About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, September 15, 2011

MAJAMBAZI WAPORA MILIONI 5 NA KUJERUHI WAFANYABIASHARA WATATU NA KISHA KUTOKOMEA KUSIKOJULIKANA

                                   Na Gideon Mwakanosya, Songea
 
MFANYABIASHA mmoja Habiba Kazembe (45) mkazi wa Mtaa wa Muungano uliopo Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma amevamiwa na kundi la watu wanaosaidikiwa kuwa ni majambazi na kuporwa fedha taslimu shilingi milioni 5 akiwa amelala chumbani kwenye nyumba ya kulala wageni ya Mataya iliyopo katika kijiji cha Lusewa Wilayani Namtumbo na wafanya biashara wengine watatu wamejeruhiwa vibaya kwa kupigwa risasi na majambazi hayo ambayo yalitoroka na kutokomea kusiko julikana.
 
Walio jeruhiwa kwa kupigwa na risasi wametajwa kuwa ni Edga Kayombo mfanya biashara Mkazi wa Eneo la Lizaboni Manispaa ya Songea, Michael Komba mfanya biashara ambaye ni Mkazi wa Mahenge Songea Mjini na Muhudumu wa nyumba ya kulala wageni wa nyumba ya Mataya Mariamu Azizi .
 
Habari zilizopatikana mjini hapa ambazo zimethibitishwa na Majeruhi zimeeleza kuwa tukio hilo  limetokea  September 15 majira ya saa za usiku huko katika Kijiji cha Lusewa kilichopo Wilayani Namtumbo ambako inadaiwa majambazi ambao idadi yao haikuweza kufahamika mara moja wakiwa na silaha aina ya SAR na SMG walivamia nyumba ya kulala wageni  kisha waliwajeruhi watu watatu kwa kuwapiga na risasi watu watatu sehemu mbalimbali za miili yao na kumpora mfanyabiashara mmoja shilingi milioni tano nakutokomea nazo.
 
Mmoja wa majeruhi Edga Kayombo ameuambia mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com/  jana mchana kuwa yeye amejeruhiwa kwa  kupigwa risasi mkono wa  kushoto  akiwa amelala kwenye gari ambalo lilikuwa nje ya nyumba ya kulala wageni baada yakukosa vyumba .
 
Amefafanua  kuwa  kundi hilo la watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi walivamia nyumba hiyo ya kulala wageni saa 9 usiku yeye akiwa kwenye gari ghafla alisikia  mlio  wa  risasi  zikipigwa ndani  ya nyumba  ya kulala  wageni .
 
Amesema  kuwa  baada ya  kusikia  milio  ya risasi  aliondoka  na  kwenda ndani ya nyumba ya kulala wageni ambako walikuwa wamelala  wafanyabiashara  wenzake   lakini akiwa anatoka  kwenye  gari  hilo  alikutana na watu watatu  wakitokea kwenye nyumba hiyo ya kulala wageni wakiwa na siraha wameshika  mikononi ambapo mmoja kati yao alimpiga risasi kwenye mkono wa kushoto.
 
Ameeleza zaidi  kuwa  majambazi hao baadaye waliondoka na kutokomea kusikojulikana na  yeye alianza kupiga kelele kwa ishara ya kuomba msaada ambapo majirani walifika kwenye eneo la tukio kisha waliwachukua majeruhi hadi kituo cha polisi cha lusewa ambako walipatiwa hati ya matibabu ambako walikimbizwa kwenda hospitali ya serikali ya Mkoa kwa matibabu zaidi.
 
Mganga Mfawidhi wa hospitali ya Mkoa Songea Dkt Benedict Ngaiza ameiambia nipashe kuwa majeruhi hao walipokelewa majira ya saa 5 na nusu asubuhi ambapo alibainisha kuwa Kayombo amepigwa risasi kwenye kiganja cha mkono wa kushoto, Komba amepigwa risasi kwenye makalio na Mariam Azizi amepigwa risasi sehemu za siri chini ya kinena na kwamba mpaka sasa risasi moja bado ipo kwenye paja lake wanafanya jitihada ya kuondoa risasi hiyo mwilini.
 
