About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, January 26, 2015

SABABU ZA MWAKYEMBE KUHAMISHWA WIZARA HIZI

WAZIRI HARRISON MWAKYEMBE

Na Mwandishi Wetu
Kwa taarifa zilizopatikana ambazo si rasmi saana ni kwamba mpango mahususi wa kumuondoa waziri Mwakyembe kwenye wizara yake ya uchukuzi na kuhamishiwa kwenye wizara nyingine umepangwa na mtoto wa rais bwana Riziwan si yeye peke yake bali na vigogo wengine wakubwa serikalini na wafanyabiashara wakubwa. 

Kuna ushahidi wa kutosha kuwa Riziwan alimsisitiza baba yake kutomrudisha Mwakyembe kwenye wizara hiyo ya uchukuzi kutokana na waziri huyo kuleta usumbufu kwenye biashara za Riziwan,vigogo na wanafaofanya biashara haramu hapa nchini.Kuna wafanyabiashara wengi walikua hawalipi ushuru walikuja kuanza kulipa baada ya waziri Mwakyembe kukamata wizara hiyo.

Mtoto kwa baba hakui kwa minaji hiyo ni dhahiri kuwa baba kamsikiliza mtoto kwa kufuata matakwa ya mtoto.