About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Wednesday, October 26, 2011

MHANDISI MANYANYA AANZA ZIARA KWA KUPOKELEWA NA DUA MBALIMBALI KUTOKA KWA WASAIDIZI WA CHIFU WA KINGONI

Wasaidizi wa Chifu wa Kabila la Kingoni (Mjukuu wa Nduna Songea Mbano na Gama) wakitoa dua zao kwa Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Ruvuma na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri ya Makumbusho ya Taifa ya Majimaji alipotembelea Makumbusho ya Taifa ya Majimaji Songea kabla ya kuanza ziara yake ya siku tano mkoani Ruvuma

Wazee wa Ngoma ya Beta wakimpa Nasaha mbalimbali  Mhandisi Manyanya kwa heshima na Mila za Desturi za Kingoni walipomtembelea Ofisini kwake kabla ya kuanza ziara yake

Ndivyo mapokezi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Manyanya alipopokelewa na wakina mama wa BetterLife Tanzania mara alipowasili mjini Songea kabla ya kuanza ziara yake ya siku tano mkoani Ruvuma

MBUNGE STELLA MANYANYA AFANYA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU TANO MKOANI RUVUMA

                                                     Mhandisi Stella Manyanya
Na Mwandishi Wetu,Songea
MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Stella Martin Manyanya ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa anatarajia kuanza ziara ya siku tano mkoani Ruvuma kuwashukuru wapiga kura wanawake na wananchi kwa ujumla wao  kwa kukipa ridhaa chama cha Mapinduzi (CCM)kushika dola
Katika ziara hiyo Octoba 26 Mhandisi Manyanya atafanya mkutano wa hadhara Songea Mjini na Kijiji cha Kitanda Wilayani Namtumbo ambapo atafungua vikundi vya ujasiliamali na kuwahutubia wananchi wa eneo hilo
Octoba 27 atawasili Wilayani Tunduru na kufanya mkutano wa hadhara ambapo Octoba 28 atafanya mkutano Songea Vijijini,Octoba 29 atasalimia Halmashauri kuu ya chama cha Mapinduzi pia atafanya mkutano wa hadhara  kata ya Burma Wilayani Mbinga
Ziara hiyo itakamilika Octoba 30 kwa kufanya mkutano wa hadhara Wilayani Nyasa katika Kata ya Ngumbo na kisha kurejea Mkoani Rukwa kwa shughuli zingine za kiserikali