About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Thursday, December 22, 2011

DIWANI MSTAAFU GOLDEN SANGA (SANGA ONE) ATOA MSAADA WA ELFU HAMSINI KWENYE KIKUNDI CHA SANAA CHA WAZALENDO KWA AJILI YA MAANDALIZI YA UZINDUZI WA FALAMU YAO YA MAJARIBU

 Diwani Mstaafu wa Kata ya Bombambili Halmashauri ya Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma Golden Sanga maarufu kwa jina la Sanga One akimkabidhi shilingi elfu hamsini(50,000/=) Mwenyekiti wa kundi la sanaa la Wazalendo Abdalah Bin Ahmed kwa jina la kisanii Ramsh,katikati ni Mlezi wa kundi hilo Mama Ndimbo,wa kwanza kushoto ni Mhasibu wa kundi hilo Zainab Nungu kwa jina la kisanii Walda
 Diwani Mstaafu Sanga One akizungumza na kundi la wasanii la Wazalendo mara baada ya kukabidhi msaada wa fedha kwa ajili ya maandalizi ya uzinduzi wa filamu mpya ya kundi hilo,Katikati Mlezi wa kundi hilo Mama Ndimbo,wa kwanza kulia ni Mwenyekiti wa kundi hilo Abdalah Bin Ahmed-Ramsh
 Sanga One akiwa kwenye picha ya pamoja na wasanii wa kundi la Wazalendo mara baada ya kuzungumza nao hivi karibuni kwenye ukumbi wa Better Life Tanzania mjini Songea
Baadhi ya wasanii wa kundi la Wazalendo wakiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wao

KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI WA HALMASHAURI YA SONGEA CHAANZA ASUBUHI HII KATIKA JENGO LA MAENDELEO

 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Beatrice Msomisi akiwasalimia wajumbe wa Baraza la Madiwani
 Kutoka kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Peramiho Jenista Mhagama,Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Beatrice Msomisi,Mwenyekiti wa Halmashauri ya Songea Rajabu Mtiula,Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Andrwe Mhagama
 Madiwani wa Halmashauri ya Songea wakiendelea na kikao chao kilichofanyika kwenye ukumbi wa jengo la Maendeleo(Mnara wa saa)
Wataalamu na wakuu wa idara mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea wakisikiliza kwa umakini hoja mbalimbali zinazoendelea kuwasilishwa kwenye kikao hicho