About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Sunday, August 12, 2012

KADA WA CCM APANDISHWA KIZIMBANI KWA TUHUMA ZA UDHALILISHAJI

Na Gideon Mwakanosya,Songea
ALIYEKUWA mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi( CCM) kata ya Bombambili manispaa ya Songea mkoa wa Ruvuma Alfonsi Haule(54) ambaye kwa sasa ni Mwenyekiti wa serikali ya  mtaa wa Sokoine amepandishwa kizimbani kujibu shtaka la udhalilishaji kijinsia.
Mwendesha mashitaka ambaye ni wakili wa serikali kanda ya Songea Juntwa Tulibake mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya mkoa wa Ruvuma Aziza Lutala alidai kuwa Mei mosi mwaka huu majira ya saa za usiku katika eneo la Bombambili wakati wa mkesha wa Mwenge isivyo halali Haule alimdhalilisha kijinsia kigogo mmoja wa Jumuiya ya Umoja wa wanawake Tanzania UWT ambaye jina lake limehifadhiwa(………….).

Wakili Tulibake alifafanua zaidi mahakamani hapo kuwa mshitakiwa Haule alifanya tendo hilo bila ridhaa ya mlalamikaji kitendo ambacho ni kosa kwa mujibu wa kifungu namba 138D(I) ya sheria ya kanuni ya adhabu ya sura namba 16 ya sheria.
Alisema kuwa udhalilishaji uliofanywa na mtuhumiwa anadaiwa kuwa alimvyua nguo za ndani na hijabu kwa lengo la kutaka kumfanyia kitendo cha aibu mlalamikaji .

Hata hivyo wakili Tulibake aliiomba mahakama iangalie uwezekano wa kupanga tarehe nyingine ya kutajwa shauri hilo kwa kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.
Mshitakiwa Haule alikana shitaka na yupo nje kwa dhamana hadi Septemba 10 mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena mahakamani.

Mwisho.