About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Sunday, March 2, 2014

FUIME ATANGAZA NIA YA UBUNGE 2015 JIMBO LA SONGEA MJINI KUPITIA CHADEMA


MWENYEKITI WA CHADEMA RUVUMA AMTIMULIA VUMBI DKT NCHIMBI



 MTANGAZA NIA YA UBUNGE JIMBO LA SONGEA MJINI JOSEPH FUIME AKIHUTUBIA MOJA YA MIKUTANO YAKE
MAMIA YA WAKAZI WAKIMSIKILIZA MTANGA NIA YA KUGOMBEA UBUNGE KATIKA KATA YA LIZABONI

Na Stephano Mango, Songea


MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoa wa Ruvuma Joseph  Lusius Fuime ametangaza nia ya  kugombea Ubunge kwa tiketi ya Chama hicho katika Jimbo la uchaguzi la Songea mjini ifikapo mwaka 2015 katika kinyang’anyiro cha uchaguzi mkuu

Fuime  ambaye Diwani wa Kata ya Mjini katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea akitangaza nia hiyo  jana ya kutaka kugombea jimbo ambalo kwa sasalinaongozwa na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt Emmanuel Nchimbi  kwenye mkutano wa hazara uliofanyika kwenye viwanja vya Soko kuu la Songea Mjini alisema kuwa ametafakari kwa muda mrefu pia ameombwa na makundi mbalimbali ya jamii ya Songea kuchukua fomu ya kugombea kiti hicho


Alisema kuwa baada ya kutafakari ameamua kwa dhati kusikiliza kilio cha makundi hayo na kugombea ubunge kwa tiketi ya CHADEMA  ili kwa pamoja kuweza kuondoa kero mbalimbali ambazo zinawasumbua wakazi hao


“Naomba niwaondoe hofu wanachama wenzangu ndani ya Chadema kuwa kutangaza kwangu nia  ya kutaka kugombea Ubunge hakuna maana kuwa wanachama wengine wanaotaka kugombea washindwe kutangaza nia ya kuwania nafasi hiyo”


Alisema kuwa wanachama ndio wenyewe  mamlaka ya kumchagua mgombea mwenye kujua matatizo ya wakazi wa Manispaa ya Songea na mbinu ya kushirikiana na wananchi hao kuweza kuyatatua kwa maslahi mapana ya ustawi wa jamii hiyo, pia atakayeweza kupambana na mgombea wa Ubunge kwa tiketi ya ccm.


Alieleza zaidi kuwa baada ya kufikia uamuzi huo kabla ya kutangaza nia aliamua kukaa na wazee wote wa Songea Mjini ambao wote kwa pamoja wameonyesha ushirikiano mkubwa na wamemwakikishia kuwa mwaka 2015 wakati wa uchaguzi watamuunga mkono kama walivyomuomba


Fuime ambaye pia ni Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Ccm katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea alijigamba na kuwaeleza wakazi wa Songea kuwa yeye ndiye anayefaa kupambana na Mbunge wa Songea Mjini kwa tiketi ya Ccm  Dkt Emmanuel Nchimbi.


Alifafanua zaidi kuwa Chadema imejipanga kwa dhati kutotoa nafasi tena ya uongozi kwenye Jimbo la uchaguzi la Songea Mjini kuchukuliwa na Ccm ambalo lina kata 21 na kati ya hizo 8 zinaongozwa na Madiwani wa Chama cha Chadema na kwamba mwaka 2015 kata zilizobaki zitanyang’anywa na Chadema.


Aliongeza kusema kuwa dawa ya kupambana na manyang’au waliomo ndani ya Ccm ni kujipanga na kuwabana kwa kutowapa nafasi ya aina yeyote kuanzia sasa na mpaka ifikapo 2015 kwani hivi sasa miradi mbalimbali katika Halmashauri ya Manispa ya Songea imekuwa ikijengwa chini ya viwango ambapo alitoa mfano kuwa miundombinu ya barabara, ujenzi wa vyumba vya madarasa na ofisi zimekuwa zikijengwa chini ya viwango huku manyang’au wa Ccm wakineemeka.


Alisema kuwa Wananchi wa Songea ambao wamekuwa wakikabiliwa na shida mbalimbali kutokana na ombwe la uongozi unaotokana na mfumo mbovu wa Ccm wana kila sababu ya kuunga mkono wazo lake la kuwania kiti cha Ubunge ili kuweza kufanikisha ustawi bora wa maisha ya wakazi wote kwa ushirikiano


Awali katika vipindi viwili vya uchaguzi mkuu vilivyopita Chama cha Demokrasia na Maendeleo kilikuwa kinamnadi Wakiri wa kujitegemea Edson Osward Mbogoro kugombea nafasi hiyo ambapo alikuwa akibwagwa na Mgombea wa Ccm  Dkt Emmanuel Nchimbi  ambaye ndiye Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini hadi sasa.


MWISHO