About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Wednesday, September 14, 2011

VIWANJA 6354 KWA SHUGHULI MBALIMBALI VYAPIMWA MPAKANI MWA TANZANIA NA MSUMBIJI

                                     Na Joseph Mwambije,Songea
HALMASHAURI ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma imepima jumla ya Viwanja 6354 katika eneo la mpakani mwa Tanzania na Msumbiji la Mkenda ili kulifanya eneo hilo kuwa Mji mdogo ulipangika kimipango miji  na kuwa Mji wa mfano wa mpakani Nchini
 
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Fanuel Ndemfoo wakati akizungumza na mwandishi wa mtandao wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ mjini Songea Joseph Mwambije ofisini kwake alisema kuwa hiyo ni awamu ya pili ya upimaji viwanja katika eneo hilo lenye daraja kubwa la Mkenda linaloziunganisha Nchi hizo mbili na kwamba awamu ya kwanza ya upimaji ilifanywa Januari 2009/2010 ambapo viwanja 1000 vilipimwa.
 
Alisema  kuwa ni nafasi nzuri kwa Watanzania kujitokeza  kuwekeza katika eneo hilo badala ya kuwaachia wageni na kujenga Hoteli,Shule,nyumba za kulaa wageni na uwekezaji mwingine.
 
‘Lengo letu ni kuwa na Mji mdogo ulipangika vizuri na kuwa  Mji wa mfano Nchini kwa kuwa Miji mingi ya mipakani haijapimwa na baadhi yake ni Namanga na Tunduma hivyo tunategemea mpaka mwaka 2015 tutakuwa na Mji ulikamilika na unaovutia’alisema Kaimu Mkurugenzi huyo.
 
Kaimu Mkurugenzi huyo anabainisha kuwa katika Mji huo mdogo wenye wakazi 3000 viwanja vya makazi vilivyopimwa ni 4775,viwanja vya biashara ni 1074,maeneo ya Shule za  awali 36,maeneo ya wazi 80,maeneo ya masoko 16,maeneo ya Shule za msingi 10,maeneo ya umma ni 33 na maeneo ya Zahanati ni 13.
 
Viwanja vingine anasema kuwa ni  maeneo ya kuegesha magari (Parking) viwanja saba,Maeneo ya Kanisa na misikiti 18,maeneo ya makaburi viwanja 10,Maeneo  ya ujenzi wa nyumba za Serikali 10,Maeneo ya biashara ndogondogo viwanja 6 na maeneo ya viwanja vya michezo 13.
 
Anasema kuwa viwanja vingine ni maeneo ya  vituo vya mafuta 10,maeneo ya hoteli 31,maeneo ya Vituo vya polisi 7,maeneo ya mapumziko matano(5),maeneo ya mpira wa gofu 1,maeneo ya vituo vya afya mawili(2),maeneo ya Hospitali mawili,maeneo ya Mama lishe na Baba lishe moja na  maeneo ya majumuiko ya jamii mawili.
 
‘Kimsingi tumejipanga kuufanya mji hu kuwa wa kuvutia kama ilivyo miji mingine ya wenzetu iliyopo mpakani tuna viwanja vya maeneo ya masoko ya kisasa(Super market) mawili,maeneo ya maduka 9,maeneo ya  Ukumbi mawili na maeneo ya huduma za jamii 106’alisema Ndemfoo.
 
Anafafanua kuwa viwanja vingine ni maseneo ya ujenzi wa Sekondari 12,maeneo ya ujenzi wa Chuo mawili,maeneo ya kutengenezea magari(gereji) mawili,maeneo ya michezo mawili,maeneo ya ujenzi wa majengio ya umma mawili na maeneo ya ujenzi wa nyumba za ibada mawili  na kufanya kuwa jumla viwanja 6354.
MWISHO.