About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, September 12, 2011

MAELFU YA WAKAZI WA TUNDURU WAJITOKEZA KUMZIKA MWENYEKITI WA TLP TUNDURU RAJABU MNYACHI

                             Na  Steven  Auguastino, Tunduru
 
MAELFU ya wakazi wa mji wa Tunduru wamejitokeza kumzika aliyekuwa Mwenyekiti wa chama cha Tanzania Labour Party (TLP) Wilaya ya Tunduru Rajab Mohamed Mnyachi aliyefariki Dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu na kulazwa katika hospitali ya serikali ya wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma.
 
Msemaji wa familia ya Marehemu Mnyachi Bw. Shaibu Namkumbe akizungumza na mtandao wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ alisema kuwa marehemu Mnyachi alikuwa anasumbuliwa na  maradhi ya shinikizo la damu.
 
Akifafanua wasia wa marehemu mnyachi Bw. Namkumbe alisema kuwa kipindi cha uhai wake alijishikisha na alikuwa mkereketwa wa mageuzi kupitia vyama ya siasa pamoja na kugombea nyadhifa mbali mbali.
 
Alisema mwaka 1986 hadi 1999 marehemu  Mnyachi alikuwa mwenyekiti wa Chama cha NCCR Mageuzi na aligombea katika kinyang`anyiro cha Ubunge wa jimbo la Tunduru akiwa anapambana na marehemu Juma jamardini Akukweti wa CCM katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 1995.
 
Taarifa hiyo iliendelea kueleza kuwa Mwaka 1999 marehemu alikihama chama cha NCCR Mageuzi na kujiunga na TLP ambako pia alichaguliwa kuwa mwenyekiti wake hadi umauti ulipo mkuta Septemba 9 mwaka huu.
 
Akiwa katika chama hicho pia marehemu alitoa hamasa kubwa na kukifanya chama hicho kupata wanachama wengi na kugombea katika vinyang`anyiro vya Ubunge katika chaguzi za mwaka 2000, 2005 na uchaguzi mdogo wa kuziba pengo la marehemu Akukweti mwaka 2007.
 
Wakiongea kwa nyakati tofauti baadhi ya wananchi wanaomfahamu Marehemu Mnyachi, katibu wa Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kusini Bw. Maulidi Kalambo (Yakanungu) na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Wilaya ya Tunduru Bw. Maurid Said mbali na kukiri kuwa Marehemu alikuwa mahiri katika medani za siasa na kuongeza kuwa sasa Tunduru imeishiwa watu wenye vipaji.
 
Katika maelezo yao viongozi hao walisema kuwa Marehemu mnyachi, marehemu  Mazee Rajab wa CUF pamoja na Simbili Makanyaga wa UDP aliyehamia jijini Dar es salaam baada ya kuchaguliwa kuwa katibu Mwenezi wa Chama hicho Taifa walikuwa ni hazina kubwa na kwamba sasa Wilaya ya Tunduru inategemea majaliwa ya mungu kupata vijana wenye kipaji na watakao kubalika katika kuleta changamoto za maendeleo vinginevyo CCM itaendelea kushika hatamu.
 
Mwisho.   

ASKARI WANYAPORI AKUTWA AMEUWA NA WATU WASIOFAHAMIKA

                                               Na Gideon Mwakanosya,Songea.
ASKARI wa idara  ya wanyamapori Nchini  Msumbiji  Babu Abdalah (35) amekutwa akiwa ameuwawa kwa kupigwa na kitu chenye ncha kali sehemu za kifuani na watu wasiofahamika huko katika  kijiji cha Chikomo wilayani Tunduru Mkoa wa Ruvuma.
Akizungumza na Mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com/ ofisini kwake jana kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda alisema kuwa tukio hilo limetokea Septemba 10 mwaka huu majira ya saa 9 alasiri huko katika kijiji cha Chikomo.
Alisema kuwa siku hiyo ya tukio inadaiwa kuwa afisa mtendaji  wa kijiji hicho Ally Mtukusye alipatiwa taarifa ya tukio hilo kasha aliwasiliana na polisi wa kituo kikuu cha Tunduru ambao walifika kwenye eneo la tukio wakiwa wameongozana na mganga ambaye ndiye aliyethibitisha kuwa askari huyo wa idara ya maliasili toka Nchi ya Msumbiji amekufa kutokana na kipigo.
Kamuhanda alisema kuwa  Askari huyo alikutwa akiwa na majeraha makubwa sehemu za usoni upande wa kushoto na kifuani upande wa kushoto ambayo  ndio yalimsababishia  kuvuja kwa damu nyingi atimaye kufariki dunia.
 Hata hivyo kamanda Kamuhanda alisema kuwa kufuatia tukio hilo hakuna aliyekamatwa au kutiliwa mashaka na chanzo bado kinaendelea kuchunguzwa.
MWISHO.

