About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Wednesday, March 6, 2013

MAAFISA UGANI WAPATIWA MAFUNZO YA ZAO LA UFUTA



Na, Stephano Mango,Pwani
MAAFISA Ugani nchini wametakiwa kukithamini na kukiendeleza kilimo cha zao la Ufuta ili kiweze kubadilisha maisha ya watanzania kutokana na mahitaji ya soko kuwa makubwa kwa sasa na kufanya zao hilo kwa baadhi ya maeneo kuwa zao kubwa la kibiashara

Hayo yalisemwa na Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Nurdin Babu kwenye ufunguzi wa mafunzo maalumu kuhusu kilimo bora cha ufuta, uliowashirikisha maafisa ishirini na wadau mbalimbali wa zao la ufuta wilayani Rufiji Mkoani Pwani yaliyofanyika  Mji mdogo wa Ikwiriri Wilayani Rufiji

Babu alisema kuwa Ufuta ni zao lisilotiliwa maanani na wakulima wengi nchini kwa miaka mingi pamoja na uwingi wa faida zake kwa binadamu, lakini kwa miaka ya hivi karibuni, takribani sehamu zote ambako hali ya hewa imekuwa rafiki wa kulistawisha zao hilo, wakulima wengi wameligeukia na kuanza kulima kwa kasi.

Alisema kuwa Wilaya ya Rufiji ni mojawapo ya wilaya ambazo zinastawisha zao la ufuta kwa siku nyingi na siku za hivi karibuni kasi ya uzalishaji imeongezeka kutokana na upatikanaji wa uhakika wa soko la ufuta.

“Hili ni zao lenye faida kubwa kama utekelezaji wa taaluma ya uzalishaji utafuatwa kwa makini, ambalo ndiyo lengo kuu la mafunzo haya na ni lazima walau kwa kuanzia tani elfu tano (5000) katika msimu ujao wa kilimo 2012/2013 kutoka tani za sasa 400 kwa mwaka na tani 280 mwaka 2005/06., anasisitiza Babu.

Akizungumza kwenye Mafunzo hayo Afisa Habari Mshauri Mkoa wa Pwani Silas Bwena alisema kuwa Serikari kupitia wizara ya viwanda, biashara na masoko, chini ya mradi wa MUVI mkoa wa Pwani imetoa mafunzo hayo kwa maafisa ugani ili waweze kuifikisha Elimu waliyoipata moja kwa moja kwa walengwa, ambao ni wakulima wadogowadogo walioko kwenye kata na vijiji husika.
Bwena alisema kuwa Mafunzo hayo yamelenga kumuwezesha mkulima kupata taaluma na uelewa mzuri zaidi katika kilimo cha zao hili tofauti na wanavvoelewa sasa ili kuboresha uzalishaji kwa lengo la kuongeza mazao yaliyo bora yatakayowezesha kupata bei nzuri kwenye soko
MWISHO