Kwa upande wake Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP)  George Chiposi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambalo amedai kuwa limetokea majira ya saa 9 usiku huko katika Kijiji cha Lusewa Wilayani Namtumbo kwenye nyumba ya kulala wageni ya Mataya ambako kundi la Majambazi wakiwa na siraha zinazosadikiwa kuwa ni SAR  na SMG waliingia kwenye nyumba ya kulala wageni ya mataya na kupiga risasi na baadaye walifanikiwa kuvamia chumba cha mfanyabiashara mmoja habiba kayombo ambaye alidaiwa kuwa alitokea Tunduru kuja kufanya biashara kwenye mnada na walimpora fedha tasilimu shilingi milioni tano na baadaye walimjeruhi kwa kumpiga makofi na wapangaji wengine walijeruhiwa kwa kupigwa risasi.
 
Chiposi amesema kuwa watuhumiwa hao baada ya kupora fedha za mfanyabiashara huyo walikimbia na kutokomea kusiko julikana na polisi inaendelea kuwasaka majambazi hao ambao mpaka sasa bado hawajafahamika.
 
MWISHO

WANAHARAKATI WAKUTANA NA KUJADILIANA KUHUSU HAKI ZA BINADAMU NA USAWA WA KIJINSIA KATIKA KUMILIKI RASILIMALI ZA NCHI ZA UKANDA WA AFRIKA

Akifungua tamasha hilo la 10 la jinsia Profesa Dzodzi Tsikata wa chuo kikuu cha Ghana alisema kuwa tatizo la ukosefu wa ajira katika soko la Dunia na hasa kwa vijana waliohitimu chuo kikuu ni miongoni mwa sababu ziliopelekea kuibuka kwa migogoro mingi katika nchi za Afrika,ingawa kimsingi vurugu hizo pia zinachangiwa kwa kiasi kikubwa na mapungufu ya Demokrasia na utawala bora miongoni mwa nchi za kiarabu.
 
Profesa Tsikata alisema katika siku za hivi karibuni kumeibuka kile kinachoitwa wimbi la migogoro kwa nchi za Kiarabu ambalo kwa kiasi kikubwa limechangiwa na hali duni ya maisha ya watu kutokana na ukosefu wa ajira kwa vijana na wahitimu wa vyuo, japo kimsingi limechangiwa kwa kiasi kikubwa na mapungufu ya kidemokrasia na utawala bora miongoni mwa nchi za Kiarabu.
 
Alisema kwa upande wa Afrika, takwimu za ukosefu wa ajira kwa nchi nyingi ukiondoa Afrika Kusini, kuongezeka kwa ajira katika sekta isiyo rasmi, imetoa kisingizio cha kushindwa kwa serikali za nchi hizo katika utekelezaji wa programu za mabadiliko ya kisera na kiuchumi, na zaidi kushindwa huko kunadhihirishwa na machafuko ya kisiasa yaliyotokea wakati wa chaguzi za Kenya, Nigeria, Ivory Coast na Guinea, na misukosuko ya kiuchumi katika nchi za Swaziland na Malawi hivi karibuni.
 
‘ Kutokana na hali hii Tamasha hili ni fursa muhimu ya kutafakari na kujadili kwa pamoja hali ya maisha endelevu katika Afrika, na mapambano ya harakati za usawa wa kijinsia na pia kutafuta mbinu mbadala zitakazohamasisha upatikanaji wa maisha endelevu na bora na kutoa fursa sawa za maendeleo kwa walio wengi....badala ya mtindo wa sasa wa wachache kupata...’’ alisema Profesa Tsikata.
 
