About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Friday, April 26, 2013

NI UJUMBE WA MAJONZI AMBAO UMEWALIZA WENGI ULIOTOLEWA NA JOSHUA NASSARI MBUNGE WA ARUMERU MASHARIKI KUHUSIANA NA POLISI KUPIGA MKWALA NYUMBANI KWA LEMA NA TISHIO LA KUKAMATWA KWAKE

Nimepata kwa mshtuko na nikakataa kuamini kama ni kweli kuwa polisi wa Arusha wamevamia na kuizingira nyumba ya mbunge mwenzangu wa Arusha, Lema.


Nimelazimika kumpigia simu RPC kuthibitisha na cha ajabu akaniambia ni kweli.

Nimemshauri kama kiongozi mwenzake mwenye dhamana ya kusaidia kuilinda

kweli na haki ili kuleta Amani ya kweli kwenye mkoa wangu wa Arusha. Sidhani kama ni busara kutaka kuvamia nyumbani kwa Raia mwema achilia mbali Kiongozi mkubwa kama mbunge. "Kama watawala wanafanya hivi kwa mti mbichi, itakuwaje kwa mti mkavu" itakuwaje kwa mwananchi wa kawaida anayeishi usa river au unga ltd? Ukifuatilia na kuangalia video ya tukio la uhasibu chuoni arusha, utagundua makosa ya mtawala mkuu wa mkoa, ambaye kimsingi ni mkiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa kuwa sehemu ya sababu ya uvunjifu wa amani, kutokujua hata kusoma saikolojia ya watu.

Nyumbani kwa mbunge hakai mbunge mwenyewe. Kuna watoto akiwemo mwenye umri wa miezi mitano, mke, ndugu etc. Utapigaje mabomu kwenye nyumba hii, bila shaka yatakuwa mauaji. Lema si jambazi, ni kiongozi, ni role model, ni raia mwema sana na mzalendo kwa taifa lake.

Hii wapi sababu ya kuvamia kwake usiku na kuwapa wanafamilia pychological tortue.

Kama amenielewa atasikia, otherwise "truth will always stand" . Tuko tayari na tulishakuwa tayari, hatujashtukizwa. Tunaendelea kuongezewa kura za madiwani arusha juni 16, 2013. Ni vyema watawala wakakumbuka habari ya Farao na Mungu juu ya mateso ya wana wa Israel utumwani. "Mungu akaufanya moyo wa farao kuwa mgumu, ili azidi kujidhihirisha kwa wana wa Israel"

MWISHO