About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, February 10, 2014

WAFANYABIASHARA SONGEA WAIGOMEA SERIKALI MASHINE ZA TRA

Na Stephano Mango, Songea.
 
WAFANYABIASHARA   wa maduka mbalimbali katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma wamegomea kufungua maduka  yao  kwa kile kinachodaiwa  kuwa    serikali imeshindwa kuwasikiliza kilio chao cha mashine za kielektroniki   (EFD) ambazo zinatakiwa kwa muda mrefu waliomba zishushwe bei .

Uchunguzi uliofanywa na waandishi wa habari  wa mjini Songea  umebaini kuwa  katika mitaa yote  ya Manispaa ya Songea  maduka yote yamefungwa  na kwamba katika eneo la soko kuu  kwenye vibanda  vinavyolizunguka soko hilo  navyo vimefungwa isipokuwa  wafanya biashara ndogondogo wanaouza mchele, unga , nyanya na mbogamboga ndio wanaoendelea kufanya biashara .

Badhi ya wafanya biashara  waliohojiwa  kuhusiana na mgomo huo walisema kuwa  kwa muda mrefu     waliiomba mamlaka ya mapato Tanzania (TRA)  Mkoa wa Ruvuma  iangalie uwezekano  wa kushusha   bei ya mashine  za kielektroniki  amabazo zimekuwa zikiuzwa kati ya shilling laki sita  na laki nane  jambo ambalo walidai kuwa bei hiyo wafanyabiashara wengi wanashindwa kuimudu .

Walisema kuwa hivi karibuni alifika mijini Songea Naibu Waziri  wa fedha Mwigulu Nchemba na kufanya mkutano mkubwa kati yake na  wafanya biashara  lakini alishindwa kutoa maelezo yakinifu kuhusiana na bei   ambayo imeonekana kuawa ni kandamizi kwa wafanyabiashara hao.

Walifafanua kuwa wafanyabiashara hawagomei kuzinunua mashine hizo isipokuwa wamedai kuwa kwa muda mrefu wamekuwa wakivutana kwa kuitaka serikali iangalie namna ya kuzishusha bei ambayo wafanyabiashara wanaweza kuimudu tofauti na hivi sasa.

 Wameelezakuwa  mawakala wa kuuza mashine hizo mkoani Ruvuma wameteuliwa wachache na kuonekana kuwa kuna viwingu namna ya upatikanaji wa mashine hizo hivyo wameiomba serikali itumie mfumo wa soko huria.

 Kwa upande wake meneja wa mamlaka ya mapato [TRA] mkoani Ruvuma Apili Mbaruku alithibitisha kuwa maduka katika manispaa ya Songea kuwa yamefungwa lakini alieleza kuwa ofisi yake inafanya utaratibu wa kuangalia tatizo jinsi lilivyo.

 Naye katibu mtendaji wa chama cha wafanyabiashara [TCCIA]mkoani Ruvuma ,Moyo akiongea kwa njia ya simu alisema kuwa kuanjia majira ya saa za asubuhi wafanyabiashara kwa pamoja waliamua kufunga maduka yao wakidai kuwa bei za mashine za kielektroniki ni kubwa tofauti na biashara wanazo zifanya lakini kufuatia tukio hilo la mgomo tayari mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu ameitisha kikao kwa mazungumzo zaidi.
 
Hata hivyo mkuu wa mkoa wa Ruvuma Mwambungu akiongea kwa njia ya simu alithibitisha kuwepo kwa mgomo huo na kwamba anatarajia kukutana na wafanyabiashara pamoja na maafisa kutoka mamlaka ya mapato ili kuangalia tatizo hilo.
    MWISHO.