About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Friday, September 16, 2011

MKUU WA MKOA WA RUKWA ATUA KATIKA VIWANYA VYA TGNP-MABIBO,AKUTANA NA WANAHARAKATI NA WAANDISHI WA HABARI

 Mratibu wa Mtandao wa Jinsia Tanzania Lilian Liundi wa pili kutoka kushoto akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya (MB) alipotembelea Tamasha la 10 la mwaka 2011 lililomalizika jana katika viwanja vya Mabibo

 Mwenyekiti wa kamati ya Maadili na Mafunzo wa MCT Juma Nyumayo na Dada Lilian Liundi wakifuatilia kwa umakini mkubwa mikakati ya maendeleo iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanyaalipokuwa anazungumza na wafanyakazi wa TGNP na Waandishi wa Habari katika ofisi za TGNP
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akizungumza na waandishi wa Habari na Wafanyakazi wa mtandao wa Jinsia Tanzania(TGNP)
Huyu ndiye Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akisikiliza maoni mbalimbali ya maendeleo Mkoani Rukwa kutoka kwa Waandishi wa Habari

HEKAHEKA ZA WASHIRIKI WA TAMASHA LA 10 LA JINSIA KWA MWAKA 2011 ZINAENDELEA KWENYE VIWANJA VYA TGNP-MABIBO JIJINI DAR ES SALAAM

 Waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali kutoka mikoani wakijadiliana wakati wa tamasha hilo linalomalizika Septemba 16
 Washiriki wakifuatilia mada zinazowasilishwa wa Wanaharakati mbalimbali wakati wa Tamasha la Jinsia Tanzania kwa mwaka 2011
 Hawa ni miongoni mwa washiriki wakifuatilia mijadala mbalimbali katika viwanja vya TGNP-Mabibo wakati wa warsha za pamoja
 Ndivyo Tamasha la Jinsia lilivyokuwa kwani washiriki mbalimbali wakiendelea kupata mbinu za kujikomboa kutoka kwenye makucha ya ubeberu na ubepari unaoendelea kujitokeza barani Afrika
Hii ni sehemu tu ya washiriki wa Tamasha walivyokuwa katika hali ya umakini wakati wa Tamasha hilo

MASKINI JAMANI;;;;MAMA AGONGWA NA YEBOYEBO NA KUSABABISHA KIFO CHA MWANAYE

YEBOYEBO YAMGONGA MAMA NA KUSABABISHA KIFO CHA MTOTO
Na Gideon Mwakanosya,Songea
JESHI la Polisi Mkoani Ruvuma linamshikiria mwendesha Pikipiki mmoja Omari Mdoka mkazi wa kijiji cha Mchoteka kilichopo Wilayani Tunduru kwa tuhuma za kumgonga Mwanamke Halima Mohamedi (19) na kusababisha kifo cha mtoto wake aliyekuwa amebebwa mgongoni wakati anatoka shambani.
Akizungumza na Mwandishi wa mtandao huu wa www.stephanomango.blogspot.com ,Gideon Mwakanosya jana ofisini kwake Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoani Ruvuma Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Geoge Chiposi amesema kuwa tukio hilo limetokea September 15 mwaka huu majira ya saa 9 alasiri katika kijiji cha Mkalola kilichopo Wilayani Tunduru.
SSP Chiposi ameeleza kuwa siku hiyo ya tukio inadaiwa kuwa mwendesha pikipiki Mdoka akiwa anatoka Mchoteka kwenda Kijiji cha Mkalola alimgonga mtembea kwa mguu Halima Mohamedi ambaye alikuwa amembeba mtoto wake mgongoni Asha Mauridi Mwenye umri wa miezi tisa.
Amefafanua zaidi kuwa Mdoka ambaye alikuwa akiendesha pikipiki yenye namba za usajiri T 813 BLM, aina ya Sunlge alikimbia mara tu ya kutokea ajari hiyo, lakini baadaye wananchi wa kijiji hicho walifanikiwa kumkamata akielekea katika kijiji cha Nalasi.
Hata hivyo Kaimu kamanda wa Polisi SSP Chiposi ameeleza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni kwamba mwendesha pikipiki alikuwa kwenye mwendo mkali ambao ulisababisha kushindwa kumudu usukani wakati mwanamke huyo Halima Mohamedi akiwa amembeba mwanaye mgongoni akijaribu kumkwepa kandokando ya barabara upande wa kulia ambapo alimgonga na kukimbia na Polisi wanaendelea kufanya upelelezi na utakapo kamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kujibu mashitaka yanayo mkabili.
 MWISHO.