About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, July 23, 2012

MAVETERANI WA SIMBA WACHAPWA BAO MOJA NA MAVETERANI WA YANGA

 Maveterani wa Yanga wakiwa katika uwanja wa mazoezi ili kuweza kujiweka sawa katika mechi na Maveterani wa Simba

Mechi ambayo ilimalizika kwa kuichapa Simba bao 1 katika dakika ya 13 ya kipindi cha pili na mchezaji Kelvin Haule



 Wachezaji wa Maveterani wa SIMBA wakifanya mazoezi ili kuweza kuleta upinzani wa dhati katika mechi yake na YANGA




                     Mdhamini wa Mechi hiyo Golden Sanga (Sanga Transport) ambaye ni VETERANI WA YANGA
 Mdhamini wa Mechi hiyo Paskary Msigwa (Top One Inn) ambaye ni VETERANI WA SIMBA
 Mohamend Mchele (kushoto) akiwa na watazamaji wengine katika mechi hiyo
 wa kwanza toka kushoto ni Godfey Mvula, Peter Mhina na Amasha wakiwa na watazamaji wengine
 Washabiki wa Simba wakionyesha manjonjo yao katika uwanja wa Sokoine ambao mechi hiyo ilikuwa inachezwa jana
 Wachezaji wa Yanga Gerson Msigwa na Kabisama wakishusha pumzi wakati wa mapumziko
Methew Msigwa akiwa na wachezaji wenzake wakitafakari namna ya kuwafunga wapinzani wao wakati wa mapumziko ya kipindi cha kwanza

MKUTANO WA CCM MJINI KIGOMA

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala wa Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI,) Aggrey Mwanri akihutubia, kwenye mkutano wa CCM uliofanyika, jana , Julai 22, 2012, kwenye Uwanja wa Community Centre, Mwanga mjini Kigoma.

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye akihutubia, kwenye mkutano wa CCM uliofanyika, jana , Julai 22, 2012, kwenye Uwanja wa Community Centre, Mwanga mjini Kigoma.

Waziri wa Nchi Ofsi ya Rais, Mahusiano, Steven Wasira akihutubia kwenye mkutano wa CCM uliofanyika, jana , Julai 22, 2012, kwenye Uwanja wa Community Centre, Mwanga mjini Kigoma.
Mamia ya wananchi waliofurika kwenye mkutano wa CCM katika Uwanja wa Community Centre, Mwanga mkoani Kigoma

Wazee kwenye mkutano wa CCM, Uwanjwa wa Community Cetre Mwanga Kigoma

Viongozi mbalimbali wa CCM waliohudhuria katika mkutano huo

AUAWA KWA TUHUMA ZA KUIBA KANISANI


Na Augustino Chindiye, Tunduru

WANANCHI wenye hasira wamempiga na kumuua kazi wa mtaa wa Kadewele mjini Tunduru mkoani Ruvuma aliyefahamika kwa jina la Nasoro Hashim (18) baada ya kutuhumiwa kuingia na kuiba katika nyumba ya Paroko wa Kanisa kuu lililopo katika Jimbo la Tunduru/ Masasi.

Mashuhuda wa tukio hilo walidai kuwa katika mkasa huo marehemu Hashim alikutwa na kidhibiti cha simu tatu za mkononi mali za viongozi wa Kanisa hilo.

Walisema katika tukio hilo marehemu alishtukiwa baada ya kuonekana wakati akitoka katika nyumba hiyo na Sista mmoja ambaye hawakutaja jina lake ambapo baada ya kugundua hali hiyo alipiga kelele za kuomba msaada na kulifanya kundi hilo kujitokeza.

Walisema baada ya kipigo hicho marehemu alikimbizwa katika hospitali ya serikali ya Wilaya kwa matibabu ambapo alifariki baada ya muda mfupi.

Mganga aliye ufanyia uchunguzi mwili wa marehemu Hashim Dkt. Jeshi Daraja alisema kuwa chanzo cha kifo hicho ni kutokwa na damu nyingi kuliko sababishwa na kupasuka kwa fuvu la kichwa kulikotokana na kupigwa na kitu kizito.

Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Deusdedit Nsimeki, mbali na kukiri kuwepo kwa tukio hilo alisema kuwa Polisi wanaendelea na uchunguzi ili sheria iweze kufuata mkondo wake kwa waliohusika na tukio hilko.

Aidha kamanda Nsimeki alitumia nafasi hiyo kuwataka wananchi wa Mkoa huo kuachana na tabia za kuchukua sheria mikononi.
Mwisho