About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, August 16, 2012

KADA WA CCM RUVUMA AKUTWA CHOONI GESTI AKIWA AMEKUFA



Na Stephano Mango, Songea

MJUMBE wa Kamati ya Utendaji wa Jumuiya ya wanawake Tanzania(Uwt) Mkoani Ruvuma Amina Chimata (55) mkazi wa mjini Tunduru amefariki dunia akiwa chooni kwenye nyumba ya kulala wageni ya Tulia iliyopo karibu na kituo cha mabasi Songea

Habari zilizopatikana jana mjini hapa ambazo zimethibitishwa na Katibu wa Chama cha Mapinduzi (Ccm) Mkoa wa Ruvuma Verena Shumbusho zimesema kuwa tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa za asubuhi wakati Chimata alipokuwa akijiandaa kwenda kuhudhuria kikao cha Kamati ya Siasa ya chama hicho mkoa
Shumbusho alifafanua kuwa baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Siasa mkoa walikuwa tayari wameshafika kwenye eneo la Ccm Mkoa kwa ajiri ya kuanza kikao hicho na ghafla mmoja wa wajumbe alipigiwa simu toka kwa muhudumu wa nyumba ya kulala wageni ya Tulia kuwa aende haraka kwenye nyumba hiyo kwani Chimata tangu alivyoingia bafuni na baadae aliingia chooni kwenda kujisaidi hajatoka kwa muda mrefu

Alifafanua zaidi kuwa baada ya mjumbe huyo kupokea taarifa hiyo aliwasiliana na viongozi wa Ccm Mkoa kisha walikwenda kwenye eneo la tukio ambako walikuta mlango wa choo hicho ukiwa umevunjwa na Chimata akiwa amelala kwenye sakafu ya choo hicho huku Polisi wakiwa tayari wameshaanza kufanya uchunguzi kuhusiana na tukio hilo ambapo mwili wa Chimata ulichukuliwa na kupelekwa kwenye Hospital ya Serikali ya Mkoa wa Songea kwa ajiri ya uchunguzi zaidi ambako ilithibitika kuwa Chimata alikuwa tayari amefariki dunia kwa ugonjwa wa shinikizo la damu na kisukari
Alisema kuwa kutokana hilo kikao cha Kamati ya Siasa ya Mkoa na badala yake wajumbe walikutana wakiwa na huzuni ili kuweza kupanga kuusafirisha mwili wa marehemu kwa mazishi

Kwa upande wake Katibu wa Uwt mkoa wa Ruvuma Mariam Yusuph alipoulizwa kuhusiana na tukio hilo alisema kuwa Uwt Mkoa wa Ruvuma na Taifa kiujumla imepata pigo kubwa sana kutokana na kuondokewa na kiongozi huyo ambaye alikuwa ni msaada mkubwa sana kwenye jumuiya na chama kwa ujumla

Naye Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Deusdedit Nsimeki alithibitisha kutokea kwa tukio hilo ambalo alidai kuwa lilitokea agosti 15 mwaka huu majira ya saa 4:30 asubuhi katika nyumba ya kulala wageni ya Tulia na uchunguzi wa awali umebainisha kuwa Chimata katika uahi wake alikuwa anasumbuliwa na magonjwa ya kisukari na shinikizo la damu kwani baada ya tukio hilo kutokea alikutwa akiwa amehifadhi dawa ya magonjwa hayo kwenye mfuko wake
MWISHO