About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Monday, April 9, 2012

MWANAFUNZI WA SEKONDARI YA MSAMALA AIBIWA MALI ZA THAMANI YA SHILINGI LAKI 9.5

NA AUGUSTINO CHINDIYE,SONGEA
WATU wasiojulikana wamevunja nyumba na kuiba mali mbalimbali zenye thamani ya Sh laki 9.5 kwenye nyumba inayomilikiwa na Dainess Mgumba (17) mkazi wa eneo la Mahenge B katika halmashauri ya manispaa ya Songea mkoani Ruvuma  .
Kamanda wa polisi mkoani Ruvuma Michael Kamhanda alisema kuwa tukio hilo lilitokea aprili 3 mwaka huu majira ya saa 8 mchana huko katika eneo la Mahenge ambako Dainess ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha 3 katika shule ya sekondari ya kutwa ya Msamala aligundua kuvunjiwa nyumba yake na kuibiwa mali mbalimbali zilizokuwemo ndani .
Kamanda Kamhanda alizitaja mali zilizoibiwa kuwa ni keyboard ,DVD deck,Radio aina ya Aiwa,simu moja ya mkononi aina ya sumsung  na receiver aina ya media com vyote vikiwa na thamani ya Sh laki 9.5 na alidai kuwa watuhumiwa bado hawajakamatwa  na upelelezi wa tukio hilo unaendelea kufanywa ili kuwabaini wale wote waliohusika katika kutenda kosa hilo .
Alieleza zaidi kuwa kutokana na polisi kwa kushirikiana na sungusungu kuweka  ulinzi mkali nyakati za usiku kwa hivi sasa waharifu wamebadilisha mbinu za utendaji  wa makosa hivyo kwa sasa wamekuwa wakifanya uharifu huo nyakati za mchana ambapo alitoa mfano wa tukio hilo kuwa lilitokea wakati Dainess akiwa shuleni na aliporudi alikuta nyumba yake imevunjwa kufuli na alipoingia ndani alikuta mali zake zimeibiwa .
Alisema kuwa kwa hivi sasa polisi inaendelea kuwasaka waharifu wa tukio hilo lakini amewataka wananchi mkoani Ruvuma waone umuhimu wa kufanya dhana ya ulinzi jirani ambao utaweza kudhibiti kwa kiasi kikubwa hali hiyo ya uharifu unaofanywa na watu wanaodaiwa kuwa ni vibaka nyakati za machana .
Amewashauri viongozi wa serikari za mitaa  kwenye maeneo yao wawe na mikakati ya kuwa na dhana ya ulinzi jirani ambayo itaweza kuwakimbiza waharifu ambao walikuwa wamezoea kuiba nyakati za usiku na hivi sasa wameamua kuiba mchana baada ya kugundua kuwa zoezi la ulinzi shirikishi linalofanywa na polisi kwa kushirikiana na wananchi nyakati za usiku zimepamba moto mkoani Ruvuma.
MWISHO

AKUTWA AMEKUFA NA KUHISIWA KABLA AJAUAWA KUWA ALIBAKWA

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Michael Kamhanda
Na Gideon Mwakanosya, Songea
MWANAMKE mmoja aliyefahamika kwa jina la Mary Jonathan (23) Mkazi wa Mateka katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea Mkoani Ruvvuma amekutwa akiwa amekufa kandokando ya mto Ruvuma na inasadikiwa kuwa kabla ya kuuwawa alikuwa amebakwa na watu kadhaa wasiofahamika.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Michael Kamuhanda alisema kuwa tukio hilo lilitokea April 5 mwaka huu majira ya saa za asubuhi ambapo inadaiwa kuwa Mary alikutwa amekufa huku akiwa uchi wa mnyama pia alikutwa na jeraha upande wa kushoto wa kichwa chake.
Hata hivyo Kamanda Kamuhanda alisema kuwa Polisi inaendelea kufanya uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo ambalo bado linaonekana kuwa na utata kwani inadaiwa kuwa Mary aliondoka nyumbani kwa wazazi wake walioko eneo la Mateka kwenda Mahakama ya Mwanzo  ya Songea Mjini ambako alikuwa amekwenda kusikiliza kesi yake ya kutishiwa kuuwawa
Kwa mujibu wa baba yake mzazi wa Mary Sajent Jonathan wa Gereza la Mahabusu Songea ni kwamba Mary alitoka nyumbani April 4 mwaka huu majira ya saa za asubuhi na aliaga kuwa anaelekea Mahakamani kusikiliza kesi aliyokuwa amemfungulia mtu mmoja ambaye hakutaka kutaja jina lake anayedaiwa kuwa alimtishia kumuua kwa maneno.
Sajenti Jonathan alieleza zaidi kuwa mtoto wake tangu alipoondoka April 4 mwaka huu majira ya saa za asubuhi nyumbani kwake hakurudi hadi April 5 mwaka huu majira ya saa za asubuhi alipokutwa akiwa amekufa huku akiwa na jeraha moja upande wa kushoto wa kichwa chake.
“Ninawaambia ndugu zangu kuwa mtoto wangu Mary tangu alipoondoka juzi mpaka jana asubuhi ndiyo ameonekana akiwa ameuwawa na watu wasiofahamika na sasa hivi taarifa ya tukio hilo iko Polisi nafikiri ndiko taarifa kamili mnaweza mkazipata” alisema Sajenti Jonathan.
Alisema kuwa mwili wa marehemu hivi sasa umehifadhiwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Serikali ya Mkoa Songea na taratibu za mazishi zinatarajiwa kufanywa mara tu Polisi watakapomaliza uchunguzi wao.
 MWISHO