About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Sunday, June 24, 2012

MIAKA 15 JERA KWA KOSA LA KUUA BILA KUKUSUDIA


Na Augustino Chindiye, Tunduru
Mahakama kuu Tanzania kanda ya Songea Mkoani Ruvuma kupitia vikao vinavyofanyika Wilayani Tunduru imemhukumu Said Adam (25) kutumikia kifungo cha miaka 15 baada ya kupatikana na hatia ya kosa dogo la kuua bila kukusudia.

Hukumu hiyo ilitolewa baada ya Adam kukiri kwa hiari yake kufanya kosa hilo kinyume cha Sheria ya kanuni ya adhabu namba 195 pamoja na marekebisho yake ya mwaka 2002 ambapo alidaiwa kumuua
kikongwe marehemu Asha Ramadhani (63)ambaye kifo chake kilisababishwa
na tukio la kumbakwa.

Akitoa hukumu hiyo hakimu mkuu mwenye mamlaka ya Ki Jaji Wilifred Ndyansobera alisema kuwa pamoja na kuzingatia ungamo la mtuhumiwa huyo mahakama yake imemtia hatiani kwa kosa hilo na kwamba adhabu hiyo ni halali ukilinganisha na kosa alilolifanya.
   
Awali akimsomea shitaka Mwanasheria wa Serikali Wilibrod Ndunguru alidai mbele ya mahakama hiyo kuwa Said Adamu kwa kukusudia kinyume cha Sheria ya kanuni ya adhabu namba 196 sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002 alimuua kikongwe huyo katika tukio la ubakaji na  kifo chake July 18/2011 katika tukio lililotokea katika kijiji cha Naleo Wilayani Namtumbo kosa ambalo mtuhumiwa kuyo alilikanusha kuto litenda.

Baada ya mtuhumiwa huyo kukana kufanya kosa hiyo Wakiri wa Utetezi  Dickson Ndunguru aliiomba mahakama hiyo imsomee mteja wake kosa dogo la kuua bila kukusudia endapo upande wa Jamhuri haunge kuwa na pingamizi na ombi hilo na kukubaliwa na kumuomba mteja wake akiri baada ya upande wa Jamhuri kutokuwa na pingamizi katika Shauli namba 4/2012.

Baada ya mtuhumiwa huyo kukiri upande wa Jamhuri unao ongozwa na Wilbroad Ndunguru aliiomba mahakama hiyo impatie adhabu kali kwani kosa alilo litenda ni baya nani la kinyama.

Naye mwanasheri wa Utetezi  Dickson Ndunguru katika hoja zake aliiomba mahakama hiyo impatie adhabu ndogo kwasababu ni mkosaji wa mara ya kwanza,amekiri kosa hilo na kuondolea usumbufu mahakama pamoja na kuokoa muda na kwamba kosa hilo alilifanya kwa bahati mbaya na kujikuta akisuguana na Sheria.
Mwisho