WANNE WASHIKILIWA NA POLISI RUVUMA KWA TUHUMA ZA MAUAJI WILAYANI TUNDURU

                                        Na Gideon Mwakanosya,Songea.
JESHI la Polisi mkoani Ruvuma linawashikilia watu wanne wakazi wa kijiji cha kitanda wilayani Tunduru kwa tuhuma za kumpiga na kitu chenye ncha kali sehemu mbambali za uso na kumsababishia kifo mwanamke mwenye umri wa miaka 60 mkazi wa kijiji hicho.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma  Michael Kamuhanda akizungumza na mwandishi wa mtandao wa http://www.stephanomango.blogspot.com/, Gideon Mwakanosya kutoka mjini Songea, alisema kuwa tukio hilo limetokea septemba 10 mwaka huu mwajira ya saa 2.00 usiku huko katika kijiji cha kitanda kilichopo wilayani Tunduru.
Kamuhanda amemtaja aliyeuwawa kuwa ni Mwanahawa Landi (60) mkazi wa kijiji hicho na amewataja wanaoshikiliwa na polisi kuhusiana na tuhuma za mauaji hayo kuwa ni Mohamed Saidi (25), Kassim Said (39), Said Baina (76) na Ally Said (37) wote wakazi wa kijiji cha kitanda.
Alifafanuwa zaidi  kuwa inadaiwa kuwa siku hiyo ya tukio Mohamed Issa (70) alitoa taarifa kwenye kituo cha polisi cha Tunduru kuwa Mwanahawa ameuwawa kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali usoni na ambayo yalimsababishia sura yake kuharibika kabisa na watu wasiofahamika.
Kamanda Kamuhanda alisema kuwa chanzo cha mauaji hayo bado kinachunguzwa lakini tayari watu wanne polisi imewatia mbaroni kwa mahojiano zaidi na kwamba uchunguzi utakapokamilika watuhumiwa watafikishwa mahakamani ili kujibu tuhuma za mauaji.
MWISHO.

NIMESAFIRI KIKAZI WAPENZI WASOMAJI WA MTANDAO HUU

Stephano Mango
Mmiliki wa mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com/, ambaye ni ndugu Stephano Mango amesafiri kikazi toka Songea mpaka Jijini Dar Es Salaam, ambapo ameungana na wanaharakati wengine nchini na nchi jilani kwa ajili ya kuhudhuria Tamasha la Jinsia Tanzania ambalo linaanza kufanyika kesho Septemba 13-16 mwaka huu 2011

Katika Tamasha hilo Mada mbalimbali zitawasilishwa na wanaharakati na wasomi waliobobea katika utetezi wa masuala ya jinsia na haki za binadam, kwa mwaka huu Mada itakuwa ni ,"Ardhi,Nguvu Kazi na Maisha Endelevu" chini ya Kampeni kubwa ya "Haki ya Uchumi:Rasilimali ziwanufaishe Wanawake Walioko Pembezoni.

Hivyo,ndugu wasomaji jiandaeni kupata habari mbalimbali kutoka katika tamasha hilo kwani mtandao huu wa http://www.stephanomango.blogspot.com,utakuwa/ makini kuwaletea wasomaji vitu murua kwa kukidhi kiu yako ya kupata matukio muhimu ya kiharakati

MIAKA 50 YA UHURU WA TANZANIA NA UFANYAJI KAZI ZENYE UCHUMI MDORORO

Akina mama ambao majina yao hayakuweza kufahamika mara moja wakiwa wamebeba miwa kwa ajiri ya kwenda kuiuza ili kuweza kujipatia kipato cha kujikimu kutokana na ugumu wa maisha unaowakabili katika jamii zao na taifa kiujumla,wananchi wengi wanaoishi pembezoni wamekuwa wakiishi katika mazingira duni kutokana na kushindwa kufaidi mgawanyo wa rasilimali za nchi