About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Sunday, November 27, 2011

MAWAKALA WA KUSAMBAZA PEMBEJEO ZA KILIMO TUNDURU WAPATIKANA

                 Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Juma Madaha
Na,Augustino Chindiye TunduruKAMATI inayosimamia ugawaji wa pembejeo za Ruzuku Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma imeteua Mawakala Sita watakao husika katika zoezi la usambazaji wa Mbolea na Mbegu za Mfumo wa Vocha zitakazo tumika katika msimu huu.

Sambamba na kamati hiyo kuwateua mawakala hao baada ya Kampuni zao kufikia viwango vilivyo ainishwa na Wizara husika Mawakala hao wametakiwa kuhakikisha kuwa wanatimiza maelekezo waliyopewa yakiwemo ya kuhakikisha kuwa wameleta Pembejeo hizo kabula ya Desemba 10 mwaka huu na kuanza kuzisambaza katika vijiji vyote vya Wilaya hiyo kabla mvua hazija aanza kunyesha vinginevyo nao watafutwa

Katika zoezi hilo pia kamati hiyo inayo ongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Juma Madaha pia imewafuta uwakala Mawakala 11 bada ya kampuni zao kushindwa kufikia viwango vilivyo bainishwa na Wizara ya Chakula,viwanda na biashara.

Akizungumzia taarifa hiyo Mwenyekiti wa kamti hiyo aliwataja Mawakala walioteuliwa kutoa huduma hiyo kuwa ni Zuberi Namahala, Crispin Mumba, Halima Luambano,Joseph Kalaliche,Augustino Lukosi na Alli Chimwala ambao pamoja na mambo mengine kamati hyo ilijiridhisha kuwa kampuni za wafanyabiashara hao zimekuwa zikifanya kazi hiyo muda wote ikiwa ni tofauti na Mawakala waliofutwa

Dc Madaha aliendelea kueleza kuwa wengi wa mawakala waliofutwa kwa sababu ya kukosa sifa baada ya kamati hiyo kubainika kuwa kampuni zao kutokuwa na ofisi wala maduka ya kutolea huduma hali iliyosababisha wafanyabiahsara hao kujitokeza wakati wa kutafuta Vocha tuna si kutoa huduma kwa wakaulima.

Katika taafa hiyo Dc Madaha aliwataja mawakala hao kuwa ni
Michael Mdete ambaye pamoja na kukosa Duka la kuuzia Pembejeo hizo lakini alikosa sifa kutokana na kuwa na kesi mahakamani baada ya kubainika kuchakachua kwa kugushi na kujipatia Vocha wakati akiwa hajatoa huduma husika kwa waklima.

Wengine ni Bernadetha Methodi Pili aliyekosa sifa za uwakala
kutokana na kuwa ni mke wa Afisa kilimo msaidizi wa Wilaya hiyo ambaye pia ndiyo mratibu mkuu wa huduma hiyo kwa Wakuliwa wa Wilaya hiyo, Craudio Kiwone anaye kabiliwa na tuhuma za kusambaza Mbengu za kienyeji kwa wakulima badala ya mbegu Bora katika msimu uliopita.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo Mawakala wengine walifutwa ni Hadini
Ngunguni,Haridi Kalisinje,Yusuph Kapindo, Mjesye Mjesye,Mohamed
Limbe,Kiyonjo Hasan, Reheme Kalengo na Mchekenae ambao walikosa nafasi hiyo kutokana na kutokuwa na maduka ya kuuzia pembejeo hizo

Akizungumzia mahitaji ya Pembejeo kwa Wakulima wa Wilaya hiyo Afisa Kilimo na Mifugo wa Wilaya ya Tunduru Chiza Marando alisema kuwa jumla ya tani 12 elfu za Mbolea za kupandia na kukuzia pamoja na Tani 400  za Mbegu Bora za mpunga na mahindi ili kukidhi mahitajika kwa Wakulima wa Wilaya hiyo na kuzisambaza  kabla ya kipindi cha mvua

Mwisho

PIKIPIKI ZA MCHINA ZAENDELEA KUWAMALIZA WATANZANIA NA WENGINE KUACHWA WAKIWA WALEMAVU

Kamanda wa Polisi Mkoani Ruvuma Michael Kamuhanda Na,Augustino Chindiye Tunduru

MKAZI wa Mjini Tunduru Ramadhani Namadogo (31 ) amefariki dunia baadaya kupata ajali mbaya ya pikipiki aina ya SANLG  yenye namba za usajiri T310 BVM ambayo ilidaiwa kuwa ikiiendesha mwenyewe.

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema kuwa katika tukio hilo pia ajali hiyo ilimjeruhi rafiki wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Mussa Saanane(27) ambaye hivi sasa amelazwa katika Hospitali ya serikali ya Wilaya ya Tunduru kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Mashuhuda hao waliendelea kueleza kuwa ajali hiyo ilitokea katika mta wa Lambayi Mjini hapa wakati marehemu huyo akirejea nyumbani kwake akiwa anatokea katika maeneo ya Kadewelere ambako ilidaiwa kuwa yeye na majeruhi walienda kupata kinywaji ili kujiliwaza kutokana na ugumu wa maisha.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda
amedhibitisha kuwepo kwa tukio hilo na kueleza kuwa chanzo cha tukio hilo ni ulevi na kwamba uchunguzi wa Polisi umebaini kuwa Pikipiki hiyo aambayo ilikuwa ni mali ya Marehemu ilikuwa ikiendeshwa na Majeruhi ambaye kwa sasa yupo chini ya ulinzi wa Jeshi hilo.

Akiongea kwa shida majeruhi huyo ambaye amelezwa kitanda namba 12 katika Wodi ya Wanaume katika hospitali hiyo mbali nakukiri kuwa wakati ajali hiyo ikitokea walikuwa wamelewa alikanusha kuwa wakati ajali hiyo inatokea Pikipiki hiyo ilikuwa ikiendeshwa na marehemu pia alikiri kuwa yeye aliendesha pikipiki hiyo wakati yeye na marehemu
wakielekea Kadewele.

Akizungumzia tukio hilo Mganga mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Tunduru Dkt. George Chiwangu alisema kuwa kifo hicho kilisababiswa na kutokwa na damu nyingi zilizotokana na kitendo cha kupasuka kwa fuvu la kichwa.

Kuhusu hali ya majeruhi Saanane alisema kuwa hali yake inaendelea vizuri ingawa taarifa zinaonesha kuwa anahitaji kukaa chini ya uangalizi wa maafisa tabibu kwa muda mrefu ili kunusuru maisha yake kufutia majeraha mabaya aliyoyapata kichwani.

Msemaji wa familia hiyo Kaka wa Marehemu Seiph Namadogo alisema
kuwa kifo cha ndugu yake huyo ni cha kawaida na kwamba kinacho
wasikitisha wanafamilia wote ni kitendo cha marehemu kuuza nyumba na kununua piki piki hiyo ili aitumie kwa ajili ya kusanyia abiria akidai kuwa ingeweza kumsaidia kujikwamua kiuchumi kumbe alikuwa anakaribisha umauti wake.

Mwisho