About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Friday, September 23, 2011

BAADA YA UBAKAJI WA DEMOKRASIA YA UCHAGUZI WA UMEYA MAPAMBANO YANAENDELEA MIONGONI MWA MADIWANI

 Joseph Fuime ambaye ni Diwani wa Kata ya Mjini akiongoza mapambano ya kurudisha demokrasia mikononi mwa wapiga kura
 Sanduku la kura lalejeshwa meza kuu baada ya kurejeshwa toka mikononi mwa watu wasiopenda demokrasia
 Madiwani waendelea kutaharuki tukio la kihistoria la uchaguzi wa kuziba nafasi iliyoachwa wazi na marehemu Ally Said Manya

Wananchi wakiwatathimini kwa umakini mkubwa wawakilishi wao walipokuwa wanachapana makonde katika ukumbi wa Saccos wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

VULUGU,TIMBWILI LAANZA BAADA YA NAIBU MSTAHIKI MEYA MARIAM DIZUMBA KUTANGAZA MATOKEO YA UCHAGUZI WA UMEYA

 Naibu Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Mariam Dizumba akitangaza matokeo ya uchaguzi huo
 Kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Dkt John Nchimbi akiwatuliza Madiwani ambao walikuwa wakimzomea Mstahiki Meya aliyevaa Joho nyekundu Charles Mhagama na kuambiwa kuwa amechakachua matokeo na hivyo hawamtambui
 Viongozi hao wakiteta jambo baada ya kunusa harufu ya kushtukiwa mchezo wao walioufanya
 Madiwani wakianza kurushiana maneno yaliyokosa staha na kupelekea vurugu kuanza ndani ya kikao cha baraza la Madiwani
Hapa sasa ni ubabe wa kuzuia sanduku la kura lisitolewe ndani ya ukumbi wa uchaguzi ili zihesabiwe tena na madiwani waweze kujiridhisha kuhusu matokeo ya kura walizozipiga

KURA ZAENDELEA KUHESABIWA NA WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI

 Wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi Jimbo la Songea Mjini wakiendelea kuhesabu kura zitakazo mkubali au kumkataa mgombea Umeya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Charles Mhagama
Wa kwanza kutoka kushoto ni Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Manispaa ya Songea Naftan Saiyoloi akiwa na Mweka hazina wa Halmashauri hiyo Kessy Mpakata

MADIWANI WAENDELEA KUPIGA KURA HUKU UTULIVU UKIWA WA KUTOSHA AMBAKO HAKI NA WAJIBU WA MPIGAJI KURA UKIENDELEA

 Mgombea Umeya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea ambaye ni Diwani wa Kata ya Matogoro akitoka kupiga kura katika uchaguzi huo
 Diwani wa Kata ya Mateka Maricelino Mapunda akitumia vyema haki yake ya kumchagua Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

 Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Dkt Emmanuel John Nchimbi ambaye pia ni Waziri wa Habari,Utamaduni na Michezo akipiga kura wakati wa zoezi hilo la upigaji kura
Madiwani wakitafakari wakati wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi huo wakihesabu kura

UCHAGUZI WA UMEYA MANISPAA YA SONGEA NI VITUKO VILIVYOSHEHENI AIBU MBELE YA MBUNGE DKT NCHIMBI

 Diwani wa Kata ya Matogoro Charles Mhagama ambaye ni mgombea Umeya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea akifuatilia kwa umakini mkubwa kanuni za uchaguzi wa nafasi hiyo kutoka kwa msimamizi wa uchaguzi huo
 Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Dkt Emmanuel Nchimbi akiwasalimia madiwani kwenye mkutano huo wa uchaguzi wa nafasi wazi ya Umeya
 Msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Songea Mjini Nachoa Zakaria ambaye pia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea akionyesha wajumbe sanduku la kupigia kura katika uchaguzi huo uliofanyika leo
                                    
 Kutoka kulia ni Msimamizi wa uchaguzi Nachoa Zakaria akihakikisha majina ya wajumbe watakaopiga kura,kushoto ni Naibu Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Mariam Dizumba
 Hapa ni dua kwanza,ndivyo alivyoanza Diwani wa Kata ya Misufini Salum Mfamaji,akiwa diwani wa kwanza kupiga kura katika uchaguzi huo

MADIWANI WAVUTANA ZAIDI YA DAKIKA 10 UCHAGUZI WA UMEYA MANISPAA YA SONGEA

 Kutoka kushoto ni Diwani wa Viti Maalum(CCM) Rehema Millinga,Rhoda Komba (CHADEMA)Christian Matembo wa kata ya Seedfarm
 Kutoka kushoto ni Madiwani wa CCM,Willon Kapinga kata ya NdilimaLitembo,James Makene kata ya Matarawe,Gerald Ndimbo kata ya Ruhuwiko

 Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo Dkt Emmanuel Nchimbi ambaye pia ni Mbunge wa Songea Mjini
Mkurugenzi wa Halmashauri Manispaa ya Songea Zakalia Nachoa