About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Friday, December 2, 2011

WALIPAKODI WATAKIWA KULIPA KWA WAKATI ILI KUKUZA UCHUMI WA NCHI

 Meneja wa TRA mkoa wa Ruvuma Apili Mbaruku

 Meneja Msaidizi wa TRA mkoa wa Ruvuma Novatus Millinga
Afisa elimu huduma kwa Mlipakodi Mkoa wa Ruvuma Jackson Mseti

 Kaimu Mhasibu wa TRA mkoa wa Ruvuma Zahoro Said akiwa na Afisa Manunuzi wa TRA mkoa wa Ruvuma Kasindi Joel wakati wa mkutano wa waandishi wa habari mjini hapa


 Waandishi wa habari wakiendelea kunasa pointi toka kwa Meneja wa TRA mkoa wa Ruvuma Apili Mbaruku

 Mwandishi wa TBC Catherine Nyoni akinasa matukio mbalimbali kwenye mkutano wa waandishi wa habari mkoa wa Ruvuma na Viongozi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) mkoa wa Ruvuma ikiwa ni maadhimisho ya wiki ya mlipa kodi mwaka 2011
 Viongozi wa TRA mkoa wa Ruvuma wakitoa msaada kwa wanafunzi wenye ulemavu wa macho wanaosoma shule maalum ya Mshangano wakati wa wiki ya mlipakodi mwaka 2010
 Wanafunzi wenye ulemavu wa macho wakiwa kwenye picha ya pamoja

Viongozi wa TRA mkoa wa Ruvuma wakiwa kwenye picha ya pamoja na watoto waishio katika mazingira magumu waliopo kwenye kituo cha Kanisa la Matogoro mara baaya ya kupewa msaada wa Mchele,Sabuni,Chumvi,Mafuta ya kupaka na kupikia,miswaki na dawa ya meno wiki ya mlipakodi mwaka 2010
Na Stephano Mango,Songea
WALIPAKODI mkoani Ruvuma wametakiwa kuongeza juhudi ya kulipa kodi kwa wakati ili kuifanya Serikali iweze kujitegemea na kufanikisha kutoa huduma mbalimbali kwa wananchi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo nchini
Akizungumza na Waandishi wa habari jana Ofisini kwake kuhusu wiki ya mlipakodi mkoani Ruvuma Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA)Mkoani Ruvuma Apili Mbaruku alisema kuwa mamlaka ya mapato nchini inathamini na kumtambua mlipakodi kama mhimili wa kukua kwa uchumi kupitia mapato yatokanayo na kodi wanazolipa
Mbaruku alisema kuwa watanzania walio wengi wameendelea kutimiza wajibu wao na kusaidia kukuza uchumi wa taifa na ndio maana TRA kupitia mpango wake wa kimkakati (Corporate Plan)suala la kutoa huduma bora kwa walipakodi linaendelea kupewa kipaumbele
“Mtazamo wetu ni kujenga imani kwa jamii katika kusaidia wafanyabiashara kama wabia muhimu kwa kutoa huduma bora tukitumia mifumo ya kisasa yenye kukidhi matarajio ya wateja wetu ili hatimaye walipe kodi kwa ustawi wa taifa letu”alisema Mbaruku
Alieleza kuwa kwa mwaka wa fedha wa 2010/2011 mkoa wa Ruvuma ulikusanya kodi kwa kiwango cha asilimia 97.27% kodi za ndani na 101.5% kwa kodi ya forodha ambapo kodi za ndani ilipangiwa 4.289.bil=/ na ilikusanya 4.173 bil./= wakati forodha ilipangiwa 4.289.bil/= ilikusanya 178.4m./= lengo halikufanikiwa kwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na makusanyo halisi yalikuwa zaidi ya asilimia 22% ya makusanyo halisi ya mwaka 2009/2010
Alisema kuwa kuanzia disemba 1 hadi 6 ni wiki ya mlipakodi kwa mwaka wa 2011 ambapo kauli mbiu yake ni”Tulipe Kodi Tujitegemee” lengo lake ni kuifahamisha jamii umuhimu wa kulipa kodi ili taifa lijitegemee,kupata mrejesho kutoka kwa walipakodi na wateja wetu ili kuweza kujua huduma zinazotolewa na mamlaka zina ubora wa kiwango kilichojiwekea
Alifafanua kuwa lengo  ni kuwakumbusha walipakodi haki na wajibu wao katika ulipaji wa kodi,kuonyesha uwajibikaji kwa jamii na kwamba katika maadhimisho ya mwaka huu mamlaka inategemea kuendesha semina kwa wanafunzi shule za sekondari,kutoa misaada kwa wahitaji mbalimbali na kutoa vyeti kwa walipakodi bora walioteuliwa kwa vigezo mbalimbali vilivyowekwa kitaifa
MWISHO

