About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, August 29, 2011

KAMANDA WA POLISI MKOA WA RUVUMA MICHAEL KAMUHANDA

                                                
                                                   Na Cresencia Kapinga,Songea
WATU sita wamefariki dunia papo hapo na wengine wawili wamejeruhiwa vibaya baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupinduka na kuwaka moto katika kijiji cha Chunya kilichopo wilayani Mbinga mkoani Ruvuma.
 
Kamanda wa polisi mkoa wa Ruvuma Machael Kamuhanda akizungumza na mtandao wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ alisema kuwa tukio hilo limetokea jana majira ya saa 12 jioni na kwamba miongoni mwa waliofariki miili yao imeuungua vibaya huku maiti hizo zikiwa hazitambuliki.
 
 Kamuhanda alisema kuwa tukio hilo limehusisha Gari lenye  namba za usajili  T 270 BDG Landrover likiwa linaendeshwa na Dereva Stevin Ngoko (32) kupinduka na kuwaka moto na kusababisha vifo vya watu sita papo hapo katika kiji cha Chunya barabara iendayo Mbambabay toka Mbinga.
 
Kamuhanda amewataja waliojeruhiwa katika ajari hiyo kuwa ni Jeremia Masalo (38) mkazi wa nchi jirani ya Msumbiji na Anna Godfrey (3) mkazi wa Mbambabay ambao wote wamelazwa katika Hospitali ya Serikali ya Wilaya ya Mbinga kwa matibabu.
 
Alisema kuwa watu waliokufa majina yao hayajaweza kufahamika kutokana na maiti hizo kutotambulika kwa kuwa zimeungua vibaya na zote zimepelekwa  katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya wilaya hiyo.
 
Kamuhanda alisema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi ambao ulimsababishia dereva wa gari hilo kushindwa kumudu usukani na kwamba jeshi lake linaendesha msako wa kumtafuta  dereva wa gari hilo Bw. Ngoko ambaye alitoroka mara tu baada ya kutokea ajali hiyo.