About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Saturday, November 26, 2011

WANANCHI WA LITUHI WAANZISHA UMOJA WA KILIMO CHA UMWAGILIAJI

                                 Diwani wa Kata ya Lituhi Adam Mhaiki
Na Gideon Mwakanosya,Nyasa
WANANCHI wa kata ya Lituhi Wilaya ya Nyasa Mkoani Ruvuma wameanzisha umoja wa wakulima wa kilimo cha umwagiliaji ambacho kitaweza kuwakomboa katika kuondokana na njaa na tatizo la umaskini miongoni mwa jamii
Akizungumza na Mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com/  jana Diwani wa Kata ya Lituhu Adam Mhaiki alisema kuwa hatua ya wananchi wa kata hiyo ya kuunda umoja huo imekuja baada ya kuona Serikali kupitia Wizara ya Kilimo na Chakula kuleta ushawishi mkubwa wa kuwa na mradi wa kilimo cha umwagiliaji katika maeneo mbalimbali ya Vijiji vilivyo kandokando y a mto Ruhuhu kwa Wilaya ya Ludewa na Nyasa
Mhaiki alisema kuwa hatua za awali za upimaji wa maeneo ya kilimo cha umwagiliaji tayari zimekwisha fanyika ambapo ukubwa wa eneo hilo lililopimwa ni hekari 2800 na kwamba wakulima waliounda umoja huo ni wa Vijiji vya Mwela Mpya,Nkaya,Kihulu na lituhi
Alieleza kuwa mradi huo ukikamilika unatarajiwa kuongeza uzalishaji wa mazao ya mpunga,mahindi,vitunguu,nyanya na mbongambonga na kwamba kwa sasa jitihada zinafanywa kwa kushirikiana na Serikali ya Wilaya ya Mbinga na Wilaya ya Ludewa Mkoani Iringa ambako kuna wananchi wa kata ya Ngerenge kutafuta fedha ambazo zitaweza kusaidia kujenga miundombinu imara ya kilimo cha umwagiliaji katika maeneo hayo ikiwa ni pamoja na kujenga daraja la kuunganisha wakulima wa wilaya ya Nyasa na Ludewa badala ya kutegemea kivuko kibovu kilichopo eneo la mto Ruhuhu ambacho kwa kipindi cha kiangazi huwa hakifanyi kazi kutokana na uhaba wa maji
Alieleza zaidi kuwa pia mradi huo ukikamilika utaweza kuinua hali za maisha za wananchi wa vijiji hivyo na taifa kwa ujumla kwa kupunguza umaskini wa kipato na njaa kwenye kaya nyingi katika maeneo hayo kwani kwa muda mrefu wananchi wa kata hizo wamekuwa wakitegemea kilimo cha mihogo na shughuli za uvuvi kwa kutumia vitendea kazi duni
Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Mbinga Magharibi Kapteni John Komba aliiomba Serikali kupitia Wizara ya Kilimo na Chakula kuhakikisha mradi huo mkubwa unakamilika mapema ili kuondoa kero kubwa ya wananchi wa maeneo hayo
Komba alisema wananchi wamehamasika kujiunga kwenye umoja wa wakulima ili waweze kupata nguvu ya pamoja ya mikopo na misaada kutoka kwenye mfuko wa jimbo ambao kazi yake kubwa ni kuwasaidia wananchi kwenye vikundi vya ujasiliamali ili waweze kupata ustawi katika maisha yao
Mwisho

RAIS KIKWETE ACHANGIA MILIONI 3 UJENZI WA HOSTELI YA WASICHANA WILAYANI NYASA

                             
                                                           Rais Jakaya Kikwete
                                                          RC Ruvuma Said Mwambungu
                                     DC Mbinga Kanali Edmund Mjengwa
             Mbunge Mbinga Magharibi Kapteni John Komba
Na Stephano Mango,Nyasa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete amechangia shilingi milioni tatu katika kusaidia ujenzi wa hosteli ya wasichana katika shule ya Sekondari ya Lituhu iliopo katika wilaya mpya ya Nyasa mkoani Ruvuma ili kukomesha utoro na mimba kwa wasichana wa shule hiyo
Akizungumza na Mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ Ofisini kwake Mkuu wa Shule ya Sekondari ya kutwa ya Lituhi Benjamin Mwingira alisema kuwa wananchi wa kaya ya Lituhu wakiwemo wazazi wa watoto wanaosoma katika shule hiyo kwa pamoja wameridhia mpango wa ujenzi wa Hosteli ya wasichana ambayo itaweza kuwasaidia wanafunzi wa kike kuondokana na tatizo sugu la utoro na upatikanaji wa mimba
Mwingira alisema kuwa kwa sasa wananchi hao tayari wamefyatua na kuchoma tofari laki sita zitakzotumika kwenye ujenzi huo ambapo kazi iliyobaki ni kuanza kujenga Hosteli hiyo kwa kasi kubwa mara baada ya mvua kusimama kunyesha
Amewahimiza wazazi kuthamini michango iliyotolewa na Rais Jakaya Kikwete,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu,Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Kanali Mstaafu Edmund Mjengwa na Mbunge wa Jimbo la Mbinga Magharibi Kapteni Mstaafu John Komba kwa kuhakikisha kuwa jingo hilo la Hosteli kwa wasichana linakamilika kwa wakati ili wanafunzi  wa kike 200 kati ya wanafunzi  403 wa shule hiyo waweze kulitumia
Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Mbinga Magharibi Kapteni Mstaafu John Komba alisema ametoa bati 50 na michango midogomidogo kwa ajili ya kuezekea hosteri hiyo na pia amewashukuru Rais Kikwete kwa kuwachangia shilingi milioni tatu,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu kwa kutoa mifuko 50 ya saruji na Mkuu wa Wilaya ya Mbinga ametoa mifuko 10 ya saruji
Komba aliwaomba wananchi wa kata ya Lituhi na wananchi waliopo nje ya kata ya Lituhi wakiwemo waliowahi kusoma shule hiyo kuona umuhimu wa kuchangia ujenzi huo ambao unaboresha miondombinu ya shule hiyo na kupelekea utolewaji wa elimu bora
MWISHO