Alisema kwamba umuhimu wa haki za ardhi, ajira na maisha endelevu kwa wanawake na wanaume katika nchi za Afrika zilizoko Kusini mwa Sahara unatokana na ukweli kwamba shughuli nyingi za maendeleo zinategemea kilimo ambacho si cha kisasa kutokana na kutumia zana duni na hivyo kufanya uhitaji mkubwa wa ajira.
 
‘Kadhalika utagundua kwamba zaidi ya kilimo, ardhi ina wigo mpana wa matumizi kwa ajili ya shughuli za maisha endelevu,nyumba za kuishi na kupangisha, kama mojawapo ya chanzo cha ajira, teknolojia na pembejeo, dawa zitokanazo na mimea, upatikanaji wa mafuta, ukuzaji wa rasilimali kwa njia asilia kama vile matunda ambayo huvunwa kwa ajili ya biashara...’’ anasema Profesa Tsikata na kuongeza kuwa.
 
‘Kwa sababu mada kuu katika tamasaha hili ni Jinsia,Demokrasia na Maendeleo,Ardhi,nguvu kazi,na maisha Endelevu,ni vyema tukatambua kwamba Ardhi imekuwa ikitumika pia kama mtaji wa nguvu ya kisiasa na hivyo kuwa kiini cha kutokuwepo kwa usawa wa kijinsia katika umiliki wa rasilimali....na pia umuhimu wa mifumo ya uzalishaji mali katika Afrika na maisha endelevu sambamba na mahusiano yaliyopo katika jamii za Kiafrika kwani kuna uhusiano wa karibu kati ya kushindwa kwa mafanikio ya mapinduzi ya kilimo na umuhimu uliopo wa ardhi kwa maisha bora.....’’.
 
Kuhusu mapambano ya masuala ya umiliki wa Ardhi,Ajira yenye staha na maisha bora na endelevu yenye kuzingatia usawa na haki kijinsia Profesa Tsikata alisema harakati za upatikanaji wa maisha bora na endelevu katika Afrika zinafanyika katika ngazi za kaya, jamii, mahali pa kazi, katika ngazi ya ndani na nje ya nchi na katika ngazi ya kidunia kwa ujumla.
 
Aliongeza kuwa Mapambano hayo yanajumuisha jinsi ya kujikimu kimaisha, shughuli za kila siku za uzazi na uzalishaji mali, na yanachagizwa na tafiti, uchambuzi, harakati mbalimbali na uhamsishaji sambamba na ushawishi na utetezi wa sera aghalabu unaofanywa na asasi za kijamii
 
Alisema Mapambano ya Ukombozi wa wanawake wa Kiafrika kuhusiana na haki ya kiuchumi kwa kiasi kikubwa msingi wake ni madai ya ardhi, ajira yenye staha na maisha bora na endelevu kutoka kwa wananchi wenyewe.
 
Wakati ambapo mapambano haya, hasa katika uanaharakati, hayajapata msukumo wa kutosha kwenye mapambano yanayoendelea katika ngazi ya mashirika. Masuala nyeti katika ufeminist na mchango wa utalaamu vimekuwa na mchango mkubwa katika mapambano haya.
 
Awali akiwakaribisha washiriki katika Tamasha hilo Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Jinsia Tanzania(TGNP) Ussu Mallya alisema kuwa

Alisema kuwa katika maeneo ya vijijini kumekuwepo
na uporaji mkubwa wa ardhi kwa wanawake lakini cha kushangaza viongozi
wamekuwa hawana msaada wowote wa kuwasaidia na hata wanawake wenyewe
wamekuwa na nidhamu ya uwoga katika kuyazungumzia matatizo yao waziwazi mbele ya
viongozi badala yake wamekuwa wakibaki kuwa wanyonge

"Kilichopo hapa kwa sisi wanaharakati sasa tuliopo mijini inatubidi
tufike vijijini ambako ndiko wanawake wengi wapo na hawana msaada
wowote na hawaelewi nini kinachoendelea mbele yao, mwanamke anafikia
hatua anadai haki yake ya kimsingi lakini watendaji wa vijiji
wamekuwa msumari kwao kwa kuwandamiza hivyo sisi kama wanaharakati
tujifunge mkanda kufika vijijini kuwasaidia wanawake wenzetu"alisema.
 
