About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Wednesday, August 31, 2011

BIASHARA YA VIUNGO VYA BINADAMU YAHOFIWA KUANZA RUVUMA

                                                     Na Stephano Mango,Songea.

JESHI la polisi mkoani Ruvuma limebaini kuwa mabaki ya mwili wa binadamu yaliyokutwa yamehifadhiwa kwenye mfuko na  kutupwa kati kati ya mto Nakawale wilayani Songea hivi karibuni ulikuwa tayari umeshachunwa ngozi na kuchukuliwa mifupa pamoja na kichwa kitendo kilichofanywa na watu wasiojulikana na kisha kutokomea navyo kusikojulikana.

Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda akizungumza na mtandao wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ alisema kuwa tukio hilo lilitokea Agosti 24 mwaka huu majira ya saa 4 asubuhi katika eneo la Nakawale wilayani Songea ambako Afisa mtendaji wa kijiji hicho alipewa taarifa na wananchi kuwa kuna mwili wa binadamu ukiwa umehifadhiwa kwenye kiloba umeonekana upo kati kati ya mto.
Alisema kuwa Afisa mtendaji huyo ambaye jina lake halikuweza kupatikana baada ya kupata taarifa hiyo alikwenda kwenye eneo la tukio ambako aliwakuta wananchi wamekusanyika kisha alifanya mawasiliano na polisi ambao baadaye walifika kwenye eneo la tukio wakiwa wameongozana na daktari wa serikali kwa ajiri ya uchunguzi.
Aidha alisema kuwa baada ya kufanyika kwa uchunguzi wa mwili huo ilibainika kuwa mwili huo ulikuwa ni wa marehemu Jafar Shabani mkazi wa kijiji hicho huku ukiwa umechunwa ngozi ,mifupa pamoja na kichwa na kubaki nyama na  nguo za marehemu huyo zikiwa kando kando ya mto huo ambazo ndizo zilizopelekea wananchi kugundua kuwa aliyeuawa kuwa ni Shaban.
Kamuhanda ameeleza zaidi kuwa polisi baada ya kufanya uchunguzi zaidi walibaini kuwa siku chache kabla ya tukio hilo marehemu huyo alikuwa amegombana na Said Kandemanje(37) ambaye tayari amekamatwa na anahojiwa na polisi kuhusiana na tukio hilo.
Aidha kamuhanda alisema kuwa uchunguzi uliofanywa unaonyesha kuwepo kwa vitendo vya ufukuaji wa makaburi yaliyoko kwenye vijiji vya nchi jirani ya Msumbiji ambako karibu na mpaka wa Tanzania na kuchukua viungo mbali mbali vya binadamu vinavyodaiwa kupelekwa nchi nyingine kwa uuzaji wa mifupa hiyo ya binadamu.
Alisema kuwa Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wa kina kuhusiana na matukio hayo ili kuweza kubaini mtandao wa watu wanaofanya vitendo hivyo viovu na kuwafikisha kwenye vyombo vya kisheria kwa hatua zaidi
MWISHO

MWANAFUNZI ASAKWA KWA KUMUUA MJOMBA WAKE TUNDURU

Na Gideon Mwakanosya,Songea.

JESHI la polisi mkoani Ruvuma linamsaka mwanafunzi wa darasa la saba katika shule ya msingi Mtonya iliyopo katika Tarafa ya Nakapanya wilayani ya Tunduru mkoani humo kwa tuhuma za kumuua mjomba wake ambaye alikuwa anaenda kumsaidia mama yake ambaye alikuwa anapigwa na kaka yake.
 
Akizungumza mwandishi wa mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ ofisini kwake kamanda wa polisi wa Mkoa wa Ruvuma Bw.Michael Kamuhanda alisema kuwa tukio hilo la mauaji limetokea jana majira ya saa 8 usiku wakati wa ugomvi baina ya marehemu ambaye jina lake ni Michael Gabriel(23) mkazi wa kijiji hicho na dada yake Marisela Jamadin(27).


Kamanda Kamuhanda alisema kuwa inadaiwa siku ya tukio hilo katika kijiji hicho cha Mtonya Gabriel aliuawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani na mtoto wa dada yake huyo Agrey Emmanuel(14) ambaye ni mwanafunzi wa darasa la saba katika shule ya msingi Mtonya wilayani humo na baada ya kugundua kuwa ameua alikimbia na kutokomea kusikojulikana.
Kamanda Kamuhanda alisema kuwa mwanafunzi huyo Agrey anatarajia kufanya mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi  utakaofanyika nchini kote mwezi ujao na hivyo jeshi la polisi mkoani humu linaendelea kumsaka kuhusiana na tuhuma hizo na uchunguzi unaendelea kuhusiana na tukio hilo na hakuna mtu yeyote anayeshikiliwa.
Hata hivyo kamada Kamuhanda alisema kuwa chanzo cha ugomvi huo ambao umepelekea  Gabriel kuhuwawa na mpwa wake bado hakijajulikana licha ya kwamba polisi wanaendelea na uchunguzi.
Mwisho.