About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Saturday, January 14, 2012

WAKULIMA WA TUMBAKU WALALAMIKIA MBOLEA YENYE KIWANGO DUNI

  Na Stephano Mango, Songea
 WAKULIMA wa zao la tumbaku wa wilaya za Songea na Namtumbo mkoani Ruvuma wameulalamika uongozi wa chama kilele (APEX ) ya tumbaku na Chama Kikuu cha Ushirika cha  Songea na  Namtumbo ( SONAMCU)  kwakuwaletea mbolea ambayo iko chini ya kiwango  na kuwasababishia hasara kubwa wakulima wa zao hilo.
 
  Wakizunguza na wandishi wa habari mjini Songea wakulima zaidi ya 20  ambao waliongozwa na Salum Brashi ambaye ni Mkulima toka Chama cha  Ushirika cha Msingi cha Mnazini kilichapo  Wilayani  Namtumbo walisema kuwa  katika kipindi cha mwaka 2009/2010  na 2010/2011  wakulima wa zao hilo walipata hasara  kubwa baada ya kutumia mbolea hiyo na kusabisha kuzalisha tumbaku isiyo kuwa na ubora.
 
 
Wakulima hao walieleza zaidi kuwa hali hiyo ya kutumia mbolea ambayo ipo chini ya kiwango jambo ambalo wamekuwa wakitumia nguvu kubwa isiyo kuwa na tija katika uzalisha wa zao hilo na kuwafanya hali zao   kuwa duni kimaisha na kuendelea kuwadhofisha kiuchumi .
 
 
Walifafanua kuwa   mfano kwa kawaida mbolea aina ya NPK 20.10.10   ambayo ndio inayofaa kwa zao la tumbaku wao badala yake walileta mbolea aina ya NPK 1.2.10.10 na msimu wa 2010/2011 ililetwa mbolea aina 6.10.10 badala ya mbolea iliyozoeleka ya NPK 20.10.10.
 
Walisema kwakuwa mbolea hiyo iliyoletwa haikuwa na nitrogen 20 ndio maana  tumbaku hiyo ilikosa nikotin (sumu)  hivyo wameiomba Serikali kuchua hatua za haraka za  kuwasiliana na Uongozi wa chama kilele (APEX)  ya tumbaku na Chama Kikuu cha Ushirika  cha Wilaya ya Songea na Namtumbo (SONAMCU)  kuhakisha kuwa wanaleta mbolea inayofaa kwa zao hilo.
 
 
Aidha wakulima hao wameiomba Serikali ione umuhimu wa kuzuia  mbolea ambayo kwa hivi sasa imeifadhiwa kwenye maghala ikisubili kusambazwa kwa wakulima wa zao la tumbaku wakihofia kuwa mbolea hiyo haina sifa  kama iliyo letwa kwa misimu miwili ya kilimo iliyopita na badala yake ichukuliwe sampuli kwenda kupima kwenye maabara ya mkemia mkuu ,TBS na maabara nyingine zilipo hapa nchini  ambazo zitaweza kubaini ukweli huo.
 
 
Kwa upande wake Meneja shughuli wa Chama Kilele (APEX) ya tumbaku yenye makao makuu mkoani Morogoro Samuel Jokeya akizungumza na waandishi wa habari jana mjini Songea alisema kuwa wakulima  wa tumbaku  wa Wilaya ya Songea na Namtumbo wamekuwa na malalamiko kuwa Vyama APEX  na SONAMCU vimekuwa wakileta mbolea kwa wakulima ambayo iko chini ya kiwango jambo hilo ambalo alidai siyo la kweli.
 
Jokeya  alisema kuwa  malalamiko ya wakulima wa zao la tumbaku kuwa haifai kwa matumizi ni gumu na halina udhibitisho kwani  wakulima inawezekana hawazingatii kanuni bora za wataalum wa zao hilo na matumizi ya za duni za kilimo.na kwamba  utatuzi wa jambo hili unafanyika huku akiwa ameshauri  maabara zilizopo kupima vipimo vyote wanavyo pelekewa badala ya vichache nakuomba kupewa  cheti kinachothibitisha ubora wa mbolea inayoletwa.
 
Alifafanua kuwa chama chake kinaleta mbolea kutokana na  mahitaji yanayotolewa na Vyama vya Ushirika vya msingi na amedai kwamba  endapo wanaona mbolea inayoletwa haiwafai  SONAMCU inalo jukumu la kusitisha  mahitaji ya wakulima na wakaagiza mbolea ambayo wanaona inawafaa kwa ajili ya zao hilo.
 
 
Alisema mpaka sasa tayari mbolea kwa ajili ya tumbaku ya mvuke (VFC ) imeletwa mifuko 7735, mbolea aina ya CAN imeletwa mifuko 1878 , UREA  mifuko 16394 na mbolea ya moshi mifuko 2323 .
 
 
Naye mbunge wa Jimbo la Namtumbo Vita Kawawa alipoulizwa na waandishi wa  habari kuhusiana na malalamiko alikili kupokea kero hiyo kutoka kwa wapiga kura wake na ameeleza kuwa kila Chama cha Ushirika cha msingi kina wajibu wa kutafuta pembejeo na siyo kutegemea toka kwenye Vyama vikuu ambayo vimeoneka kuwa vinaleta mbolea ambayo haifai kwa matumizi ya kilimo cha tumbaku.
 
Kawawa  ambaye pia ni Mwenekiti wa Bodi ya tumbaku nchini alieleza kuwa  kama malalamiko yanaendelea kuwepo zaidi ya mbolea hiyo ni vyema Chama Kilele APEX ya tumbaku  na SONAMCU wakatafuta njia mbadala ya kumaliza utata uliopo kati yao na wakulima  wa zao hilo.
 
 
Hata hivyo jitihada za kuwapata Maafisa Kilimo wa Wilaya ya Namtumbo na Songea  kutolea ufafanuzi  juu ya tatizo hilo ziligonga mwamba baada ya kutopatikana kwenye simu zao za mikononi.
 
Mwisho.