About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Tuesday, January 31, 2012

VIONGOZI WA UWT WATAKIWA KUWASHIRIKISHA WANACHAMA KATIKA CHAGUZI ZAKE

                        KATIBU WA UWT MKOA WA RUVUMA MARIAM YUSSUF
Na Stephano Mango,Songea
WATENDAJI na viongozi wa Jumuiya ya Wanawake ya Chama cha Mapinduzi mkoa wa Ruvuma wametakiwa kuwahamasisha na kuwashirikisha kikamilifu wanachama wa Jumuiya hiyo iliwaweze kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali ndani ya chama
Wito huo umetolewa jana na Katibu wa Jumuiya ya Wanawake Tanzania(Uwt) Mkoa wa Ruvuma Mariam Yussuf wakati akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake kuhusu mchakato wa uchaguzi wa Jumuiya za Chama cha Mapinduzi
Yussuf alisema kuwa viongozi wa Uwt  kupitia vikao halali vya Jumuiya wanapaswa kuwahamasisha wanachama kushiriki katika uchaguzi kwa kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kwani wanawake wanaweza hata bila kuwezeshwa
Alisema kuwa wanachama wanatakiwa waendelee kuhudhuria vikao na mikutano inayowahusu ili kuweza kutumia haki stahiki ya kidemokrasia kwa kuomba kuchaguliwa au kuchagua viongozi bora watakaotuvusha wakati huu mgumu
Alieleza kuwa Jumuiya ya Uwt tayari imeshawatangazia wanachama wake utaratibu wa uchukuaji wa fomu za kugombea nafasi za uongozi kuanzia ngazi za matawi,kata,wilaya,mkoa na Taifa ili wale wenye sifa za uongozi waweze kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi mbalimbali za uongozi
Alieleza zaidi kuwa wanaotaka uongozi ni vema wasifanye kampeni kabla ya wakati kwa kuanza kurushiana maneno machafu,kwa kutoa rushwa kwani kwa kufanya hivyo kutasababisha kuleta uadui na ustawi wa jamii na jumuiya ya Uwt na Ccm kwa ujumla hivyo tuepukane na vitendo hivyo
MWISHO

WAKULIMA SONGEA WATAKIWA KULIMA KWA WINGI NA KWA KUZINGATIA KANUNI BORA ZA KILIMO


Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu akiongea na watendaji wa vijiji vya Magagula.Muungano Zomba na Lugagara wilaya ya Songea jana alipotembelea kuhamasisha wakulima kuzalisha mahindi kwa kuzingatia kanuni bora za kilimo.Wengine ni Mkuu wa Wilaya ya Songea Thomas Sabaya(kulia) na mwenyekiti wa Halmashauri ya Songea Rajab Mtiula(Picha na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Ruvuma)




Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu (mwenye kaunda suti nyeusi) akisikiliza maelezo ya kilimo kutoka kwa Mkuu wa wilaya ya Songea Thomas Sabaya (kulia) wakati wa ziara ya kukagua usambazaji wa pembejeo kijiji cha Lugagara wilaya ya Songea