Alisema kuwa wanawake wa vijijini wanapaswa kusaidiwa kwani walio
wengi hawaelewi hata hii katiba mpya wapo ili mradi na hata
ikiwezekana matamasha haya yanayofanyika miaka inayokuja ifike
wakati angalau yahamie ngazi za wilaya au kata ili wanawake waelewe
nini kinazungumziwa
 
Ni wazi kuwaTamasha hilo la mwaka 2011 ni fursa nyingine kwa wanaharakati kujadili na kubadilishana uzoefu kwa lengo la kuondoa unyanyasaji wa kijinsia na haki za binadamu nchini ili kuweza kuleta ustawi stahiki kwa wananchi wa tanzania na hasa zaidi katika harakati ya mapambano kwenye ngazi ya jamii na hasa wanawake walioko pembezoni,kuhakikisha kuwa wanapata haki na fursa sawa katika kufikia na kumiliki rasilimali katika ngazi zote hususani katika muktadha huu wa mtikisiko wa uchumi na fedha
 
Mwandishi anapatika
Simu 0755 335051
Baruapepe;stephano12mango@yahoo.com
 
wanawake katika nchi za afrika wanatakiwa kuacha uwoga na kuwa tayari kuwaeleza
ukweli viongozi wao juu ya matatizo ambayo yamekuwa hayapewi
kipaumbele na kutozungumziwa na kufanyiwa maamuzi stahiki na mamlaka husika

"Wanawake kwa kiasi kikubwa bado tumekuwa na woga na ule unafiki wa
kuwaogopa viongozi wetu pale tunapokuwa na matatizo tunashindwa
kueleza hali halisi ya matatizo yaliyopo kwa kuona kiongozi si mtu wa
kumwambia unaona kama mungu mtu wakati ni mtu wa kawaida
tu"alisema Mallya

TAMASHA LA JINSIA 2011 NI FURSA NYINGINE KWA WANAHARAKATI WA MASUALA YA JINSIA
 
Na Stephano Mango
WANAHARAKATI mbalimbali wa masuala ya jinsia na haki za binadamu nchini wameungana na wanaharakati wenzao wa kutoka nchi jilani zilizopo kwenye ukanda wa afrika katika Tamasha la 10 la Jinsia lenye mada kuu ya Jinsia,Demokrasia na Maendeleo ili kujadili kwa kina masuala ya ardhi,nguvu kazi na maisha endelevu chini ya muktadha wa mfumo dume na uchumi wa soko huria,ubeberu na uliberali mambo leo
 
Tamasha hilo ni muhimu hasa katika kipindi hiki cha miaka 50 ya uhuru ambapo kumekua na tishio la ongezeko la uporaji wa ardhi unaofanywa na wawekezaji wakubwa na kuwepo kwa vuguvugu la madai ya katiba mpya toka kwa wananchi
 
Ni Tamasha la aina yake lililofanyika kwenye viwanja vya mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP) jijini Dar es Salaam kuanzia Septemba 13-16 mwaka huu 2011 kwa kuzinduliwa na mada maalum iliyotolea na Mwanaharakati wa masuala ya ardhi kutoka Ghana profesa Dzodzi Tsilsata
 
Tamasha hilo la aina yake liliratibiwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania(TGNP) kwa kushirikiana na mashirika wanachama wa Muungano wa Wanaharakati wanaotetea ukombozi wa wanawake kimapinduzi,usawa wa jinsia,demokrasia,maendeleo na haki za binadamu(FemAct)
 
