About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Saturday, January 28, 2012

MADIWANI MKOANI RUVUMA WAMETAKIWA KUSIMAMIA KIKAMILIFU MGAO WA PEMBEJEO ZA RUZUKU

                           Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu
Na Revocatus Kassimba ,Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Ruvuma
MADIWANI mkoani Ruvuma wametakiwa kutumia madaraka waliyonayo kuhakikisha wananchi walengwa wananufaika na mgao wa pembejeo za ruzuku  kwa njia ya vocha znzazotolewa na serikali zinafika kwa wakati na hakutokei udanganyifu.
Rai hiyo imetolewa jana  na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu wakati wa kikao cha kawaida cha Baraza la madiwani katika Halmashauri hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa Klasta Mlingoti wilayani Tunduru
Mwambungu aliwaambia madiwani kuwa wao ndio wenyeviti wa kamati za maendeleo za kata hivyo ni muhimu wakashirikiana na serikali katika kuhakikisha walengwa wa kunufaika na pembejero za ruzuku za kilimo wanapata kupitia taratibu zilizowekwa.
“Nawaombeni sana madiwani tumieni nafasi zenu kuhakikisha vocha zinagawiwa kwa walengwa’ alisema mkuu wa mkoa na kuongeza kuwa lengo kuu la serikali ni kuwajengea uwezo wakulima kuzalisha kwa wingi na kwa ubora mazao yao.
Alisema kuwa serikali haitamwachia yeyote yule atakayekwenda kinyume na zoezi la vocha za pembejeo kwani hizi ni fedha za umma hivyo ni budi wananchi wakapatiwa ili zisaidie kuongeza uzalishaji wa mazao na kujihakikishia uhakika wa chakula.
Mwambungu alisisitiza juu ya mtendaji au wakala wa pembejeo za ruzuku atakayebainika kuchakachua vocha kuwa hatua za kisheria za kuwafikisha katika vyombo vya sheria zitachukuliwa mara moja
Katika msimu huu wa kilimo zaidi ya wakulima laki moja na tisini watanufaika na pembejeo za ruzuku za kilimo zikiwemo mbegu bora za mahindi,mpunga, mbolea ya kupandia na kukuzia katika mkoa wa Ruvuma.
Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amewataka madiwani wa halmashauri ya Tunduru kuhamasisha wakulima kuzalisha zao la mpunga ambalo linastawi kwa wingi wilayani humo ili liwe zao mbadala la biashara badala ya kutegemea korosho pekee.
Alisema hivyo kutokana na suala la soko la korosho za wakulima kuendelea kuzorota na kusababisha kero hivyo akawaasa kutumia skimu za umwagiliaji maji zilizopo wilayani humo kuzalisha mpunga huku serikali ikiendelea kutafutia suluhu ya soko la korosho hapa nchini.
“Tunaweza kutumia mpunga miaka ijayo kama zao la biashara hivyo tuwahamasishe wakulima kulima sambamba na korosho” alisisitiza Mwambungu

Na Revocatus Kassimba
Afisa Habari
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Ruvuma

KIKAO CHA MAANDALIZI YA MASHINDANO YA SANGA ONE CUP KIMEANZA MCHANA HUU

Kutoka kushoto ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji wa Sufa Mshamu Mkuruma,Adimu Rader
Kutoka kushoto ni Katibu Msaidizi wa Chama cha Mpira wa miguu Manispaa ya Songea Godfrey Mvula,wa pili ni Katibu wa Kamati ya Ufundi SUFA Francis Kasembe,Kumburu Laukila,Shaibu Mambo
Katibu wa Chama cha Mpira wa miguu Manispaa ya Songea Ajaba Chitete


KAMATI MASHINDANO YA SANGA ONE CUP KUZINDULIWA MCHANA HUUUUUUUUUUU

Na Stephano Mango,Songea
KAMATI ya kuandaa na kusimamia Mashindano  ya Sanga One Cup kuzinduliwa mchana huu katika viwanja vya Sanga One Bombambili
Akizungumza na Mtandao huu wa www.stephanomango.blogspot.com, Diwani Mstaafu wa Kata ya Bombambili na Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu ambaye pia ni mdhamini wa mashindao hayo Golden Sanga (Sanga One) alisema kuwa tayari wajumbe hao wamepatikana ambao watafanya uchaguzi mdogo ili kuweza kuwapata viongozi wake
Sanga alisema kuwa kazi yao kubwa itakuwa ni kuandaa mashindao hayo na kusimamia mashindano hayo kwa haki na usawa ili waweze kupatikana washindi stahiki na wachezaji bora watakaoweza kuibuliwa na mashindano hayo
Alisema kuwa anategemea kuwa wajumbe hao watawapata viongozi wenye busara na uzalendo katika kusimamia mashindano hayo,kuibua wachezaji chipukizi watakao chukuliwa kuchezea timu zingine za Wilaya,Mkoa na Taifa na kuleta ushindani mkubwa katika soka
Alieleza kuwa wajumbe wa kamati hiyo tayari wameanza kuwasili katika viwanja vya mkutano ili kuweza kutimiza lengo la kikao na kwamba anaamini kuwa kamati hiyo itafanya kazi yake vizuri kama ilivyokusudiwa
MWISHO