About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Sunday, September 16, 2012

WANANCHI WAONYESHWA VIWANJA VYAO VILIVYOPIMWA NA KAMPUNI YA ARDHI PLAN

Maafisa wa Kampuni ya Ardhi Plan wakiwa kwenye eneo la ugawaji wa viwanja katika mchoro namba 8 kwenye mtaa wa Namanyigu, wa kwanza kushoto ni Gordwin Pambila na George Kimwaga


Aliyevaa miwani na kofia ni Afisa wa Kampuni ya Ardhi Plan George Kimwaga akitoa maelekezo kwa kutumia ramani kwa wananchi ambao wamemzunguka ili kuweka sawa kumbukumbu za ardhi
Kijana wa Kampuni ya Ardhi Plan akiwa amevaa kizibao chenye nembo ya Kampuni hiyo

Baadhi ya wananchi wakiwa na viongozi wa kamati ya upimaji wakiangalia maeneo husika


Baadhi ya wananchi wakiwa na viongozi wa kamati ya upimaji wakiangalia maeneo husika


Na Stephano Mango, Songea

WANANCHI wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma ambao wamepimiwa ardhi yao katika Kata ya Mshangano kwa kutumia Kampuni ya Ardhi Plan wamefurahishwa kukamilika kwa mradi huo wa viwanja elfu 18,000 ulioanza mwaka 2011 na kukamilika septemba mwaka huu

Akizungumza kwa niaba ya kamati ya ugawaji wa viwanja iliyochaguliwa na wananchi wenye maeneo katika Kata ya Mshangano kwenye eneo la ugawaji jana Telesia Komba alisema kuwa kitendo kilichofanywa na Kampuni hiyo ni cha kiungwana sana kwani wameheshimu makubaliano yaliyofikiwa kwenye mkutano wa mwaka jana wakati mradi unaanza

Komba alisema kuwa makubaliano yaliyofikiwa wakati huo kwenye mkutano mkuu wa kata wa kata hiyo kati ya Kampuni, wananchi na viongozi wa Serikali yalikuwa ni kwamba gharama za mradi huo zinatolewa na wananchi wenyewe kwa kutoa ardhi badala ya kusubiri Serikali mpaka ipate uwezo wa kifedha ambapo kwa wale wenye maeneo madogo yaani kiwanja kimoja mpaka viwili wanatozwa gharama ya fedha shilingi laki moja (100,000/=) kwa kiwanja kimoja na laki mbili (200,000) kwa viwanja viwili kama gharama za upimaji na kwa wale wenye viwanja 5 basi viwili wanaipa Kampuni

Alisema kuwa kwa wale ambao wanachelewa kutimiza wajibu wao wa kulipia gharama za upimaji hawataonyeshwa mipaka ya maeneo ya ardhi yao na kukosa nyaraka zitakazowafanya wawe wamiliki halali wa viwanja hivyo mpaka pale watakapotekeleza makubaliano

Alifafanua kuwa wananchi ambao wametimiza makubaliano husika wanaendelea kuonyeshwa maeneo yao ili waweze kuyamiliki kisheria na kuyafanyia shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii kadri ya mipango yao wenyewe

Akizungumza kwenye mkutano huo Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Namanyigu Fidolin Malindisa alisema kuwa wananchi wanapaswa kuheshimu makubaliano yaliyofikiwa ili Kampuni ipate haki yake kwa sababu tayari imeshatimiza wajibu wake wa msingi

Malindisa alisema kuwa kukamilika kwa mradi huo kutawapa fursa wananchi kuweza kuishi kwenye maeneo yaliyopimwa, pia watatumia maeneo hayo kwa kupata mkopo na kuendesha miradi mbalimbali ya kiuchumi ikiwa ni pamoja na kusomesha watoto

Naye Afisa kutoka Kampuni ya Ardhi Plan Gordwin Pambila alisema kuwa Kampuni imeanza kuwaonyesha wananchi viwanja katika mtaa wa Namanyigu ambako kuna madeni madogo ya fedha za gharama za upimaji ambazo zinadaiwa kutoka kwa wananchi

Pambila alisema kuwa wananchi wengi hawajatimiza makubaliano ya kulipia gharama za upimaji hivyo ndio wanaochelewesha ukamilishaji wa mradi huo na kuifanya Kampuni itumie muda mwingi na rasilimali nyingi kuwakumbusha kulipia maeneo hayo
MWISHO