Wakulima wa kijiji cha Magagula wilaya ya Songea wakimsikiliza mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu (hayupo pichani) jana alipofanya ziara ya kukagua shughuli za kilimo
Na Revocatus A.Kassimba,Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma
SERIKALI imewataka wakulima  mkoani Ruvuma kulima kwa wingi mahindi katika msimu huu kwa kuzingatia kanuni bora za kilimo licha ya changamoto za soko lililowakabiri msimu wa kilimo uliopita.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu wakati wa ziara yake katika vijiji vya Magagula, Lugagala na Muungano Zomba vilivyopo wilaya ya Songea .
Mwambungu aliwaeleza wananchi kuwa serikali inatambua kero ya ununuzi wa mahindi iliyotokea msimu wa 2011/2012 ambapo wakulima wengi walichelewa kupokea fedha zao kutoka Wakala wa Hifadhi za Chakula (NFRA).
Aliongeza kusema kuwa changamoto ya fedha za wakulima hazitajitokeza tena msimu ujao kwani tayari serikali imejiandaa kwa kutengwa fedha katika bajeti ili kuhakikisha mahindi yote yatanunuliwa kwa wakati.
“Limeni kuliko mwaka jana kwani serikali imejipanga kununua kwa wakati na kuhakikisha kuwa hakuna mkulima atakayecheleweshewa malipo na serikali” alisema Mwambungu na kuongeza kuwa hakuna mkulima sasa anayeidai serikali wote wamelipwa.
Mkuu wa mkoa Mwambungu alisisitiza kuwa serikali inafanya kila linalowezekana kuondoa kero ya kukopa mahindi ya wakulima hivyo ni vema wakulima wakaendelea kuunga mkono juhudi hizi za serikali kwa kuongeza uzalishaji.
Katika msimu 2011/2012 wa kilimo kwa mujibu wa taarifa za Wakala wa Hifadhi ya Chakula jumla ya tani 50,018 za mahindi zimenunuliwa kutoka kwa wakulima mkoani Ruvuma zenye thamani ya shilingi bilioni 17.5 ambapo kilo ilinunuliwa kwa shilingi 350.
Mkuu wa Mkoa alitumia fursa hiyo kuwapongeza wakulima wa vijiji hivyo alivyovitembelea kwa kutumia vema pembejeo za ruzuku kwa mfumo wa vocha kwani wameongeza uzalishaji wa mahindi na kuifanya wilaya ya Songea kuongoza katika kuzalisha mahindi mkoani.
Ziara ya Mkuu wa mkoa ilihusisha pia kukagua zoezi la ugawaji wa vocha za pembejeo ambapo kwa mujibu wa taarifa ya iliyotolewa na Mkuu wa wilaya ya Songea Thomas Sabaya alisema wilaya imepata mgao wa vocha 64,417 ambazo zimesambazwa kwa wakulima.
Sabaya alisema vocha hizo zinahusisha mbegu bora za mahindi, mbolea ya kupandia na mbolea ya kukuzia ambapo bei ya mfuko wa mbolea ya kupandia (DAP) inauzwa shilingi 80,000/=huku mkulima akichangia shilingi 52,000/=.
Kuhusu mbolea ya kukuzia (UREA) mfuko unauzwa shilingi 72,000/= na mkulima anachangia shilingi 52,000/= huku serikali ikilipia zinazobaki na kwa mbegu bora mfuko unauzwa shilingi 40,000/= huku mkulima akichangia 20,000/= na serikali zinazobakia.
Kwa upande wake Afisa Mtendaji wa kijiji cha Lugagara Bi Taifa Mahundi katika risala yake alisema wakulima wana changamoto kubwa ya upungufu wa vocha za ruzuku hivyo akaiomba serikali kuongeza mgao kwa kijiji.
Mkuu wa mkoa akijibu hoja hiyo aliwafahamisha wananchi kuwa vocha zinazotolewa ni vigumu kufanana na idadi ya wakulima kwani hiyo ni ruzuku itolewayo na serikali kuwasaidia wakulima kujenga uwezo wa kujitegemea.
Katika msimu huu wa kilimo mkoa wa Ruvuma umepatiwa vocha za ruzuku ya pembejeo za kilimo 192,000 ambapo kwa mwaka uliopita ulipatiwa vocha 204,000 hivyo kuwa na upungufu wa vocha 12,000/=.
Mkoa wa Ruvuma ni kati ya mikoa sita maarufu kwa uzalishaji wa mahindi nchini ambapo mikoa mingine ni Iringa, Mbeya, Rukwa, Kigoma na Morogoro.
…………………………………………………………………………………………………
Revocatus A.Kassimba
Afisa Habari
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Ruvuma

WAKAMATWA NA KILO 350 ZA BANGI NA KILO 112 ZA MBEGU ZA ZAO HILO

KAMANDA WA POLISI MKOA WA RUVUMA MICHAEL KAMUHANDA

Na, Mwandishi Wetu,Tunduru

KIKOSI maalumu cha Oparesheni zuia uharifu cha Polisi Wilayani
Tunduru Mkoani Ruvuma kimewakama watu watatu kwa tuhuma za kukutwa na kilo 350 za bangi zikiwa tayari kwa ajili yakusafilishwa na kusambazwa sehemu mbalimbali za masoko ya walaji.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda alisema kuwa
tukio hilo limefanikiwa kufuatia taarifa zilizotolewa na raia wema na kufanikisha kuwanasa watu hao ambao miongoni mwao yumo mtuhumiwa wa usambazaji wa madawa hayo katika sehemu mbali mbali za vijiji vilivyopo Wilayani humo.

Kamuhanda alisema kuwa Sambamba na tukio hilo pia watuhumiwa hao walikutwa na kilo 112 za mbegu za bangi ambazo zinadaiwa pia zilikuwa katika harakati za kusafirishwa zikiwa ni juhudi za wakulima wa zao hilo kujidhatiti hasa kipindi hiki
cha kilimo ili kukidhi mahitaji ya soko lao.

Kamanda Kamuhanda aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Adam Mkwanda
(33), Mkwanda Said (29) wakulima wakazi wa Kijiji cha Mpanji Wilayani humo pamoja na Mfaume Alli Mpwanda mnunuzi na msambazaji wa Bangi mkazi wa Kijiji cha Mchoteka Wilayani hapa.

Kamuhanda alifafanua kuwa katika tukio hilo watuhumiwa hao walikutwa wakiwa wamehifadhi shehene hiyo ya bangi katika maghala ya kuhifadhia chakula kukiwa na viroba 6 vilivyo kuwa vimejazwa madawa hayo vikiwa tayari kwa ajili ya kusafirishwa.

Kufuatia hali hiyo kamanda kamuhanda akatumia nafasi hiyo kutoa wito kwa wananchi kulisaidia jeshi hilo kutoa taarifa za matukio ya uhalifu na kwamba hivi sasa wamejipanga kuhakikisha watoa taarifa wanalindwa zikiwa ni juhudi za kutekeleza kwa vitendo maelekezo ya elimu ya ulinzi shirikishi yanayotolewa na jeshi hilo.

