About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Sunday, July 22, 2012

WANANCHI WAPATA MASHAKA NA MKANDARASI WA UJENZI WA LAMI NAMTUMBO HADI TUNDURU

Na Steven Augustino, Tunduru SERIKALI imeombwa kuichukulia hatua kampuni ya progressive Constraction  iliyopewa kazi ya kujenga kwa kiwango cha Lami Barabara ya Tunduru hadi Namtumbo Mkoani Ruvuma zikiwa ni juhudi za Serikali kuiunganisha mikoa ya Kusini kwenye mtandao wa barabara za kiwango cha Lami.

Hayo yamesemwa na baadhi ya wananchi waliotakiwa kutoa maoni yao juu ya maendeleo ya Ujenzi wa Barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 180 wenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni. 180.66 ambazo ilipewa kampuni hiyo kwa makubaliano ya kuikamirisha katika kipindi cha miezi 27 inayoishia mwezi july 2013.

Wakifafanua maelezo yao walidai kuwa Mradi huo ambao hadi sasa umetimiza miezi 16 iliyopita kampuni hiyo bado haijakamirisha hata ujenzi wa kambi zao hali inayo onesha wazi kutokuwepo kwa matumaini ya mradi huo kukamirisha ujenzi wake hata ikipewa miaka 10 zaidi wakiwa na maana kuwa kampuni hiyo haina uwezo kwani hata vyombo haina.

Goerge Mrope, Fatu Alli, Mohamed Said na Adam Mkwanda ni miongoni mwa wananchi waliotoa maoni hayo na kudai kuwa endapo serikali haitachukua hatua za kuuokoa mradi huo na kuufanya ukamilike kwa wakati kuna hatari ya Chama tawala CCM kufanya vibaya katika matokeo ya uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015 ambapo wapigakura hawatakuwa tayari kusikiliza la mtu na badala yake itakuwa ni kukisulubu tu.

Nao Madiwani Athuman Nkinde, Msenga Said na Mchungaji Wiliam Mazuguni katika maoni yao walionesha mashaka ya kuanguka kwa chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi huo kutatokana na wananchi wengi kuwa na uelewa hasa wakati huu ambao vyama vya siasa vya Chadema na CUF vinaendelea kujijenga na kuanza kuimung`unyua na kuwateka wanachi wa mikoa ya kusini ambako kumekuwa ni ngome kubwa ya CCM toka nchi hii ipate Uhuru.

Walisema ili kuokoa hali hiyo hatua madhubuti zinatakiwa kuchukuliwa na kufanyika kwa kazi ya ziada kwa dalili za kushindikana kukamilika kwa barabara hiyo katika kipindi kilicho pangwa zinaonekana kugonga ukuta kutokana na kampuni hiyo kuonekana kuifanya kazi hiyo kwa mwendo wa Kinyonga huku ikiwa imebakia miezi 11 ya kuikabidhi huku wakibainisha kuwa chanzo cha kuichelewa kukamirika kwa mradi huo ni uchakachuaji uliofanywa viongozi wa Wizara ya Ujenzi kutokana na kutoa kazi zote kwa mkandarasi mmoja badala ya kila kipande kupewa kampuni tofauti.

Kwa mujibu wa maelekezo ya Mikataba ya Barabara hiyo ilyogawanywa katika vipande vitatu, kipande cha Tunduru Matemanga Kilometa 58.70 Shilingi Bilioni. 63.41 kilipangwa kukabidhiwa mwezi July 2013, Matemanga Kilimasera kilometa 68.20 chenye thamani ya Shilingi Bilioni. 64.02 kilipanwa kukabidhiwa mwezi Mei 2013 na Kilimasera Namtumbo Kilometa 60.70 Chenye thamani ya Shilingi Bilioni.53.23 kilipangwa kukamilika mwezi march 2013.

Wakizungumzia hali hiyo Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu, Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Bakari Nalicho na Meneja wa wakala wa Barabara TANROADs Mkoa wa Ruvuma Eng. Abraham Kisimbo waliungana na wananchi hao kwa madai ya kutoridhishwa wala kufurahishwa na maendeleo ya Mradi huo na kuongeza kuwa serikali inajitahidi kwa kutumia nguvu zao zote kubanana na kusukumana kukabiri vitendo vya Mkandarasi wa kampuni hiyo na kuhakikisha kuwa barabara hiyo inajengwa.

Aidha Mwambungu aliwapongeza wakandarasi wanaojenga Bara bara za Songea/ Namtumbo kilometa 67.00 utakao ghalimu Shilingi Bilioni.62.88 na Peramiho/Mbinga kilometa 78.00 wenye thamani ya shilingi Bilioni.79.81 kuwa inaendelea vizuri na akaongeza kwa kuonesha mashaka ya mdororo wa ujenzi wa Barabara ya Tunduru/ Namtumbo kuwa huenda mradi huo ukapitwa na miradi mipya ya Barabara za Tunduru Mtambaswala Kilometa 202.5, Shilingi Bilioni.240.858 na Mbinga /Mbambabey kilometa 66.00 utakao ghalimu shilingi Bilioni.2.90.

Wakati hayo yakiendelea taarifa zilizovuja kutoka kwa wakaguzi wa Barabara hiyo waliotembelea Wilayani Tunduru July 12 mwaka huu zinadai kuwa kampuni hiyo hadi sasa imefanya kazi kwa asilimia 1 tu toka ikabidhiwe kazi hizo katika kipindi hicho cha miezi 16 iliyopita

MWISHO