About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Friday, September 30, 2011

HATMA YA KUFUKUZWA UWANACHAMA MADIWANI WATANO SONGEA MJINI MIKONONI MWA KAMATI YA SIASA YA HALMASHAURI KUU YA CCM MKOA WA RUVUMA

                       
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Songea Mjini Hemed Dizumba
                        
Katibu wa CCM wilaya ya Songea Alfonce Siwale
Na  Mwandishi Wetu,Songea
CHAMA cha  Mapinduzi(CCM) Wilaya ya Songea mjini Mkoa wa  Ruvuma  kimetoa mapendekezo ya kuwafukuza uanachama wa chama hicho  madiwani  watano kwa madai ya kukiuka taratibu za chama hicho kwa kupiga kura za hapana kwa mgombea wa umeya Bw. Charles Mhagama anayedaiwa kupitishwa kwa kura za hapana 14 na za ndiyo 12.
Katika kikao cha kamati ya siasa kilichokaa hivi karibuni ambacho kolikuwa na ajenda tatu ikiwemo agenda ya kufungua mkutano,kupata taarifa ya kamati ya maadili ya Ccm Wilaya kuhusu uchaguzi wa Umeya uliofanyika Septemba 23 mwaka huu na kufunga mkutano ambapo Madiwani hao katika kikao cha kwanza cha maadili walitishia kurudisha kadi za chama hicho kutokana na kutoridhishwa na muenendo wa chama hicho unaotokana na kuvurugwa na kigogo mmoja wa ngazi ya Serikalini
Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu sakata hilo jana ofisini kwake Katibu wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Songea Alfonce Siwale alikiri kufanyika kwa vikao hivyo viwili cha maadili na kamati ya siasa na kudai kuwa madiwani wote wa chama hicho walihojiwa kuhusu mwenendo wa uchaguzi wa Umeya
Siwale alisema kuwa baada ya kikao cha maadili kuwahoji madiwani wote ndipo kamati ya siasa ya halmashauri kuu ya wilaya ilipoketi na kujadili kwa kina kilichojili kutoka kwenye kamati ya maadili kuhusiana na uchaguzi huo

Katibu huyo alieleza kuwa kuna mambo mengi yamejadiliwa kwenye kikao hicho pamoja na mwenendo wa chama baada ya uchaguzi huo wa Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea uliokitia doa chama cha Ccm na kumdharirisha Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Dkt Emmanuel Nchimbi
Alipotakiwa na waandishi wa habari kueleza kilichojadiliwa kwenye kikao hicho,Siwale alieleza  kuwa kanuni za chama hicho zinaeleza kuwa kinachojadiliwa na Kamati ya Siasa ya halmashauri kuu ya Wilaya kinakuwa siri kwani mambo yake mengi yanawasilishwa kwenye Kamati ya Siasa ya chama hicho mkoa ili kiweze kuyajadili na kuyatolea maamuzi hivyo wao ndio wanaweza kutoa taarifa sahihi kwa kile tulichowapelekea kutoka Wilayani
Alipoulizwa kuhusu habari zilizozagaa mitaani kuwa Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Dkt Nchimbi ndiye aliyeshinikiza kurudishwa jina la Diwani wa kata ya Matogoro Charles Mhagama na Madiwani wawili wa Viti Maalum ,alikanusha kuwa sio kweli na kama mtu anaushahidi wa hilo basi ieleweke alifanya hivyo kwa ushawishi wa kawaida wa uchaguzi
Kwa upande wake wa Katibu wa Ccm Mkoa wa Ruvuma Emmanuel Mteming”ombe alipohojiwa na waandishi wa habari kuhusiana na sakata hilo alisema kuwa wamepokea mapendekezo kutoka Ccm Wilaya ya Songea Mjini  ya kuwafukuza madiwani watano wa chama hicho na Kamati ya Siasa ya Ccm Mkoa inaendelea na vikao vyake ili kuweza kufikia hitimisha la sakata hilo
Mteming”ombe alisema kuwa hali ya chama kwa sasa ni tete hivyo maamuzi mengi  yanayofikiwa katika vikao vya chama hicho vinapaswa kuzingatia matakwa ya wananchama wake ili kuweza kurudisha imani kwa wananchi ambao ndio wanaokiangalia chama hicho kwa ukaribu sana
Awali ilidaiwa kuwa madiwani saba wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea wanatarajiwa kunyang”anywa kadi na Chama hicho kutokana na kukisaliti chama hicho kwa kumpigia Diwani wa Kata ya Matogoro Charles Mhagama kura za hapana 12 na za ndio 14 katika uchaguzi wa septemba 23 mwaka 2011 na kuwataja madiwani hao kuwa na kata zao kwenye mabano  Christian Matembo ( SeedFarm),Faustine Mhagama(Mshangano)
Wengine ni Victor Ngongi(Ruvuma)Kurabest Mgwasa(Msamala)Gelard Ndimbo(Ruhuwiko)Wilon Kapinga (Ndilimalitembo)na Genfrida Haule diwani wa Viti Maalum wa Chama hicho
MWISHO

HAYA NDIYO MTANDAO HUU UMEWEZA KUKUSANYA SIKU YA UZINDUZI WA GARI YA DHAHABU ILIYOFANYIKA KWENYE VIWANJA VYA NSSF

 Mtendaji wa TCCIA mkoa wa Ruvuma Philemon Moyo akionyesha gari ya dhahabu iliyotolewa kwa wajasiriamali juzi kwa ushirikiano wa KOICA na TCCIA mkoa wa Ruvuma
 Wakorea wa Kujitolea wakiwa na nyuso za furaha wakati wa hafla ya uzinduzi wa gari ya dhahabu
 Wakorea wa Kujitolea wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa hafla ya uzinduzi wa gari ya dhahabu juzi
 Viongozi wa Korea,TCCIA na Kaimu Mkuuwa Mkoa wa Ruvuma Thomas Oley Sabaya wakizindua gari ya dhahabu kwa kupakia bidhaa za wajasiriamali katika gari hilo
 Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Thomas Oley Sabaya akimpa zawadi ya Mvinyo Meneja wa Programu ya Wakorea wa Kujitolea Hwang,Jin Yung(Jenne) kushoto ni Mwenyekiti wa TCCIA mkoa wa Ruvuma Mays Mkwembe
 Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Ruvuma Mays Mkwembe akizungumzia mfumo wa utafutaji wa Masoko na Uuzaji bidhaa kwa kutumia gari ya dhahabu
Meneja wa Programu ya Wakorea wa Kujitolea Hwang,Jin Yung akitoa hotuba wakati wa uzinduzi wa gari ya dhahabu
Mtaalamu wa Masoko wa Kujitolea Jaehong,Cho akitafsiri hotuba iliyotolewa na Meneja wa Programu ya Wakorea wa Kujitolea Hwang,Jin Yung wakati wa uzinduzi wa gari ya dhahabu