About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Sunday, March 18, 2012

WANNE WAKAZI WA DAR WAKAMATWA SONGEA NA MENO YA TEMBO

     Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda

NA DUSTAN  NDUNGURU,SONGEA.

WATU wanne wakazi wa jijini Dar es salaam wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoani Ruvuma kwa tuhuma za kukamatwa na nyara za serikali(meno ya tembo) zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni sita.

Akiongea na waandishi wa habari kamanda wa polisi mkoani hapa Maiko Kamuhanda alisema watu hao walikamatwa katika kijiji cha Suluti kwenye maeneo ya mashamba ya NAFCO wilayani Namtumbo aprili 15 mwaka huu majira ya saa 2.30 asubuhi.

Kamuhanda alisema watu hao walikamatwa na askari wa doria baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia wema wa kijiji cha Suluti.

Aliwataja majangili yaliyokamatwa kuwa ni John Andrew(30) ambaye ni dereva wa gari,Hemed Geofrey(30),Idd Manase(32) na Modesta Eliakim(25) wote wakazi wa Dar es salaam.

Kamuhanda alifafanua kuwa majangili hayo yalikamatwa yakiwa na vipande 30 vya meno ya tembo ambayo walikuwa wamepakia katika gari ambayo ilikuwa imebandikwa namba bandia DFP 7208 aina ya TOYOTA Landcruiser.

Alisema kwenye kadi ya gari hilo inaonyesha namba T.125 ATD Toyota Landcruiser mali ya Morrice Christopher Meenda na kwamba meno hayo ya tembo walikuwa wakiyapeleka Dar es salaam.

Kamanda huyo wa polisi aliwataka wananchi kuendelea kushirikiana na polisi kwa kutoa taarifa mbalimbali na kwamba mpango uliopo ni kwa jeshi hilo kuendelea kukabiliana na majangili hayo.

Hata hivyo alisema polisi wanaendelea na uchunguzi kuhusiana na tukio hilo.

                MWISHO.

NYUMBA 946 ZALIPOTIWA KUBOMOKA WILAYANI TUNDURU

                   Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Juma Madaha

Na Steven Augustino,Tunduru

NYUMBA  946 zimeripotiwa kubomoka kutokana na  mvua kubwa zinazoendelea kunyesha mfululizo Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma na kuwaacha wakazi wake wakiwa hawana makazi.

Hayo yamebainishwa na Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Tunduru, Afisa Tarafa wa tarafa ya Matemanga  Ally Hatibu na kuongeza kuwa pia mvua hizo zimebomoa vyoo 35 na kusomba mazao katika mashamba ya wakulima 56 na kwama hivi sasa wananchi hao wanahifadhiwa na Ndugu, jamaa na marafiki katika maeneo yao.

Hatibu aliendelea kueleza kuwa pamoja na matukio hayo pia. Mvua hizo zimeharibu vibaya  miundombinu ya barabara, Madaraja  yanayounganisha kati ya Wilaya hiyo na makao makuu ya Mkoa huo barabara za kwenda vijijini.

Akifafanua taarifa hiyo  Hatibu alisema kuwa Tarafa ya Milingoti ndiyo iliyo athirika zaidi kutokana na kubomokewa na nyumba 716 huku takwimu zikionesha kuwa tarafa ya Lukumbule ikifuatia kwa kuwa na nyumba 230 zilizo bomoka kufuatia mvua hizo.

Aidha takwimu za maafa hayo zinaonesha kuwa Kata ya Nakayaya ndiyo inayo ongoza kutokana na kubomokewa na Nyumba 122, Kata ya Milingoti 99, Masonya 88, Nanjoka 57,Mchangani 54 huku kata ya majengo ikishika nafasi ya mwisho kutokana na kubomokewa na nyumba 46.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo daraja lililobomoka ni la mto Masonya liliteteleka kutokana na mto huo kujaa pamoja na madaraja ya mito Nasanga na Msinjewe pamoja na mto Mkandu barabra iendayo katika vijiji vya tarafa za Lukumbule, Nalasi na Mchoteka na kusababisha usumbufu
kwa wanananchi kutokana na baadhi ya magari kusitisha safari za kwenda na kuingia mjini Tunduru huku kukiwa na wimbi la ongezeko la nauli kwa magari yanayokubali kufanya safari hizo kwa kubahatisha.

Hatibu aliendelea kubainisha kuwa miongoni mwa usumbufu unaowapata madereva wanaofanya safari katika maeneo hayo  ni pamoja na kutozwa fedha na wananchi walio panga miti katika maeeenero yaliyo haribika na kuwatoza kati ya Shilingi 5000 na Tsh.2000 kwa kila gali linapo vuka kuelekea upande wa pili.

Alisema kufuatia hali hiyokamati ya Ulinzi na usalama ililazimika kuwatembelea wahanga na kuwapa pole kwa mkasa huo pamoja na kujionea uharibifu wa madaraja hayo na kupeleka taarifa za maafa hayo katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ili kuangalia uwezekano wa wahanga hao kupatiwa msaada Serikalini.

Kuhusu uharibifu wa miundombinu ya Barabara na madaraja hayo, Hatibu alisema kuwa tayari Meneja wa Wakara wa Barabara Mkoa wa Ruvuma (TANROAD`s) amekwisha tuma wataalamu Wilayani humo kwa ajili ya kuhakikisha kuwa barabara zote zinafunguka na shughuli kuendelea kama kawaida.

Mwisho