Tamasha hilo lilikuwa na mada kuu ya "Jinsia,Demokrasia na Maendeleo:Ardhi,Nguvu kazi na Maisha Endelevu" na pia mada ndogondogo zilizowasilishwa na watu waliobobea ikiwemo mada ya Mapambano ya Wanawake Kwenye Ajira,Maisha Endelevu na Nguvukazi,Mapambano ya Wanaharakati Wanawake kwenye Njia za kujiajili/Kupata Ajira na Maisha Endelevu:Ardhi,Maji,Nafasi na Masoko
 
Mada nyingine ndogo iliyowasilishwa ni Mapambano ya Wanawake Wanaharakati kwenye Ujira,Mishahara na Mazingira ya Kazi,Ustawi na Usalama wa Kijamii na Kiuchumi,Mikakati ya Mapambano ya Ukombozi wa Wanawake Kuweza Kupata Fursa ya Kumiliki Ardhi,Nguvu Kazi na Maisha Endelevu
 
Lengo la tamasha hilo ni kutoa fursa kwa wanawake,wafeministi,wapigania haki za binadamu na jinsia,kutafakari na kubadilishana ujuzi na tarifa kwenye masuala ya kipaumbele kwenye mada pana jinsia,demokrasia na maendeleo
 
Kuimarisha vuguvugu la usawa wa jinsia,demokrasia na maendeleo kutokana na uzoefu na ujuzi wa wanaharakati,ikiwa ni pamoja na kusherehekea nguvu ya wanaharakati na kuimarisha ushirikiano katika kujenga vuguvugu la kutetea haki za kiuchumi na ukombozi wa wanawake katika ngazi na nyanja zote za jamii
 
Kuweka kumbukumbu na kubadilishana uzoefu katika harakati za kimapinduzi za kuleta mabadiliko chanya kwenye masuala ya jinsia,demokrasia na maendeleoa
Tamasha la mwaka huu limeunganisha watu kutoka katika nchi za Uganda,Zimbabwe,Burundi,Ghana,Afrika Kusini,Marekani,Kenya na Ufaransa na kufanikiwa kupata washiriki 2500 kutoka ngazi ya Wilaya na vijiji nchini kote
 
Masuala yanayopewa kipaumbele katika tamasha la mwaka huu yalijengwa kutokana na ushiriki mpana na mawasiliano yaliyofanyika kati ya waandaaji na wanaharakati katika ngazi ya kijamii,kitaifa,kikanda na kimataifa
 
Akizungumzia Mwongozo wa muktadha wa Tamasha la Jinsia kwenye uzinduzi wa Tamasha la mwaka 2011,Mwenyekiti wa Tamasha la Jinsia Mary Rusimbi alisema kuwa Tamasha ni nafasi ya wazi kwa ajili ya watu binafsi,vikundi,mashirik na mitandao walio katika mapambano yanayofanana ili kubadilishana uzoefu,taarifa na kujengana uwezo
 
Rusimbi alisema kuwa wanaharakati hao hukutana na kusherehekea mafanikio na kuthamini changamoto zilizo mbele yao,ili kuchangia katika mijadala ya wazi kuhusu maendeleo,kujenga na kuimarisha mitandao na kupanga kwa pamoja kwa ajili ya kuleta mabadiliko ya kijamii kwa mtazamo wa ukombozi wa wanawake kimapinduzi
 
Alieleza zaidi kuwa tamasha la jinsia 2011 linafanyika wakati muhimu katika historia ya Tanzania na Afrika kwa ujumla kutokana na ongezeko kubwa tangu 2008 la ubadhilifu wa rasilimali za taifa kama vile ardhi,madini,maji,misitu na nyinginezo
 
Alisema kuwa ubadhilifu huo unaofanywa na mashirika ya uwekezaji ya kitaifa kwa kuungwa mkono na serikali za nchi za afrika na wahisani pia wakati huo huo mapambano dhidi ya unyonyaji yameongezeka kwani miaka 50 baada ya uhuru Tanzania bado haijaweza kujitegemea kiuchumi,kisiasa,kijamii,kijeshi,kidini na kiutamaduni
 
