About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Sunday, October 2, 2011

UCHAGUZI WA UDIWANI KATA YA MATIMIRA CCM WAIBUKA KIDEDEA

                Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Peramiho Anna Mbogo

Na Mwandishi Wetu,Songea
Mtandao huu wa www.stephanomango.blogspot.com umefanikiwa kupata matokeo ya uchaguzi wa Udiwani Kata ya Matimila Wilaya ya Songea Vijijini ambapo Chama cha Mapinduzi(CCM) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)walisimamisha wagombea
Matokeo ya uchaguzi huo uliofanyika Octoba 2 mwaka huu 2011 ambayo yamethibitishwa na Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Peramiho ambaye pia ni Kaimu Mkurugenzi wa Songea Vijijini Anna Mbogo ni kuwa mgombea wa nafasi hiyo kutoka CHADEMA ,Eleuterius Kasmir Pili amepata kura 923 na mgombea wa CCM ,Menas Cosmas Komba amepata kura 1386
Kwa matokeo hayo,mtandao huu unaungana na wananchi wote wapenda maendeleo kumpongeza mshindi aliyeibuka kidedea katika uchaguzi huo,pia unatoa pole kwa wale wote waliojeruhiwa kwa namna moja au nyingine katika harakati za uchaguzi huo
Mungu awabariki na kuwapa nguvu wale walioumia kutokana na vurugu zilizojitokeza wakati wa kampeni na wakati wa kusubiri majibu
Mtandao huu una laani vikali nguvu za ziada zilizokuwa zinatumika na vyama vyote viwili ambavyo vilisimamisha wagombea katika uchaguzi huo ulioacha majeruhi zaidi ya 12na kusababisha haki za binadamu kuvurugika na kuchafua demokrasia stahiki
Tunaendelea kuwasiliana na Waandishi wengine waliopo kwenye uchaguzi wa udiwani na ubunge huko Igunga ili tuweze kuwajuza habari za matokeo ya uchaguzi katika maeneo hayo
MWISHO

KAMATI YA MAADILI YA CCM MKOA WA RUVUMA YAWAHOJI MADIWANI WATANO KUHUSU SAKATA LA UMEYA

Na, Mwandishi Wetu,Songea

KAMATI ya Maadili ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Ruvuma imewahoji Madiwani watano wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea ambao walituhumiwa na Chama hicho Wilaya ya Songea mjini kuwa wamekisaliti chama kwa kumpigia kura za hapana mgombea Umeya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

Kamati hiyo iliyokuwa na wajumbe Corneus Msuya ambaye ni Mwenyekiti wa Chama hicho Mkoa wa Ruvuma,Emmanuel Mteming'ombe ambaye ni Katibu wa CCM mkoa wa Ruvuma,Henriet Ndimbo ambaye ni Katibu wa Uchumi na Fedha wa chama hicho mkoa, na Mama Litunu iliwahoji Madiwani hao ili kujiridhisha na tuhumu walizotuhumiwa nazo na CCM Wilaya ya Songea Mjini

Madiwani ambao wamehojiwa ni Christian Matembo(SeedFarm) Victor Ngongi(Ruvuma)Kurabest Mgwasa(Msamala) Faustine Mhagama(Mshangano) na Genfrida Haule diwani wa Viti Maalum wa chama hicho

Kwa mujibu wa Katibu wa CCM Mkoa wa Ruvuma Emmanuel Mteming'ombe akizungumza na mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ alisema kuwa kikao hicho cha Maadili kilikuwa kinawapa fursa ya kujitete madiwani walihotuhumiwa

Mteming'ombe alieleza kuwa kimewahoji madiwani hao na chama kimetafakari tuhuma zao na majibu ambayo wamejitetea,baada ya hapo kitatoa onyo kwa madiwani wote akiwemo na Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Dkt Emmanuel Nchimbi kutokana na utomvu wa nidhamu aliouonyesha katika uchaguzi huo wa Umeya wa Songea mjini

Mtandao huu utaendelea kuwajuza wasomaji wake kila kitu kitakachojili bila kumuonea mtu,kumuogopa kwa wadhifa wake ili kuwawezesha wadau wa mtandao huu kujiridhisha na kutafakari viongozi wao waliopewa dhamana na wananchi walivyokuwa na tabia ya uroho wa madaraka kwa faida yao binafsi huku wakiwaacha wananchi wakiwa maskini wa kutupwa