About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Wednesday, September 5, 2012

WATOTO WANNE WA FAMILIA MOJA WATEKETEA KWA MOTO



Na Agustino Chindiye, Tunduru

MAJONZI na simanzi vyatawala katika mji wa Tunduru na viunga vyake vyake kutoka na msiba wa kusikitisha wa watoto wanne wa familia moja ambao wamefariki dunia baada ya miili yao kuteketea kwa kuunguzwa kwa moto uliozuka katika chumba walicho kuwa wanalala.

Kufuatia hali hiyo Mama yao Mzazi Asha Hamadi aliyedaiwa kuacha Mshumaa ukiwaka na kuwafungia watoto hao amelazwa katika Hospitali ya serikali ya Wilaya ya Tunduru akiwa hajitambui kutokana na kuugua ugonjwa wa moyo.

Mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa chanzo cha moto huo ni mshumaa ambao uliachwa ukiwa unawaka huku wazazi wao wakiwa wamewafungia kwa nje na kulala chumbani kwao.

Watoto hao ambao ni marehemu kutoka katika familia ya Kipemba walitambuliwa kwa majina ya Harid Nasoro (7),Hamid Nasoro (5)Ally Nasoro(4) na Alkam Nasoro(3).

Akizungumzia tukio hilo Baba wa Marehemu hao Nasoro Hamadi alidai kuwa Watoto wake walipatwa na mkasa huo baada ya kufungiwa kwa nje na mama yao mzazi Asha Hamadi kutokana na kilichodaiwa kuwa walifanya hivyo ili kuwadhibiti wasitoke nje kutokana na utundu walio kuwa nao.

Alisema chanzo cha kuamua kulala na mshumaa huo kilitokana na watoto hao kuzowea kulala na mwanga huku siku hiyo umeme ulizima baada ya Luku yake kwisha huku kukiwa na zuio la wateja wa huduma hiyo kutoluhusiwa kununua Umene kupitia huduma za Simu, M-pesa, Nmb Mobile kama ilivyo kuwa imezoeleka.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Deusdedit Nsimeki amethibitisha kuwepo kwa tukio hilo ambapo pia alisema kuwa Polisi wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo

Kwa mujibu wa taarifa ya Mganga aliyezifanyia uchunguzi miili ya marehemu hao Dkt. Moses Nwahasunga amesema kuwa chanzo cha vifo hivyo kilitokana na miili yao kukosa hewa safi na kuungua vibaya baada ya moto huo kulipuka ndani ya chumba.

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Chande Nalicho ametuma salamu za rambirambi na kuitaka familia hiyo kuwa na subira wakati huu wa majonzi makubwa yaliyowakuta.

Msiba huo ambao uliwasisimua watu wengi na kuzusha simanzi na vilio kila kona ya mji wa Tunduru Miili ya watoto hao imezikwa katika makabuli yalipo katika mtaa wa Mabatini mjini

Mwisho