Alieleza kuwa Tanzania bado imetawaliwa na utegemezi mkubwa kwa nchi za magharibi kupitia makampuni makubwa ya kimataifa ya uwekezaji na kupelekea taasisi hizo kudhibiti kwa kiasi kikubwa sera zetu za kiuchumi
 
Alifafanua kuwa Serikali imekuwa ikitekeleza kwa niaba yao,sera za utandawazi kupitia sera za ulegezaji wa uchumi na uuzaji wa bidhaa nje ili kuweka mazingira wezeshi kwa makampuni ya kibepari badala ya wazalishaji wadogo wadogo
 
Alisema kuwa matokeo yake mapato ya serikali yanazidi kutegemea makampuni machache yanayouza nje bidhaa kama vile maua,mbogamboga,madini,utalii na viwanda ambapo wanawake ndio waathirika na unyonyonywa zaidi na mfumo uliopo kwani wengi wao ndio wazalishaji wadogowadogo iwe ni wakulima,wafugaji au wavuvi
 
Alisema kuwa wao ndio wanaonyonywa zaidi na kuporwa rasilimali kutokana na mwingiliano wa mifumo kandamizi ya kibeberu,kibepari na mfumo dume na kufanya wao kunufaika zaidi iwapo mifumo hii kandamizi ya kiuchumi itaondolewa
 

WASHIRIKI WA TAMASHA LA JINSIA 2011 WATAKA WAFANYAKAZI WA NDANI WATHAMINIWE KWA KUPEWA HAKI ZAO ZOTE

Na FATUMA KITIMA ,Dar es Salaam.
SERIKALI imetakiwa kuwajibika na kuchukua hatua pamoja na mipango endelevu kwa jamii hasa kwa wafanyakazi wa ndani ili kuweza kuwasaidia watoto hao kuondokana na ukatili uliokithiri.
Wakitoa changamoto hizo wanaharakati mbalimbali katika Tamasha la Jinsia ,Demokrasia na Maendeleo Tanzania (TGNP) katika viwanja vya Mabibo jijini Dar es Salaam, walisema kuwa kukosekana kwa mipango madhubuti iliyowekwa na Serikali ndiyo kumesababisha tatizo hilo lilipo kwa sasa.
Mwanaharakati Sophia Kimbereja kutoka Wilaya ya Newala mkoani Mtwara  alisema kuwa Serikali iangalie kwa kina zaidi watu wanaowafanya ukatili kwa watoto hao katika nyumba zao na  kuchukuliwa hatua za kisheria.
“Wanawake tushirikiane kwa pamoja katika kutokomeza ukatili kwa watoto kwani tukiamua tunaweza “alisema Bi. Kimbereja.
Alitoa mwito kwa Serikali kuchukua hatua kwa watu wanaoenda vijijini kuchukua watoto na kudai wanakwenda kufanya kazi za ndani kumbe wanawachukua kwa lengo la kuwatumikisha katika biashara za ukahaba.
Kwa upande wake Matesa Bandoma aliainisha kuwa katika tatizo hilo la ukatili ambalo limekithiri linawakumba familia za hali ya chini kwa kuwa watoto zao ndio wanafanya kazi wa ndani.
“ Sisi kama wazazi au wanawake inabidi tubadilike ili jamii zetu ziweze kuwa bora kwa maendeleo yetu na vizazi vijavyo kwani tusipofanya hivyo watoto wetu watatulaumu kwa kushindwa kutimiza wajibu wetu”alisema Bandoma
Bandoma aliongeza kuwa mbali na changamoto hiyo ya ukatili lakini  kuna idadi kubwa ya wafanyakazi wa ndani hawajui kusoma na kuandika .
mwisho