About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, January 23, 2012

WASHAURIWA KUTOJITOA KWENYE TAASISI ZA FEDHA WAKATI WA MTIKISIKO WA KIUCHUMI WA VYAMA HIVYO

Na Stephano Mango,Songea
WANACHAMA wa Chama  Cha  ushirika cha Akiba na Mikopo  cha walimu Songea Manispaaa wameshauriwa kuacha tabia ya kujitoa  uanachama kutokana na kukosa uvumilivu baada ya mikopo yao kuchelewa kutolewa kwa wakati  au wanapokosa mikopo  na badala yake  wametakiwa kuwa wavumilivu.
Wito huo umetolewa jana na Meneja mikopo wa benki ya NMB tawi la Songea Derick Fidelis wakati akifungua mkutano mkuu  wa  14 wa wanachama  wa chama hicho uliofanyika kwenye ukumbi wa Songea Club.
Amesema,Wanachama wanapaswa kuwa wavumilivu na si kukimbilia kujitoa pindi mikopo waliyoomba  kutoipata kwa wakati  na badala yake wajue kuwa matatizo hayo ni ya kawaida  hivyo wasikate tamaa wala kukimbia matatizo.
“Walimu tunapaswa kuwa  wavumilivu tuache tabia ya kujitoa uanachama pindi tunapokosa mikopo au kucheleweshewa mikopo , tuwe wavumilivu matatizo ni jambo la kawaida ,nyinyi  ni wadau wa kubwa wa NMB ili benki iendelee tunawategemea sana kwani mapato mengi ambayo yanaingia benki yanatokana na michango ya walimu,na mikopo mingi tunawakopesha walimu,”alisema Derick.
Aidha, Meneja mikopo ameahidi kuwa  benki hiyo itaendelea kuboresha huduma zaidi ili kufanikisha malengo ambayo  wateja wao wakiwemo walimu wanahitaji , ameishauri bodi ya chama hicho kukaa na kuomba mkopo ili kuweza kumalizia jengo lao ili kuinua uchumi wa chama hicho.
Akitoa  salamu wakati wa mkutano huo Mwenyekiti wa chama hicho  Martin  Challe amewataka wanachama hao kuendelea kuwa wajasili na kutokubali kuyumbishwa au kushawishiwa  kujitoa uanachama na watu ambao wasiopenda  na ustawi na maendeleo ya chama hicho.
“Tayari kunawachama ambao wamejitoa ukiuliza wanadai kuwa  kwa sababu uchumi wa chama siyo mzuri na kuchelewa kupata  mikopo  waliporudi kuomba  tena uanachama  nasi tumewakataa kwani walikimbia baada ya kuona tumeyumba,”alisema.
Mwisho.