About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, November 7, 2011

AJINYONGA KUTOKANA NA KUKATA TAMAA YA MARADHI SUGU YANAYOMSUMBUA

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Michael Kamhanda
Na Gideon Mwakanosya,Songea
BAKARI Hassani ( 30) Maarufu kwa jina la Namopwe Mkazi wa Kitongoji cha Moponi mashambani kilichopo katika Kijiji cha Nakapanya Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma amekutwa akiwa amekufa huku akiwa amening’inia kwenye tawi la mti mrefu baada ya kujinyonga kwa kutumia kamba ya katani.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda amesema kuwa tukio hilo lilitokea novemba 5 mwaka huu majira ya saa 7 mchana huko katika Kitongoji cha Moponi mashambani kilichopo katika Kijiji cha Nakapanya.
Amesema kuwa inadaiwa siku hiyo ya tukio majira ya saa za mchana Wananchi waliokuwa wakipita kwenye eneo la tukio walishtuka kuona mtu akining’inia kwenye mti mrefu ambao upo kandokando ya barabara na baadaye wananchi hao walipiga kelele kwa ishara ya kuomba msaada na muda mfupi tu watu walifika kwenye eneo hilo ukiwemo uongozi wa Serikali ya Kijiji cha Nakapanya .
Ameeleza zaidi kuwa baadaye uongozi wa Serikali ya Kijiji hicho ulitoa taarifa ya tukio hilo katika Kituo cha polisi mjini Tunduru na askari walipokwenda kwenye eneo la tukio nao waliukuta mwili wa Bakari ukiwa unaning’inia juu ya mti mrefu.
Alisema kuwa askari hao ambao waliongozana na mganga toka hospitali ya Serikali ya Wilaya ya Tunduru walibaini kuwa Bakari alikuwa amejinyonga kwa kutumia kamba ya katani ambayo alijifunga shingoni kisha kujining’iniza kwenye mti mrefu.
Amebainisha zaidi kuwa uchunguzi wa awali wa polisi kwenye kitongoji hicho umebaini kuwa Bakari kabla hajafikia uamuzi wa kujinyonga alikuwa akilalamika kwa muda mrefu kuwa amekata tamaa ya kuishi duniani kutokana na kuugua kwa muda mrefu maradhi hayakuweza kutajwa.

KARDINARI PENGO AWAPONGEZA WATANZANIA KWA KUITUNZA AMANI NA MSHIKAMANO WA TAIFA MIAKA 50 YA UHURU

 Na Augustino Chindiye,Tunduru
IMEELEZWA kuwa wakati Taifa la Tanzania likielekea kutimiza Miaka 50 ya UHURU  Wananchi wake wameishi katika amani na utulivu licha ya kuishi katika lindi la umasikini uliopindukia hali inayo onesha kuwa mgao wa rasilimali za nchi hauendi kwa usawa.

Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Baraza la umoja wa Maaskofu Africa Mwasisi wa Jimbo la Tunduru-Masasi, Askofu Mkuu wa Jimbo kuu la Dar es salaam Mwadhama Polycarp Kardnali Pengo wakati akiongea katika maadhimisho ya Jubilei ya fedha ya miaka 25 ya Jimbo la TUNDURU –Masasi mjini hapa.

Alisema mbali na kuishi katika machungu hayo Watanzania wanatakiwa kupongezwa kutokana na kuishi katika Umoja licha ya kuwepo kwa tofauti za udini na akawataka waumini wa Madhehebu ya Kikristo kuyatumia maadhimisho ya Jubilei hiyo kugeuza mienendo na kuanza maisha mapya ya kiroho na kuondoa kasoro za kijamii kwa vile uhuru umo pia katia Uchumi, Siasa na jamii.

Kardinali Pengo ambaye alikuwa mgeni katika maadhimisho hayo aliongeza kwa kukemea kejeli ambazo zimekuwa zikitolewa na baadhi ya watu kuwa uenezaji wa Injili ambao umekuwa ukifanywa na makanisa si chochote wakati  bila juhudi hizo huenda nchi ingekwisha vurugika na kuivunja amani hiyo.

Akiongea na waamini katika ibada ya Misa takatifu iliyofanyika katika kanisa kuu la Mtakatifu Xafery, Askofu wa Jimbo la TUNDURU-Masasi Mhashamu Castory Msemwa alisema maadhimisho ya Uhuru wa nchi yetu iwe changamoto ya kuwafanya viongozi waliopewa mamlaka kutambua nafasi zao na kurudisha haki za jamii hasa waliopo vijijini ambao ndio walipa kodi hodari lakini wakiwa hawaoni manufaa yatokanayo na kodi zao.

Alisema maadhimisho hayo yalifanye Taifa lifungue milango ya kutoa na kupeana haki na stahili za kila mtu ili kuyafikia maisha Bora na si Bora maisha kwani Uhuru wa kweli ni ule unaomfanya mtu awe katika kupata mambo yote ya msingi katika maisha yake.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na uongozi wa Jimbo hilo, jimbo la TUNDURU- Masasi lilianzishwa oktoba 17/1986 chini ya Mhashamu Askofu Polycarp Pengo.