Alisema watuhumiwa hao wanatarajiwa kufikishwa mahakama baada ya kukamilika kwa tatratibu za upelelezi ili sheria
iweze kufuata mkondo wake.

Wakati hayo yakijiri uchunguzi unaonesha kuwa wakulima wengi Wilayani humo wamekuwa wakishawishika kulima zao hilo kutokana na kivutio cha bei ambayo hutolewa na wafanyabiashara wake huku kukiwa na wimbi kubwa la ongezeko la watumiaji wa madawa hayo ambayo hudaiwa kuwapatia stimu.

Kwa mujibu wa uchunguzi huo Debe moja la bangi linauzwa kati ya Tsh.20,000/= na 30,000/=  ikiwa ni tofauti na Bei ya mahindi ambayo debe moja hivi sasa linauzwa kwa bei ya 7,000/=.

Mwisho

WAKULIMA WA KOROSHO WATAKIWA KUWA NA SUBIRA WAKATI SOKO LA MAZAO YAO LINATAFUTWA

   MKUU WA MKOA WA RUVUMA SAID MWAMBUNGU

Na Augustino Chindiye,Tunduru

WAKULIMA wa Korosho Nchini wametakiwa kuwa na subira wakati serikali ikiendelea kutafuta suluhisho la kudumu la upatikanaji wa soko la uhakika wa zao

Hayo yamesemwa jana na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said
Mwambunmgu wakati akiongea na Madiwanai wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Mkoani humo na kuongeza kuwa hali hiyo imetokana na Serikali kubaini tatizo la ubabaishaji wa Soko la Mazao hayo katika msimu wa Mwaka 2011/2012 hali inayo tishia wakulima kupata malipo ya pili.

Sambamba na ahadi hiyo pia Mkuu huyo wa Mkoa wa Ruvuma amewaahidi wakulima wa mazo hayo kuwa kauli ya serikali juu ya Suluhisho la kupatikana kwa Soko la uhakika litatolewa katika kikao kitakachoketi February 2 Mwaka huuu Mjini Dodoma  na kuwahushisha Wakuu wa Mikoa Mitano inayao lima Korosho nchini.

Akifafanua taarifa hiyo Mkuu wa Mkoa huyo alisema kuwa kikao hicho ambacho Mgeni Rasmi atakuwa Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Prof.Jumanne Maghembe, Pia kitawahusiha Maafisa Kilimo wa Mikoa na Wilaya husika, wadau na viongozi wa vyama vya Ushirika katika Wilaya na Mikoa hiyo.

Mwambungu aliitaja Mikoa itayaohusika katika Mkutano huo kuwa ni
Ruvuma, Mtwara, Lindi,Pwani na Morogoro ambayo alidai kuwa pamoja nautekelezaji wa majukumu yao ya kawaida pia kwa pamoja wameapa kutolifumbia macho suala la ubabaishaji wa soko la mazao hayo kutoka kwa wakulima zikiwa ni juhudi za kuwarudishia ari wakulima baada ya kuhakikishiwa upatikanaji wa soko la mazao yao.

Kufuatia kuyumba kwa soko la zao hilo Mkuu wa Mkoa huyo akatumia
nafasi hiyo kuwataka viongozi wa Wilaya ya Tunduru kubuni mikakati mbalimbali ya kuwainua wananachi kwa kuwahimiza Wakulima kulima kwa wingi za la Mpunga na kulitumia kwa chakula na Biashara likiwa ni mbadala wa zao la Korosho.

Alisema Wilaya ya Tunduru ambayo ni kati ya Wilaya tano zilipo Mkoa Ruvuma ni tajiri wa rasilimali ardhi ambayo imesheheni Mito na mabonde yanayo tiririsha maji kipindi cha mwaka mzima na kwamba endapo viongozi watajipanga vyema katika kuwawezesha wakulima kwa kuwawekea miundombinu ya uhakika wataweza kuwaondoa katika mawazo mgando ya utumwa wa kutegema zao moja tu ambalo linaonekana kubezwa na walaji wakati huo wakiwa na mahitaji nalo.

Nao Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Juma Madaha na Mkurugenzi mtendaji
wa Halmashauri hiyo Efraemm Ole Nguyaine walisema kuwa pamoja na
maandalizi ya miundombinu inayoendelea kutekelezwa pia Wilaya hiyo imekwisha jenga Skim 4 za umwagiliaji imenunua matrekta madogo zaidi ya 200 na kuyasambaza katika vikundi vijijini zikiwa ni juhudi za dhati katika utekelezaji wa kauli mbiu ya Kilimo kwanza.

Kwa upande wao baadhi ya Madiwani ambao walitaka majina yao yasitajwe gazetini ambao mbali na kukiomba kikao hicho kutoa kauli yenye maslahi kwa Wakulima walionesha mashaka
makubwa kuwa kikao hicho si lolote kwa madai ya kuwepo kwa fufunu za wanunuzi “kuiweka” kiganjani Serikali hali inayo wafanya kuwa na kiburi cha kuiyumbisha watakavyo huku viongozi wake wakishindwa kutoa kauli.
Mwisho