya ambaye anaonekana waziwazi kuwa hakubaliki ndani ya Baraza la Madiwani na nje ya baraza la hilo kutokana na mwenendo wake mbovu licha ya uchaguzi wake kutokuchaguliwa na Madiwani hao kwani alipigiwa kura 12 za ndiyo na kura 14 za hapana

Mtandao umebahatika kuiona barua ya Madiwani kumi wa Halmashauri hiyo yenye kumbukumbu namba MD/SO/013 ya Tarehe 15/3/2013 yenye hoja mbili ambazo zina vipengele vitano vinavyosisitiza kumuomba Mkurugenzi kuitisha mkutano maalumu wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa hiyo ,

Imebaini kuwa barua hiyo ndiyo ambayo imeichanganya kamati hiyo ya Siasa na kuamua kuitisha kikao cha dharula cha kuwatisha Madiwani hao kuacha mara moja mkakati huo na Chadema kwa maslahi ya Ccm kwani kufanya hivyo ni kukiaibisha chama na kukidhorotesha mbele ya umma

Madiwani hao ambao wamehojiwa na Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Songea Mjini ni James Makene Diwani wa Kata ya Matarawe, Victa Ngongi Diwani wa Kata ya Ruvuma, Faustini Mhagama Diwani wa Kata ya Mshangano, Kulabest Mgwasa Diwani wa Kata ya Msamala, Wilon Kapinga Diwani wa Kata ya Ndilimalitembo na Genfrida Haule Diwani wa Viti Maalum

Imebainika kuwa Madiwani wawili wa Chama cha Mapinduzi (Ccm)walioungana na Madiwani nane wa Chadema kuandika barua hiyo ni Diwani wa Kata ya Matarawe James Makene na Victa Ngongi ambaye ni Diwani wa Kata ya Ruvuma

Taarifa zilizoufikia mtandao huu zimesema kuwa Kanuni za Kudumu za Halmashauri hiyo za mwaka 2003 ibara namba 4 na ibara namba 80 zinaeleza ili kuitisha mkutano maalum wa baraza la Madiwani kujadili hoja mbalimbali za kutokuwa na imani na Meya kujiorodhesha na kufikia idani ya theluthi moja ya Madiwani na kueleza malengo ya mkutano huo

Katika Halmashauri hiyo kuna jumla ya Madiwani 28 ambao theluthi yao ni Madiwani 9 ambapo madiwani 10 ndio waliojiorodhesha na kuweka saini zao za kusudio hilo ambalo linaonekana kuwa ni mwiba mkali kwa Ccm

Mmoja wa Madiwani wa Ccm ambao wamehojiwa na Viongozi wa Chama hicho ambaye hakutaka jina lake litajwe ameuambia mtandandau huu kuwa toka awali Charles Mhagama hakuchaguliwa na Madiwani wa Halmashauri hiyo ndio kiini cha kuwepo kwa makundi mawili ambayo moja linamuunga mkono na na kundi jingine ambalo halikubaliani na kundi linguine licha ya utendaji kudaiwa kuwa ni mbovu

Diwani huyo alilesema kuwa Chama hakina uwezo wa kuwachagulia Madiwani Meya Mbovu na kuendelea kuweka mazingira ya kumlinda licha ya kuwa tuhuma zake kuwa wazi na kuwatesa wananchi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

Alifafanua kuwa jukumu la kumchagua Meya ni la Madiwani bila kujali itikadi ya chama chochote kwani Meya huyo ni kiongozi wa Madiwani kwa maslahi ya wakazi wa Manispaa ya Songea ambao ndio waliowachagua madiwani wawawakil;ishe kwenye malengo ambayo yana maslahi kwa jamii

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Ccm Wilaya ya Songea Mjini Gerod Mhenga alipohojiwa kwa njia ya simu jana alithibitisha kuwepo kwa kikao hicho cha Kamati ya Siasa ya Wilaya yenye lengo la kubaini tatizo lililopo kati ya Madiwani na Meya wao hadi kufikia hatua ya kuungana na Madiwani wa Chadema ya kumtaka Mkurugenzi kuitisha mkutano maalum wa kujadili mwenendo wa Meya

Akizungumza na mtandao huu Mstahiki Meya wa Halmashauri hiyo Charles Mhagama alikanusha baadhi ya tuhuma wanazo mtuhumu na kusema kuwa kama Madiwani wana jambo lao basi wanatakiwa kufuata kanuni ili ziwaruhusu kulisema jambo lao

Hata hivyo Mkurugenzi wa Manispaaa hiyo Nachoa Zakaria alipohojiwa jana ofisini kwake alisema kuwa Halmashauri inaweza kumuondoa madarakani Meya ni lazima kuwe na theluthi mbili ya madiwani wanaotaka kumuondoa na sio theluthi moja kama walivyoomba Madiwani hao kumi hivyo hawezi kuitisha kikao hicho bila kukidhi matakwa ya kanuni.

MWISHO