About


Karibu ujiunge na chuo cha kisasa cha Easy Tech.Computer kwa mafanikio yako,Walimu waliobobea katika fani hiyo wanapatikana chuoni hapo

elimak

elimak

Pages - Menu

Wednesday, October 12, 2011

MEYA ALIYECHAKACHUA MATOKEO YA UCHAGUZI CHARLES MHAGAMA AENDELEA KUFEDHEHEKA NA SASA AKATALIWA MBELE YA VIONGOZI WA MKOA WA RUVUMA

 Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Charles Mhagama anayedaiwa kuchakachua matokeo na kuitwa Meya wa Mbunge
 Mbunge wa Songea Mjini Dkt Emmanuel John Nchimbi
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu aliyesimama,kutoka kushoto Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Nachoa Zakaria,wa pili Charles Mhagama,wa pili kulia Mkuu wa Wilaya ya Songea Thomasn Oley Sabaya
Na Stephano Mango,Songea

SAKATA la Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma kumkataa Mstahiki Meya wa Halmashauri hiyo limechukua sura mpya na kusababisha kikao cha kuzungumza na Mkuu wa Mkoa Mpya wa Ruvuma Said Mwambungu kuhahirishwa kutokana na idadi ndogo ya madiwani wanaodaiwa kuwa kwenye mgomo
Hali hiyo ilijitokeza jana katika kikao maalumu cha Mkuu wa Mkoa mpya wa Ruvuma na Madiwani wa Halmashauri hiyo kilichofanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

Akizungumza kwenye kikao hicho baada ya utambulisho Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu alisema kuwa leo nilipanga kuzungumza na Madiwani wote wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea ambapo nimejulishwa kuwa idadi yao ni 27 lakini mliofika ni 16 tu
Mwambungu alisema kuwa kutokana na jambo nyeti ninalotaka kuwaeleza ni vyema kikao hichi ambacho nimekiitisha kikahahirishwa hadi pale nitakapo panga tena ili Madiwani wengi mhudhurie katika kikao hicho kwani nimejulishwa Madiwani wengine wameenda kwenye ziara ya Kamati ya Siasa ya Wilaya ya kukagua miradi iliyotekelezwa na Halmashauri hiyo

"Naomba nitoe rai kwenye kuhusu kuhahirisha kikao hichi ili kifanyike siku nyingine ambayo Madiwani wengi watapatikana hivyo nawaombeni mnikubarie rai yangu kwa lengo jema"alisema Mwambungu

Jambo hilo liliungwa mkono na Madiwani wote ambapo Mkuu wa Mkoa aliwaruhusu Madiwani kutoa maoni yoyote ili kuweza kuiboresha siku hiyo itakayopangwa kwa ajiri ya kuzungumza naye

Ndipo aliposimama Diwani wa Kata ya Bombambili Kenny Mbangala na kueleza kuwa wakati meza kuu inajitambulisha nimemsikia Diwani wa Kata ya Matogoro anajitambulisha kama Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea wakati Baraza hili katika uchaguzi wake wa Septemba 23 mwaka huu hatukumchagua yeye na uchaguzi ukavurugika

"Sina hakika kama nimemsikia vibaya Mheshimiwa Mhagama wakati anajitambulisha kwani nimesikia akijitambulisha kuwa yeye ni Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea badala ya kujitambulisha kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii na Uchumi kwa kuwa tumeharifiwa kuwa Naibu Meya Mariam Dizumba anaumwa na amelazwa hivyo tumeshtushwa na utambulisho huo"alisema Mbangala

Akichangia hoja hiyo Diwani wa Kata ya Matarawe James Makene alisema kuwa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) kina Madiwani 7 ambapo Chama cha Mapinduzi(CCM) kina Madiwani 20 ambapo siku ya uchaguzi tulimchagua Charles Mhagama kuwa Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

Ndipo aliposimama Diwani wa Kata ya Mjini Joseph Fuime na kusema kuwa siku ya uchaguzi Madiwani tulikuwepo tulikuwa 26 kwa ujumla wetu bila kuangalia itakadi ya Chama Madiwani 14 tulimkataa Charles Mhagama kuwa Mstahiki Meya ambapo Madiwani 12 walimpigia kura za ndiyo na kila mmoja anajua hilo

"Tumesikitishwa na kitendo cha kubadilisha matokeo siku hiyo ambapo uchaguzi ulivurugika baada ya Naibu Meya Mariam Dizumba kutangaza matokeo wakati Msimamizi wa uchaguzi ambaye ni Mkurugenzi Nachoa Zakaria ambaye siku ya uchaguzi alikuwepo na kumuachia mpiga kura kama Madiwani wengine Meya atangaze matokeo hayo kinyume"alisema Fuime

Alifafanua kuwa huyo mtu aliyepo mbele yetu sisi tulimkataa ingawa alikuwa mgombea pekee yake hata Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa Nachoa Zakaria anajua,yemwenye Charles anajua kuwa yeye sio Mstahiki Meya kwani hakuchaguria kila mtu anajua hilo iwe ni mfanyakazi wa Manispaa na umma wote kwa ujumla wao wanajua kuwa Charles Mhagama hakuchaguria kuwa Mstahiki Meya

Alieleza zaidi kuwa Halmashauri ya Manispaa ya Songea ipo katika wakati mgumu sana hivyo muda umefika sasa Charles Mhagama ajiudhuru nafasi hiyo aliyojipachika ili kuweza kupisha uchaguzi mwingine kwa maslahi ya wananchi wetu kwani hata yeye mwenyewe hanajua hilo na bila kufanya hivyo hakuna jambo ambalo litaendelea kutokana na sakata hili

Akizungumza baada ya sakata hilo Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu alisema kuwa yote mliyosema Madiwani nimewasikia na yanazungumzika lakini mmeyasema mahali ambapo sio pake na kwamba kwa sababu mmenikubalia kuzungumza nanyi siku nyingine basi leo tuhahirishe hadi wakati ujao
MWISHO