ASASI YA ROA YAFANIKIWA KUHUDUMIA WAGONJWA 489 SONGEA

                    Mwenyekiti wa ROA Methew Ngarimanayo
Na Stephano Mango,Songea

SHIRIKA lisilo la Kiserikali la Ruvuma Orphans Association (ROA) katika kipindi cha Julai hadi Septemba mwaka huu kwa kushirikiana na timu ya watoa huduma kwa wagonjwa majumbani limefanikiwa kuwatambua wagonjwa 516 kati ya hao wagonjwa 489 wamepatiwa huduma na wagonjwa 268 wanaendelea kupata huduma katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea na Halmashauri ya Wilaya ya Songea.

Hayo yamesemwa jana na Mwenyekiti wa Shirika hilo  Mathew Ngalimanayo wakati akizungumza na Mtandao huu wa www.stephanomango.blogspot.com  jana ofisini kwake mjini Songea.

Amefafanua zaidi kuwa Shirika hilo lisilo la Kiserikali la Roa lilianzishwa tangu Aprili mwaka 1999 na kusajiliwa rasmi Aprili 6 mwaka 2001 na kwamba lengo kubwa la kuanzishwa kwa Shirika hilo ni kushughulikia changamoto wanazokabiliana nazo watoto yatima na watoto waishio katika mazingira hatarishi.

Amebainisha zaidi kuwa Shirika hilo pia lilianzishwa kushughulikia changamoto ziletwazo na ugonjwa hatari wa Ukimwi katika jamii  kwa kushirikiana na Serikali,na wadau wengine wa Maendeleo.

Ameeleza zaidi kuwa shirika lake limetoa huduma kwa wgaonjwa wa muda mrefu majumbani katika Kata 15 zilizopo katika Manispaa ya Songea na Halmashauri ya Wilaya ya Songea na kwamba kwa kushirikiana na Shirika lisilo la Kiserikali la The foundation for civil society la Jijini Dar es Saam limefanikiwa kuhamasisha mitaa na kata katika Manispaa ya Songea na Halmashauri ya Wilaya ya Songea kufungua na kuiendesha mifuko ya kusaidia watoto yatima na watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi.

Ngalimanayo amesema kuwa Shirika hilo lisilo la Kiserikali la Roa pia limefanikiwa kuwahudumia wagonjwa 489 kati ya wagonjwa 516 waliotambuliwa ambapo wagonjwa 29 wamepata nguvu na wanaendelea vizuri na shughuli zao za kila siku na wagonjwa 268 wanaendelea kuhudumiwa majumbani na pia Roa imefanikiwa kuwapatia huduma watoto yatima 234 walioko katika mfumo wa Elimu.

Amesema kuwa pia wamefanikiwa kuwakumbusha wananchi juu ya wajibu wao wa kimsingi wa ulinzi,matunzo na malezi ya watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi kwa kila mtaa kuwa na kamati ya kuratibu na kusimamia masuala ya watoto wanoishi katika mazingira hatarishi na kuanzisha mfuko maalumu wa kila mtaa wa kuhudumia watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi na watu wa makundi mbalimbali katika kata hizo wamehamasishwa juu ya masuala ya Vvu/ Ukimwi na kuendesha zoezi la upimaji Vvu/Ukimwi kwa hiyari.

Ametaja changamoto wanazokutana nazo kuwa ni ukosefu wa fedha za kutosha wa kuendeshea shughuli za shirika hilo kadiri ya malengo na mipango iliyopo,mwitiko hasi wa baadhi ya wananchi na watendaji wa Serikali kuhusu dhana ya mifuko ya kusaidia watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi.

Ameitaja mipango ya shirika hilo ya baadaye kuwa ni kuendelea kuelimisha na kuhamasisha wananchi kuanzisha mifuko ya jamii ya kusaidia watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi,kugharamia gharama za masomo kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu kwa kuwapatia karo,sare za shule,vifaa vya darasani na gharama zingine zinazohusiana na masuala ya elimu na kujenga uelewa kwa jamii juu ya haki na wajibu wa watoto yatima na watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi.

MWISHO