DIWANI WA VITI MAALUMU CHADEMA ATOA MSAADA WA MADAWATI SONGEA

      Diwani wa Viti Maalum kupitia tiketi ya Chadema katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea Rhoda Komba 
 Wanafunzi wa darasa la awali katika shule ya Msingi Zimanimoto iliyopo kwenye Kata ya Mfaranyaki Halmashauri ya Manispaa ya Songea wakiwa wamekalia madawati yaliyotolewa na Diwani wa Chadema Rhoda Komba



 Wazazi wa wanafunzi wa darasa la awali wakiwa kwenye viwanja vya shule ya msingi Zimanimoto kwa ajili ya kusherehekea mahafali ya watoto wao na kupokea msaada wa madawati kutoka kwa Diwani wa Chadema Rhoda Komba

Diwani Rhoda Komba akimtunuku cheti cha kuhitimu darasa la awali Juma Abasi
Na Stephano Mango,Songea
DIWANI wa Viti Maalum kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma Rhoda Komba amekabidhi msaada wa madawati 10 yenye thamani ya TSh 450,000 kwa ajili ya darasa la awali katika Shule ya Msingi Zimanimoto
Komba akizungumza wakati wa hafla fupi ya mahafali ya awali katika viwanja vya shule hiyo jana alisema kuwa kuna siku alipita kandokando ya shule hiyo na kuwaona wanafunzi wa darasa la awali wakiwa wamerundikana kwenye darasa moja na kugombania madawati
“Hali ile ilinihudhunisha sana nikaamua kutafuta fedha kwa ajili ya kutengeneza madawati ili nije niwakabidhi kwa lengo la kupunguza idadi ya wanafunzi wanaokaa chini na kukuza malezi ya watoto hao kwa kuwapatia elimu bora”
Alisema kuwa elimu bora kwa mtoto ni nguzo muhimu sana kwa maendeleo ya taifa letu na endapo atalelewa vizuri katika darasa la awali atakuwa amejengeka vyema kitabia na kielimu na kumsababisha kuwa na uwezo anapoingia darasa la kwanza
Aidha Diwani huyo pia ameahidi kumsomesha mtoto aliyehitimu darasa la awali katika mahafari hayo Immakulata Gomela mwenye ulemavu wa ngozi kwa kumpatia sare za shule,madaftari,michango ya shule,viatu na huduma ya afya kuanzia darasa la kwanza hadi darasa la saba
Akizungumza kwenye hafla hiyo Mwalimu wa darasa la awali Joha Tambulu alisema kuwa darasa la awali lina wanafunzi 90 ambao wanakalia madawati tisa na kusababisha adha kubwa ya ufundishaji kwani dawati moja linapaswa likaliwe na wanafunzi watatu lakini wanakaa wanafunzi saba na wengine wanakalia matofali
Tambuli alisema kuwa kwa msaada huu wa madawati  10 kunafanya darasa la awali kuwa na madawati 19 ambayo kwa kiasi kikubwa kumepunguza mlundikana wa wanafunzi kwenye dawati moja na kufanya wanafunzi wengi kushindwa kuandika vizuri na kupelekea kuwa na mwandiko mbaya
MWISHO