About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Wednesday, February 29, 2012

WAHUKUMIWA KUTUMIKIA KIFUNGO CHA MIAKA 11 JERA

Na, Augustino Chindiye Tunduru

MAHAKAMA ya hakimu mkazi mfawidhi wa Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma imewahukumu watu wawili kutumikia kifungo cha miaka 11 jela baada ya
kupatikana na hatia katika matukio tofauti ya wizi.

Akitoa hukumu hizo kwa nyakati tofauti Hakimu wa Mahakama hiyo Geofrey Mhioni alisema kuwa anatoa adhabu hiyo baada ya Mahakama hiyo kuridhishwa na ushahidi uliotolewa na upande wa walalamikaji.

Waliohukumiwa kutumikia adhabu hiyo ni Michael Lukas (31) aliyehukumiwa kutumikia  kifungo cha miaka 5 jela baada ya kupatikana na hatia katika  Shauli la Jinai Namba 119/2011 la tuhuma za wizi wa kuaminiwa kinyume na kifungu namba 273 (B) cha sheria.

Katika shauri hilo Lukas alikuwa anatuhumiwa kuiba Pikipiki yenye namba za usajiri T175 BQU mali ya Said Yasini ambaye alimuazima kwa madai ya kutaka kumpeleka mkewe katika hospitali ya Misheni ya
Mbesa kwa ajili ya kupatiwa matibabu na kwenda kuiuza kwa Shilingi 800.000 katika kijiji cha Londo Mkoani Lindi.

Akifafanua hukumu hiyo Mhini alisema kuwa katika kuonesha nia mbaya mtuhumiwa huyo pia alishirikiana na Mtu aliye muuzia na kufaniliwa kubadilishwa namba za usajiri wa pikipiki hiyo kuwa nmaba
T434 BEE .

Katika tukio la pili aliyehukumiwa na mahakama hiyo ni Salm haji (29) aliye kuwa anakabiliwa na shauli la Jinai namba 153/201 na kupatinana na  hatia katika makosa ya Kuvunja nyumba kinyume na Sheria namba 294
(2)cha kanuni ya adhabu  sura ya 16.ambapo alikiri kosa hili alihukumiwa kutumikia kifungo cha miaka 6 jela na kosa la wizi kinyume na kifungu namba 265  pamoja na kifungu cha 258 cha kanuni ya adhabu kosa ambalo alihukumiwa kifungo cha miaka 5 jela na kuelezwa kuwa
adhabu zote zinaenda kwa pamoja.

Awali akiwasomea mashauri hayo Mwendesha mashtaka mkaguzi msaidizi wa Polisi ASP Alfred Kasolo alisema kuwa Mtuhumiwa Lukasi alifanya kosa
hilo Septemba 12/2011 huku mtuhumiwa wa shauli la jinai namba 153 /2011
Haji yeye alitenda kosa hilo Nov 12 2011 ambapo alivunja na kuiba
mali yenye thamani ya Shilingi 126,0000 katika nyumba ya  George
Komba.

Mbali na kutokuwa na kumbukumbu za  makosa ya nyuma kwa watuhumiwa hao
baada ya mahakama kuwatia hatiani ASP Kasolo aliiomba mahakama hiyo
kutoa adhabu kali ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye tabia za
aina hiyo.

Wakitoa utetezi wao kabla ya kupewa kwa adhabu hiyo watuhumiwa hao kwa
nyakati tofauti Haji aliiomba mahakama hiyo impatia adhabu ndogo
kutokana na afya yake kusumbuliwa na kifua kikuu, huku mtuhumiwa Lukas
akiomba aonewe huruma kutokana na kusumbuliwa na vidonda vya tumbo.

Mwisho