About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, May 29, 2012

WAZEE WILAYANI TUNDURU WALILIA MATIBABU BURE

Na Steven Augustino, Tunduru

WAKATI Serikali ikitamba kutoa matibabu bure kwa Wazee na  Watoto chini ya miaka mitano,Wazee Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma wamelalamikia kutozwa fedha pindi wanapoenda kupata huduma za
matibabu,

Hayo yalibainishwa na Shekhe Mkuu wa Baraza la Waislamu Tanzania ( Bakwata) Wilayani humo Alhaji Waziri Alli Chilakweche wakati akiongea na Viongozi wa madhehebu hayo na viongozi wa kimila  katika ibada maalumu ya Hitma ya kuwakumbuka marehemu na wanafamilia wa Mwenyekiti Mstaafu wa Jumuiya ya Wazazi wa CCM Ndawambeb Mugwa iliyofanyika katika Kijiji cha Muhuwesi.

Akifafanua katika hotuba hiyo alhaji Chilakweche alisema kuwa kinacho washangaza wazee hao ni kutotekelezwa kwa ahadi za Serikali katika utoaji wa huduma za matibabu hayo bure mbali na kuwepo kwa taarifa za wazi juuu ya haki kwa wazee hao kupata huduma hiyo bure,

Alisema kama kweli Serikali ilitoa maagizo na maelekezo hayo kwa moyo wote kwanini wanashindwa kusimamia utekelezaji wake? Alihoji Shekhe Chilakweche na kuongeza kuwa kinacho tatanisha ni vitendo vya waliopewa mamlaka kutotambua hata vitambulisho vya misamaha kwa wazee vilivyo tolewa katika ngazi na maeneo tofauti wakidai kuwa wakitaka huduma waende huko.

Alhaji Chilakweche aliendelea kufafanua kuwa endapo Serikali inawapenda wazee na kuthamini mchango wao inapaswa kuzingatia maelekezo hayo ili kuwaokoa wasife kwa kukosa dawa kutokana na kukosa fedha .

Aidha katika hotuba hiyo pia Alhaji Chilakweche akatumia nafasi hiyo kuwaagiza Mashekhe wa Misikiti yote Wilayani humo na viongozi wa kimila kutumia nafasi zao kuwaomba wananchi kujitokeza kwa wingi na kuhakikisha wanahesabiwa katika zoezi la sensa iliyopangwa kufanyika Agosti 26 mwaka huu na kuhakikisha kuwa wanatoa maoni yao katika zoezi la kutafuta maoni ya kuandika katiba mpya.

Mwisho