About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Wednesday, April 17, 2013

MADIWANI WA CCM WAHOJIWA KWA KOSA LA KUSHIRIKI KUTAKA KUMNG'OA MEYA SONGEA

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Charles Mhagama

Charles Mhagama ambaye ni Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea akiwa na Diwani wa Kata ya Matarawe James Makene ambaye ndiye MHASISI wa kumtuhumu Meya

Na Stephano Mango, Songea


MADIWANI Sita wa Chama Cha Mapinduzi wakiwemo Madiwani wawili ambao waliungana na Madiwani nane wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo( Chadema) kuandika barua kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea ya kumuomba kuitisha mkutano maalumu wa Madiwani wenye madhumuni ya kujadili hoja za kutokuwa na imani na Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo Charles Mhagama ambaye anadaiwa kutumia nafasi yake vibaya wamehojiwa kwa nyakati tofauti na Kamati ya Siasa Ccm ya Wilaya ya Songea Mjini ikiwataka kujua muanganiko wao na Chadema katika sakata la kutokuwa na imani na Meya wao.

Uchunguzi uliofanywa na mtandao kwa zaidi ya wiki mbili sasa umebaini kuwa lengo kubwa la kamati hiyo ya siasa ni kutaka kufunika hoja ya msingi ya Madiwani kumi wa Halmashauri hiyo ya kutaka kuitisha mkutano ambao una lengo la kuelezea tuhuma zinazomkabili Charles Mhagama ambaye ni Mstahiki Meya wa Halmashauri hiyo bila kujali itikadi zao za kisiasa kwa masloahi ya wakazi wa Manispaa ya Songea

Imebainika kuwa Kamati hiyo ya Siasa iliyokutana tarehe 11/4/2012 iliwahoji, kuwatisha na kuwaonya Madiwani hao kuacha kuungana na Chadema kumtisha tisha Meya wao kwani kufanya hivyo kunaendelea kuwapa umaarufu Chadema ambao hawakitakii mema Chama cha Mapinduzi na badala yake kujikita kulinda heshima ya Ccm

Taarifa za ndani ya kikao hicho zimeeleza kuwa ndani ya kikao hicho kuliibuka malumbano makali yenye kupinga wazo la Chama kumbeba Meya ambaye anaonekana waziwazi kuwa hakubaliki ndani ya Baraza la Madiwani na nje ya baraza la hilo kutokana na mwenendo wake mbovu licha ya uchaguzi wake kutokuchaguliwa na Madiwani hao kwani alipigiwa kura 12 za ndiyo na kura 14 za hapana

Mtandao umebahatika kuiona barua ya Madiwani kumi wa Halmashauri hiyo yenye kumbukumbu namba MD/SO/013 ya Tarehe 15/3/2013 yenye hoja mbili ambazo zina vipengele vitano vinavyosisitiza kumuomba Mkurugenzi kuitisha mkutano maalumu wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa hiyo ,

Imebaini kuwa barua hiyo ndiyo ambayo imeichanganya kamati hiyo ya Siasa na kuamua kuitisha kikao cha dharula cha kuwatisha Madiwani hao kuacha mara moja mkakati huo na Chadema kwa maslahi ya Ccm kwani kufanya hivyo ni kukiaibisha chama na kukidhorotesha mbele ya umma

Madiwani hao ambao wamehojiwa na Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Songea Mjini ni James Makene Diwani wa Kata ya Matarawe, Victa Ngongi Diwani wa Kata ya Ruvuma, Faustini Mhagama Diwani wa Kata ya Mshangano, Kulabest Mgwasa Diwani wa Kata ya Msamala, Wilon Kapinga Diwani wa Kata ya Ndilimalitembo na Genfrida Haule Diwani wa Viti Maalum

Imebainika kuwa Madiwani wawili wa Chama cha Mapinduzi (Ccm)walioungana na Madiwani nane wa Chadema kuandika barua hiyo ni Diwani wa Kata ya Matarawe James Makene na Victa Ngongi ambaye ni Diwani wa Kata ya Ruvuma

Taarifa zilizoufikia mtandao huu zimesema kuwa Kanuni za Kudumu za Halmashauri hiyo za mwaka 2003 ibara namba 4 na ibara namba 80 zinaeleza ili kuitisha mkutano maalum wa baraza la Madiwani kujadili hoja mbalimbali za kutokuwa na imani na Meya kujiorodhesha na kufikia idani ya theluthi moja ya Madiwani na kueleza malengo ya mkutano huo

Katika Halmashauri hiyo kuna jumla ya Madiwani 28 ambao theluthi yao ni Madiwani 9 ambapo madiwani 10 ndio waliojiorodhesha na kuweka saini zao za kusudio hilo ambalo linaonekana kuwa ni mwiba mkali kwa Ccm

Mmoja wa Madiwani wa Ccm ambao wamehojiwa na Viongozi wa Chama hicho ambaye hakutaka jina lake litajwe ameuambia mtandandau huu kuwa toka awali Charles Mhagama hakuchaguliwa na Madiwani wa Halmashauri hiyo ndio kiini cha kuwepo kwa makundi mawili ambayo moja linamuunga mkono na na kundi jingine ambalo halikubaliani na kundi linguine licha ya utendaji kudaiwa kuwa ni mbovu

Diwani huyo alilesema kuwa Chama hakina uwezo wa kuwachagulia Madiwani Meya Mbovu na kuendelea kuweka mazingira ya kumlinda licha ya kuwa tuhuma zake kuwa wazi na kuwatesa wananchi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

Alifafanua kuwa jukumu la kumchagua Meya ni la Madiwani bila kujali itikadi ya chama chochote kwani Meya huyo ni kiongozi wa Madiwani kwa maslahi ya wakazi wa Manispaa ya Songea ambao ndio waliowachagua madiwani wawawakil;ishe kwenye malengo ambayo yana maslahi kwa jamii

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Ccm Wilaya ya Songea Mjini Gerod Mhenga alipohojiwa kwa njia ya simu jana alithibitisha kuwepo kwa kikao hicho cha Kamati ya Siasa ya Wilaya yenye lengo la kubaini tatizo lililopo kati ya Madiwani na Meya wao hadi kufikia hatua ya kuungana na Madiwani wa Chadema ya kumtaka Mkurugenzi kuitisha mkutano maalum wa kujadili mwenendo wa Meya

Akizungumza na mtandao huu Mstahiki Meya wa Halmashauri hiyo Charles Mhagama alikanusha baadhi ya tuhuma wanazo mtuhumu na kusema kuwa kama Madiwani wana jambo lao basi wanatakiwa kufuata kanuni ili ziwaruhusu kulisema jambo lao

Hata hivyo Mkurugenzi wa Manispaaa hiyo Nachoa Zakaria alipohojiwa jana ofisini kwake alisema kuwa Halmashauri inaweza kumuondoa madarakani Meya ni lazima kuwe na theluthi mbili ya madiwani wanaotaka kumuondoa na sio theluthi moja kama walivyoomba Madiwani hao kumi hivyo hawezi kuitisha kikao hicho bila kukidhi matakwa ya kanuni.

MWISHO